Mwanafalsafa

  • HOME
Home → Semua Post Berkategori Habari
Showing posts with label Habari. Show all posts
Showing posts with label Habari. Show all posts
Ajali ya gari huko south B kenya

Ajali ya gari huko south B kenya

02:02







There was a bizarre accident today morning in Hazina Estate, South B involving a Range Rover that crashed into 7 vehicles. The Range rammed into the 7 cars before tipping over. A witness, Pauline, tweeted 4 pictures from the scene of the accident at 3.02am. Just now inside Hazina Estate. Glad the victim is safe but […] The post About that bizarre car crash involving a Range Rover in South B appeared first on Hapa Kenya.





Jaji akubali rufaa dhidi ya Pistorius

Jaji akubali rufaa dhidi ya Pistorius

02:49






Kiongozi wa mashitaka aliyewasilisha kesi ya rufaa dhidi ya Pistorius

Mahakama nchini Afrika Kusini imemruhusu kiongozi wa mashitaka kukata rufaa dhidi ya kosa alilopatikana nalo hatia Oscar Pistorius la kumuua mpenzi wake Reeva Steenkamp.
Kesi hio, sasa itaanza kusikiliza katika mahakama ya juu zaidi upande wa mashitaka ukitaka Pistorius ahukumiwe kwa kumuua mpenzi wake kwa kusudi.

Oscar Pistorius
Jaji Thokozile Masipa, alisema hataruhusu rufaa dhidi ya hukumu iliyotolewa ya miaka mitano dhidi ya Oscar mwezi Oktoba.
Kiongozi wa mashitaka Gerrie Nel aliambia mahakama kuwa hukumu hio ni ndogo sana ikilinganishwa na kosa la Oscar.




MAJANGA: FILE LA KESI INAYO MKABILI MAMA LWAKATALE LAIBIWA

MAJANGA: FILE LA KESI INAYO MKABILI MAMA LWAKATALE LAIBIWA

02:06





Sakata la Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la Assemblies of God jijini Dar, Dk. Getrude Rwakatare (pichani) kufunguliwa kesi ya uharibifu wa mali katika Kituo cha Polisi cha Wazo Hill, limechukua sura mpya baada ya faili la kesi hiyo kupotea katika mazingira ya kutatanisha, huku ikidaiwa kwamba limeibwa.
Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la Assemblies of God jijini Dar, Dk. Getrude Rwakatare.

Kufuatia kudaiwa kuibwa kwa faili hilo lililopewa namba WH/RB/9029/ 2014, UHARIBIFU WA MALI, mlalamikaji, Grayson Justine Mghamba amemwandikia  barua mkuu wa upelelezi, Mkoa wa Kipolisi Kinondoni akilalamika kwamba anahisi kuna njama zinaendelea ili kumnyima haki yake.
 Taarifa zilizopatikana kutoka ndani ya Jeshi la Polisi, Kinondoni jijini Dar, zinadai kwamba Grayson alimwandikia barua mkuu huyo wa upelelezi Desemba 2, mwaka huu akiomba msaada kuhusu shitaka hilo aliloripoti polisi Novemba 20, 2014 akimtuhumu mama Rwakatare kumvunjia nyumba yake na kumpora kiwanja kilichopo eneo la Bunju B, Kinondoni.
 Sehemu ya barua hiyo ambayo Uwazi inayo nakala yake, inasomeka:
“Nasikitika kusema kuwa kila nifuatiliapo faili langu ili niweze kumjua mpelelezi wa kesi yangu, naambiwa kwamba halionekani wakati wao ndiyo waliniambia nifuatilie.”
Uwazi lilipomtafuta Grayson na kumuuliza kuhusu sakata hilo, alikiri kuandika barua hiyo na kusema kwamba amefuatilia zaidi ya siku tano kwenye Kituo cha Polisi cha Wazo Hill alikofungulia kesi hiyo lakini anaambiwa faili halionekani.
 “Nimejaribu kuwaambia kama hilo faili la kwanza limeibwa basi wafungue lingine lakini wamekataa,” alisema Grayson ambaye habari yake ya kuvunjiwa nyumba na mama Rwakatare iliripotiwa kwa mara ya kwanza na Gazeti la Uwazi wiki iliyopita ikiwa na kichwa cha habari: MAMA RWAKATARE AFIKISHWA POLISI.
Katika malalamiko yake, Grayson anadai kuvunjiwa nyumba yenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 20 na mchungaji huyo, ambayo aliijenga kwa fedha alizochukua mkopo kazini kwake.
Grayson alidai kwamba nyumba yake hiyo ilivunjwa na greda kipindi alipoenda Moshi kwenye msiba wa baba yake na kiwanja chake anachodai kukinunua kihalali kwa kuandikishana na aliyemuuzia kwenye Ofisi za Serikali ya Mtaa wa Bunju B, kuzungushiwa ukuta.
Uwazi lilipomtafuta Mchungaji Rwakatare na kumhoji kuhusu sakata hilo, alisema kwamba kiwanja hicho ni mali yake tangu mwaka 2005 na alivunja nyumba hiyo kwa sababu alikuwa akikifanyia usafi kiwanja hicho alichodai kilivamiwa.




Umuhimu wa kushirikiana katika kazi hasa ya muziki

03:24










MTOTO ANYONGWA NA BABA WA KAMBO , FUATILIA KISA HAPA

MTOTO ANYONGWA NA BABA WA KAMBO , FUATILIA KISA HAPA

03:17







Baba mzazi wa marehemu (kushoto) akiwa na waombolezaji.
“Kaka yake alifika, vurugu kubwa ikazuka, baadhi ya vitu vilipotea na kuvunjika kutokana na purukushani hiyo. “Kulipokucha Hamis akaenda kuripoti ofisi ya serikali ya kijiji ambapo mgambo walifika nyumbani na kutuchukua hadi Kituo cha Polisi Mvomero ambapo baada ya kuhojiwa tuliamriwa tumlipe Hamis shilingi laki nne kufidia hasara iliyotokea nyumbani kwake, tulilipa nusu hadi sasa tunadaiwa iliyobaki.
” UGOMVI SIKU YA TUKIO “Novemba 28, mwaka huu, siku mbili kabla ya mauaji ulizuka ugomvi tena kati yangu na Zamili  akipinga kulipa lile deni. Jumamosi tuligomba tena, alikuwa akilalamika kwamba Hamis anamlipisha fedha wakati anamtunzia mwanaye, nikamwambia kama anakereka kumtunza mwanangu anipe talaka, akagoma akidai bado ananipenda.

JESHI la Polisi Mkoa wa Morogoro linamshikilia Zamili Shabani kwa madai ya kumnyonga hadi kumuua mtoto wake wa kambo, (mwaka mmoja na nusu) huku mauaji hayo yakihusishwa na wivu wa mapenzi. 
Abdulrahman Hamis Clemensi enzi za uhai wake.
Tukio hilo la ajabu lililowaacha vinywa wazi wakazi wa eneo hilo lilijiri saa 6 mchana wa Desemba 2, mwaka huu kwenye nyumba waliopanga wanandoa hao, Zamili na mkewe, Rehema Mustafa (21) iliyopo Kijiji cha Mbogo, Tarafa ya Turiani Wilaya ya Mvomero mkoani hapa.
ALIVYOSEMA SHUHUDA Kabla ya kuzungumza na mama wa marehemu, Uwazi lilipata mawili-matatu kutoka kwa shuhuda mmoja wa tukio hilo. ”Mimi moja kwa moja namlaumu mama wa mtoto, Bi. Rehema. Awali alikuwa kwenye ndoa na mumewe Hamis, wakabahatika kumzaa Abdulrahman.
“Mwanzoni mwa mwaka huu alifika Zamili akitokea Zanzibar. Kwa taarifa tulizonazo Zamili alikuwa na ishu kubwa kule  ndiyo maana akaamua kuja huku. “Unajua vijijini, mtu akitokea mjini wanawake wanamshobokea. Dada yetu Rehema akadanganywa na Zamili akatoka kwenye ndoa yake na kuolewa naye mwezi wa saba mwaka huu.
Rehema Mustafa mama mzazi wa mtoto Abdulrahman Hamis Clemensi.
“Toka waoane kila siku ni ugomvi hadi juzi yalipotokea mauaji hayo,” alidai Said Seleman Kindu, mkazi wa kijiji hicho.   MAMA WA MTOTO SASA Baada ya kuzungumza na Said, Uwazi lilimhoji Rehema ambaye alikuwa na haya ya kusema: “Awali nilifunga ndoa na Hamis Clemensi, tukabahatika kumzaa mtoto mmoja ambaye ni huyo marehemu.
Baada ya kuachana na Hamis nilikaa nyumbani miezi mitatu, nikaja kufunga ndoa na Zamili, Julai 28, mwaka huu. “Tukio zima nahisi kama lilianzia Agosti,  mwaka huu kwani nakumbuka siku moja nikiwa sokoni nilikutana na Hamis akamsalimia mwanaye, kumbe kuna mtu alituona akaenda kumwambia Zamili.
“Aliporudi usiku tuligombana sana akitaka nimpeleke mtoto kwa baba yake, nikamwambia mwanangu bado ananyonya siwezi kumpeleka kama vipi asubiri atimize miaka mitatu nitampeleka hata kwa mama yangu mzazi.
“Licha ya kumwambia hivyo, Zamili akagoma, nikamwambia basi anipe talaka nirudi kwetu pia akakataa.”  “Siku iliyofuata, usiku alichukua kisu na kuniamuru nimpeleke mtoto kwa baba’ke,  tukatoka mimi, yeye na mtoto, lakini baba yake alipotuona alijificha juu ya dari huku akimpigia simu kaka yake anaitwa Kilimo na kumjulisha.

Hata hivyo, aliahidi kwamba atafanya mauaji.” SIKU YA TUKIO “Siku ya tukio Jumanne, saa 5 asubuhi, Zamili alinituma dukani, nikataka kwenda na mwanangu, akasema nimwache atanichelewesha, nikamwacha. “Niliporudi sikumuona mtoto, nikamuuliza Zamili mtoto yuko wapi? Akanijibu  kalala, nikaingia jikoni na kusonga ugali, tukala.
“Tulipomaliza, mimi nikaenda chumbani kumwamsha mwanangu ili naye ale. Nilishangaa kumuona kalegea. Kwa utoto wangu sikujua kama amekufa, nikaenda kuita wakubwa walipofika wakamuona mtoto kichwa kimegeukia mgongoni, wakaniambia mbona amekufa! “Palepale nikaangua kilio, watu wakajaa, baadaye viongozi wa kijiji wakaja na mgambo wakamkamata Zamili na kumpeleka polisi na mimi nikakodi bodaboda, nikabeba maiti ya mwanangu kuja hapa Mkindo kwa wazazi wangu.

Waombolezaji wakiwa msibani.
Mwanangu tumemzika jana (Alhamisi iliyopita),_nimebaki na kumbukumbu ya picha tu,” (akaanza kulia). Rehama alipotakiwa kutoa picha ya Zamili alisema: ”Huyu Zamili hana picha, hata kwenye harusi yetu aligoma kupigwa picha, nadhani alikuwa akitafutwa kule Zanzibar.
Alipoulizwa kama atakuwa tayari kuishi tena na Zamili, alisema: “Siko tayari mimi nataka talaka yangu.” BABA WA DAMU WA MAREHEMU Naye baba mzazi wa marehemu, Hamis Clemensi ambaye alikuwepo kwenye msiba huo wa mwanaye alipohojiwa na Uwazi alisema:  “Huyu jamaa ni wakuja, tulipata taarifa zake kwamba hakuwa mtu mzuri kule Zanzibar.
Alishataka kuniua mimi baada ya kunivamia kwangu usiku akiwa na mke wangu  na mtoto, eti amemleta mtoto wangu, nikapanda kwenye dari na kumpigia simu kaka yangu. Nasikitika kwa kumuua mwanangu.”





VIJANA WAMVAA  MIZENGO PINDA

VIJANA WAMVAA MIZENGO PINDA

02:04







BARAZA la Vijana la CHADEMA (BAVICHA), limeitaka Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa (Tamisemi), kutoa majibu ya haraka juu ya kuenguliwa kwa wagombea wa chama hicho katika uchaguzi wa serikali za mitaa unaotarajiwa kufanyika Desemba 14 mwaka huu.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Katibu Mkuu wa BAVICHA, Julius Mwita, alisema kuwa wagombea wa chama chao wameenguliwa katika kinyang’anyiro hicho kwa sababu zisizokuwa za kimsingi.
Alifafanua kuwa, hizo ni mbinu za Chama Cha Mapinduzi (CCM), kwa kutumia viongozi walioko madarakani kutaka kuwapitisha wagombea wao ili kuwasaidia katika uchaguzi mkuu ujao.
“BAVICHA hatuko tayari kuona uonevu wa kiasi hiki tunaufumbia macho, tunamtaka Waziri Mkuu Mizengo Pinda kutoa majibu ya haraka kuhusiana na hili kabla ya siku ya uchaguzi,” alisema Mwita.
Alitaja baadhi ya maeneo aliyopata taarifa kuwa Kamati ya Rufaa imewaengua wagombea wao ni Same, Vunjo, Njombe, Simanjiro na Mwanza.
Aliongeza kuwa, kuna baadhi ya maeneo ambayo wabunge wa CCM wanawalazimisha wakurugenzi wawaengue wagombea wa CHADEMA.
Akizungumzia miaka 53 ya Uhuru wa Tanganyika, Mwita aliwataka vijana kuadhimisha kwa kutafakari hali yao kimaisha, kwani Watanzania walio wengi bado ni masikini, hivyo ni wakati wa kufanya mabadiliko kuanzia kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa.
“Kesho ni sikukuu ya uhuru wa Tanganyika, ni wakati muafaka wa kuangalia je ndani ya miaka 53 tumeweza kupigana na adui umasikini, ujinga na maradhi huku jingine limeongezeka rushwa, hivyo basi ni wakati muafaka kwa Watanzania kufanya mabadiliko kuanzia ngazi ya kata,” alisema.





ANUSURIKA KIFO , NI BAADA YA KICHWA CHAKE KUCHIMBWA A SULULU

01:17




HAKUNA neno jingine la kutumia zaidi ya kusema; KWELI MUNGU MKUBWA! Ni miezi mitano sasa imekatika tangu kusambaa kwa picha mitandaoni zilizomwonesha mwanaume mmoja akiwa ameshindiliwa sululu kichwani huku kisa kikiwa hakijulikani.


“Kwanza kabisa napenda kusema kweli Mungu ni mkubwa, nimepona! Ingawa mwili bado hauna nguvu sawasawa lakini naendelea vizuri. “Ilikuwa tarehe 19, Julai mwaka 2013  katika machimbo ya Mgodi wa Miombo- Rwamgasa  wilayani Geita, mimi ni fundi wa kuchimba maduara yanayotumika kuchimbia dhahabu.
“Baada ya kumaliza kazi zangu majira ya jioni, nikaenda kupumzika ili kujiandaa kwa siku iliyofuata. “Nilikuwa nimepumzika na wenzangu zaidi ya mia moja, unajua tena migodini. Kufika saa 3 hivi usiku nikiwa nimeanza kusinziasinzia, nilishtukia kitu kizito kinaingia kichwani mwangu upande  wa kushoto.” ALISHINDWA KUPIGA KELELE “Nilishindwa kupiga kelele nadhani kwa sababu ya kule kusinzia. Wenzangu ambao nao walianza kulala walishtuka kwa kusikia harufu ya damu, wakaamka na kuja wakanikuta sululu ikiwa imezama kichwani.

Oka Kaombe kabla ya kufanyiwa upasuaji.
“Hii sululu kule machimbo ni maarufu kwa jina la Moko, hutumika kuchimbia madini katika migodi. Nilichukuliwa na sululu yangu kichwani na kukimbizwa Hospitali ya Rufaa ya Bugando, Mwanza  kwa ajili ya matibabu ya haraka.” SIKU NNE BILA FAHAMU Oka anazidi kusimulia: “Mengine ninayosimulia niliambiwa kwani nilipoteza fahamu kwa siku nne.
Nilianza kujitambua baada ya siku nne nikiwa palepale Bugando na kujikuta nipo hospitali lakini nilikuwa siwezi kuzungumza wala kusikia vizuri. Maumivu yalikuwa makali sana kutokana na sululu kuzama kichwani maana ilipoingia ilikwenda kutokea upande wa pili wa kichwa. “Nikiwa nimeshafanyiwa upasuaji kwa kuchomolewa sululu, niliendelea kukaa Bugando kwa siku 52.”
ATOROKA BUGANDO, AMSAKA MBAYA WAKE Oka alisema kuwa, hiyo siku ya 52 aliamua kutoroka hospitalini hapo kwa sababu alishindwa kulipia gharama za matibabu ambazo ni shilingi laki tisa (900,000). “Kiasi hicho cha pesa kwangu kilikuwa kikubwa na hata sasa bado ni kikubwa ndiyo maana niliamua kutoroka,’’ alisema Oka. ALIYEMZAMISHA SULULU AJULIKANA Oka anaendelea kusimulia:
“Nilipotoka hospitalini kitu cha kwanza nilianza kumtafuta mtu aliyenifanyia kitendo kile cha kinyama, marafiki zangu wakanipa ushirikiano  na kuniambia unyama ule ulifanywa na jamaa mmoja anayeitwa  Masha. “Huyu Masha ni mchimbaji wa madini kwenye ule mgodi lakini alikimbia baada ya kufanya tukio na mpaka sasa hajulikani alipo.”
KISA CHA KUPIGWA SULULU PIA CHAJULIKANA Oka alisema taarifa alizopata baadaye kutoka kwa wachimbaji mgodini hapo ni kwamba,  lengo la Masha kumpiga na sululu lilikuwa ni kumtoa kafara (ndagu) ili aweze kupata dhahabu nyingi na awe bilionea kwa siku za usoni. “Ila Mungu ni mkubwa alitupilia mbali wazo hilo mpaka sasa niko hai,” alisema Oka.
AFYA YAKE KWA SASA Oka alisema kwa sasa anaamini amepona kabisa kidonda chake kichwani ila hawezi kufanya kazi yoyote kutokana na mwili kukosa nguvu za kutosha.
UPASUAJI MWINGINE Aliendelea kusema kuwa, akiwa Bugando aliambiwa na madaktari kuwa anatakiwa kufanyiwa upasuaji kwa mara nyingine na kuwekewa vyuma kichwani baada ya kuwekewa vyuma hivyo itabidi akae miaka mitatu bila kufanya kazi yoyote ndipo atapata nguvu za kufanya kazi kama zamani.
MAISHA YAKE KWA SASA Oka alisema maisha yake kwa sasa ni magumu kwani ana watoto 5, lakini pia alitengana na mke wake hivyo yeye ndiye baba na mama wa familia kwani hata wazazi wake wamezeeka, hivyo wanamtegemea yeye. ANACHOWAOMBA WATANZANIA Alisema kwa sababu bado ana safari ya kujitibu na pia kutunza familia, amewaomba Watanzania wenye kuguswa na mkasa wake wamsaidie pesa kwa kiasi chochote atakachojaliwa mtu kwa kutumia simu yake ya mkononi ambayo ni 0682 013479. 





Watu waliokuwa na silaha wamevamia gereza katika mji wa Minna, katikati mwa Nigeria, na kuwaachilia huru wafungwa 200.

Watu waliokuwa na silaha wamevamia gereza katika mji wa Minna, katikati mwa Nigeria, na kuwaachilia huru wafungwa 200.

00:48





http://ichef.bbci.co.uk/news/ws/304/amz/worldservice/live/assets/images/2014/11/06/141106113053_boko_haram_nigeria_prison_304x171_.jpg
Walingia kwa nguvu kwenye jela Jumamosi katika jimbo la Niger.
Polisi wanasema haijulikani ikiwa uvamizi huo ulifanywa na kundi la wapiganaji Waislamu, Boko Haram, au gengi la wahalifu.
Boko Haram wamevamia magereza kadha katika miaka ya karibuni.





Ni aibu, mbunge anaswa akicheza game kikaoni

Ni aibu, mbunge anaswa akicheza game kikaoni

00:41





 http://ichef.bbci.co.uk/news/ws/660/amz/worldservice/live/assets/images/2014/12/08/141208081111_candy_crash_512x288_bbc_nocredit.jpg
Mbunge wa chama tawala cha Conservative nchini Uingereza , amekiri kucheza mchezo maarufu kwenye tabiti yake wakati wa kikao cha kamati moja la bunge hilo.
Jarida la The Sun, limechapisha picha za mbunge huyo kwa jina Nigel Mills akicheza Candy Crush Saga kwenye tabiti yake, wakati wa mkutano wa kamati hio kuhusu mageuzi ya sera ya serikali kuhusu malipo ya uzeeni.
Jarida hilo linasema Bwana Nigel alicheza mchezo huo kwa zaidi ya saa mbili.
Hata hivyo amejitetea akisema alifahamu kilichokuwa kinaendelea katika kamati hiyo na kwamba lihusika katika kuuliza maswali. Hata hivyo alikiri kucheza mara mbili na kusema atajaribu kujizuia kucheza mchezo huo katika siku za usoni akiwa kazini.





Mwanasheria mkuu wa serikali nchini Mexico, Jesus Murillo Karam,ametoa ahadi kuwa hakutakuwa na uonevu wowote katika kesi ya kupotea kwa wanafunzi nchi humo miezi miwili iliyopita

Mwanasheria mkuu wa serikali nchini Mexico, Jesus Murillo Karam,ametoa ahadi kuwa hakutakuwa na uonevu wowote katika kesi ya kupotea kwa wanafunzi nchi humo miezi miwili iliyopita

00:39












.
Kutoweka kwa wanafunzi hao kumesababisha maandamano ya wiki kadhaa nchini humo waandamanaji wakipinda rushwa na ukatili uliozunguuka kesi hiyo.
Bwana Karam amesema kwamba uchunguzi wa kusaka walikopotelea wanafunzi hao unaendelea mpaka hapo wahusika wa tukio hilo watakapokamatwa.
Zaidi ya hayo amethibitisha mwili wa mmoja kati ya wanafunzi hao arobaini na tatu kuwa umetambuliwa kuwa ni wa Alexander Mora,mwili uliogunduliwa katika jaa la taka katika jimbo la Guerrero.
Mwanasheria mkuu huyo wachunguzi mahiri wa miili kutoka nchini Austria wakiunganisha mifupa kwa kuifananisha na kipimo cha vinasaba vya ndugu wa marehemu huyo9,ndipo walipoutambua.





Bibi huyu adhihirisha kauli ile ya Uhuru Kenyatta kwamba usalama uanza na wewe.Ona alicho kifanya hapa

00:35











Maneno ya kizalendo ya Diamond platnum "There is no place like Home... Ever!

00:27






Japokuwa nina show Canada tareh 2 lakini ilinibidi kwanza nilete Mzigo
nlioagizwa na Wananchi Nyumbani kisha ndio nirudi kuendelea na shughuri zangu!... Kama wasemavyo
"There is no place like Home... Ever!"






Nyota ya Diamond yazidi kungara ,apokea tuzo nyingine huko Lagos Nigeria

Nyota ya Diamond yazidi kungara ,apokea tuzo nyingine huko Lagos Nigeria

00:24






tuzo
Diamond Platnumz ameshinda tuzo nyingine ambayo hizi zilikua zikitolewa Lagos nchini Nigeria ambazo hizi hazikuwa na utaratibu kama wa tuzo zingine kwa kupiga kura.

Baada ya kushinda tuzo hiyo ambayo ilienda kupokelewa na Meneja wake Salaam,Diamond alipost maneno haya>>’Thanks God,we have cheated another one on the future Awards Africa in Lagos Nigeria…#samenight Thank you Allah’
Tuzo hizi zinaitwa The Future Awards Prize in Entertainment ambapo kipengele alichokuwa akiwania Diamond alikuwa na wakali mbalimbali akiwemo Panshack au Ice Prince jina lake la zamani wa Nigeria na Michael Kwesi wa Ghana.




Kafulila ampendekeza Dk.slaa kuwa mgombea urais UKAWA, Gazeti la mwananchi leo juma tatu

Kafulila ampendekeza Dk.slaa kuwa mgombea urais UKAWA, Gazeti la mwananchi leo juma tatu

00:20










Je? Idris Sultan kuibuka kidedea?

06:45
Tangu asubuhi ya leo kupitia Runinga ya Dstv zaidi ya channel 197 inaonyesha moja ya washiriki 8 waliobaki katika mjengo huo,.huku kamera ikimmulika zaidi mshiriki kutoka Tanzania Idris Sultan jambo linaloashiria huenda Watanzania tukawa na furaha na ushindi huo mnono.
Fainali za Big Brother(Hotshots),zinafanyika leo saa 2:00 usiku,huku mshiriki huyu kutoka Tanzania akiwaongoza washiriki wenzake.
   
Kila la kheri Idris Sultan.
Wabunge wa Somali wameng'oa waziri mkuu

Wabunge wa Somali wameng'oa waziri mkuu

14:56





Ni mara ya nne kwamba kura ya kutokuwa na imani dhidi yake ilipigwa baada ya majaribio ya awali kumalizika kwa ghasia.
Waandishi wanasema kuwa serikali ilikuwa imelemazwa na uhasama baina ya kiongozi huyo na rais wa taifa hilo Hassan Sheikh Mohamud.
Wanasema kuwa usalama ulikuwa umezorotoa kutokana na hali hiyo.
Abdiweli ni waziri mkuu wa pili kuwahi kuondolewa madarakani mwaka huu.
Marekani imeshtumu kura hiyo ikisema kuwa haikuzingatia maslahi ya raia wa Somali.





Rais Robert Mugabe  anatarajiwa kuhutubia maelfu ya wajumbe katika siku ya mwisho ya mkutano mkuu wa chama tawala cha ZANU-PF mjini Harare.

Rais Robert Mugabe anatarajiwa kuhutubia maelfu ya wajumbe katika siku ya mwisho ya mkutano mkuu wa chama tawala cha ZANU-PF mjini Harare.

14:51
Rais Mugabe na mkewe, Grace
Katika hotuba yake Bwana Mugabe anatarajiwa kutangaza nani atachukua nafasi ya makamo wa rais, Joice Mujuru, ambaye ametuhumiwa kufanya ufisadi.
Waandishi wa habari wanasema aliyeelekea kuteuliwa ni waziri wa sheria, Emmerson Mnangagwa, lakini baadhi ya watu wanasema Rais Mugabe huenda akamteua mkewe, Grace, kuwa naibu wake.
Makamo wa rais ndiye huenda akarithi uongozi kutoka kwa Bwana Mugabe ambaye ametimia miaka 90.
WAISHI NA MAITI NDANI  KWA WIKI 24 WAKIAMINI ITAFUFUKA

WAISHI NA MAITI NDANI KWA WIKI 24 WAKIAMINI ITAFUFUKA

17:59




Maiti
Familia moja nchini Canada iliishi na maiti katika chumba cha juu cha nyumba yao kwa miezi sita kwa kuwa waliamini marehemu atafufuka iwapo wataendelea kumuomba mungu,lakini mwili huo ukapatikana baada ya familia hiyo kushindwa kulipa mkopo waliochukua kununua nyumba hiyo.
Kaling Wald mwenye umri wa miaka 50 alipatikana na makosa ya kushindwa kuwaarifu maafisa wa polisi kwamba mumewe alifariki ,kosa ambalo na akahukumiwa kuwekwa katika muda wa majaribio na ushauri,wakili wake alikiambia chombo cha habari cha Reuter siku ya Jumanne.
Peter Wald mwenye umri wa miaka 52 alifariki mnamo mwezi machi mwaka 2013 kwa kile mamlaka inasema ni sababu za kawaida kufuatia maambukizi ya mguu wake yanayodaiwa kusababishwa na ugonjwa wa sukari.
Mkewe Kaling Wald alimwacha kitandani na kufunga chumba hicho katika nyumba yao ya Hamilton ,Ontario ili kuzuia harufu kali iliokuwa ikitoka chumbani humo kuwafikia watu waliokuwa wakiishi nyumbani humo.
Kama vile Yesu alivyomfufua Lazaro baada ya siku ya nne ,pia yeye aliamini kwamba Mungu atamfufua mumewe wakili wa mwanamke huyo alisema.




CCM KUTOICHUKULIA HATUA AKAUNTI YA ESCROW

CCM KUTOICHUKULIA HATUA AKAUNTI YA ESCROW

17:57





Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye, alisema kuwa CCM haina mpango wa kuchukua hatua zozote dhidi ya wote waliotajwa kuhusika na kashfa hiyo kwa sababu chama hicho hakijawahi kuwajadili kwa jambo hilo ambalo siyo la chama chao bali ni la Bunge la Tanzania.

“Suala hili lipo chini ya Bunge na hivyo chama hakijaingilia kati na kuchukua hatua wabunge wake waliotajwa,” alisema Nape. Aliongeza kuwa chama hakiwezi kuchukua hatua zozote dhidi ya wabunge wake waliobainika kula fedha hizo kwani suala hilo halijawahi kufikishwa kwenye vikao vyao. “Hatujawachukulia hatua (waliotajwa), wala hatuna mpango wa kuwachukulia hatua kwa sababu suala hili haliko ndani ya CCM... liko ndani ya bunge, labda kama litaingia ndani ya chama ndiyo tutalitolea maamuzi,” alisema Nape.

Kauli ya Nape imekuja siku chache baada ya chama hicho kutoa msimamo wake dhidi ya wabunge wa chama hicho waliohusika katika sakata hilo kuwa bunge lichukue hatua stahiki. Nape, akiwa na Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana, katika ziara ya kukagua, kuhimiza na kusukuma utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya mwaka 2010/15 mkoani Mtwara, walisema kila aliyehusika katika kashfa hiyo, abebe msalaba wake.

Nape alisema chama hakiwezi kulea maovu yanayofanywa kinyume na kanuni na taratibu za chama hicho, hivyo kama bunge limebaini waliokiuka maadili wachukuliwe hatua stahiki dhidi yao. Kwa upande wake Kinana alisema muda wa kulindana na kubebana ndani ya chama umeisha na anayekiuka taratibu na kanuni za chama hicho awajibishwe na akishindikana achie ngazi.

Wabunge kadhaa kutoka CCM wakiwamo mawaziri Sospeter Muhongo wa Nishati na Madini na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka, ni miongoni mwa vigogo waliotajwa kuhusika na kashfa hiyo na hivyo Bunge kuazimia kuwa waondoshwe.

Wabunge wengine wa CCM waliohusishwa na kashfa hiyo na kutakiwa kuondolewa kwenye nafasi zao za uenyekiti wa kamati za Bunge ni Mbunge wa Bariadi Mashariki anayeongoza Kamati ya Bajeti, Andrew Chenge , Mbunge wa Sengerema, Wiliam Ngeleja (Sheria, Katiba na Utawala) na Mbunge wa Lupa anayeongoza kamati ya Nishati na Madini, Victor Mwambalaswa.





FUATILIA ZAIDIKUJUA ZAIDI MAONYESHO YA ELIMU KUANZIA DISEMBA 17-21, 2014 JIJINI DAR

17:51






Mkurugenzi Mtendaji wa Global Education Link, Abdulimalik Mollel, akisisitiza jambo kwa wanahabari (hawapo pichani)
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam.
Kampuni ya Global Education Link (GEL) kwa kushirikiana na Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI), Wizara ya Elimu na Ufundi pamoja na Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (Tantrade) wameandaa maonyesho ya kwanza ya kimataifa ya elimu (TIEE) yanayotarajiwa kufanyika Disemba 17 hadi  21 mwaka huu katika viwanja vya Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam.
Akizungumza jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mkuu wa Global link Education, Abdulmalik Mollel, alisema lengo la maonyesho hayo ni kutambulisha wadau wa elimu kwa pamoja ili kuweza kutoa huduma ya pamoja kwa wananchi na kuwaelimisha juu ya mambo muhimu yaliyopo katika kila sekta.

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (Tan Tred), Jacqueline Mneney, akizungumza jambo.

Alisema ushiriki wa asasi mbalimbali kwa kushirikiana na sekta binafsi utakuwa na chachu ya mabadiliko ya elimu kwa kupitia mpango wa matokeo makubwa sasa.

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TanTrade), Jacqueline Mneney, alisema wakati umefika kwa Watanzania kujua umuhimu wa maonyesho ya Elimu maana yamekuja kutatua matatizo mbali mbali waliyokuwa wakiyapata wazazi pindi wanapokuwa wanawatafutia shule na vyuo watoto wao.

Aidha alisema maonyesho hayo yataleta manufaa makubwa na changamoto chanya hasa katika kuongeza ushindani katika sekta ya elimu ambayo itasaidia mpango wa matokeo makubwa sasa.
Maonesho hayo yanatarajiwa kupata washiriki zaidi ya 500 na wananchi mbalimbali zaidi ya 350,000 kutoka ndani na nje ya nchi.




Older Posts
Home
Subscribe to: Posts (Atom)

HABARI ZILIZO BAMBA TOP 10

  • BRAZIL TO EDGE OUT GERMANY IN WORLD CUP SEMI FINAL
  • KAULI YA UHURU KWENYE MTANDAOWA KIJAMII (TWITTER) KENYATTA HII HAPA
    Taarifa ya mahakama ya ICC, kutupilia mbali kesi dhidi ya Uhuru Kenyatta, imepokelwa na watu wengi nchini Kenya kwa hisia mseto. Baadhi w...
  • Catalonia's regional president Artur Mas says an official referendum is needed following Catalonia vote: 80% back independence - officials
    \ An informal vote on independence for Catalonia has shown more than 80% in favour, officials say. The non-binding vote went ahead after ...
  • Ukistaajabu ya Mussa ?Nusu ya sura yake inafanana na binadamu na Nusu nyingine inafanana na CHURA, ni mtoto aliye zaliwa huko dodoma
    MKAZI  wa kijiji cha Chibwechangula –Behelo katika wilaya ya Mpwapwa mkoani Dodoma, Ruth Matonya (26) amejifungua mtoto wa ajabu ambaye nus...
  • MASKINI MSUSI WA NYWELE AKUTWA AMEKUFA GESTI ,FUATILIA KUJUA ZAIDI
    Askari polisi pamoja na baadhi ya viongozi wa Serikali ya mtaa kata ya Gongoni manispaa ya Tabora akiangalia mwili wa mwanaume ...
  • Kafulila ampendekeza Dk.slaa kuwa mgombea urais UKAWA, Gazeti la mwananchi leo juma tatu
  • In long, dimly lit hallways, clusters of people wait anxiously outside courtrooms for their cases to come before a judge.
    The New York Immigration Court is an extraordinarily busy place. In long, dimly lit hallways, clusters of people wait anxiously outside co...
  • ZITHO "SHARTI MOJA , NARYDI CHADEMA"
    MBUNGE wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe (CHADEMA), amesema kuwa mwanasiasa yeyote makini kutoka vyama vya upinzani mwenye dhamira ya ku...
  • The New York clinic where Joan Rivers suffered a cardiac arrest during a medical procedure failed to follow standard protocols while treating her.Clinic cited for multiple failings
    Joan Rivers had been sedated during the procedure examining the back of her throat The comedian died on 4 September, aged 81,...
  • IT 'S MATTER OF FEW MINUTES FOR WORLD CUP 2014 START SHINNING !!!!
    The World Cup  The 2014  Brazil™ is now just a matter of minutes away and to mark the occasion FIFA have launched an updated version of th...

LABELS

  • Breaking News
  • condolonces
  • Entertainment
  • Entertainments
  • Habari
  • Majonzi
  • Michezo
  • News
  • News and Updates
  • Skendo
  • Sports and Games
Submit ExpressSEO Services & Tools

Total Pageviews

Copyright 2014 Mwanafalsafa
Template By Ridwan Hex And Game Gratis