Mwanafalsafa

  • HOME
Home → Habari → MAJANGA: FILE LA KESI INAYO MKABILI MAMA LWAKATALE LAIBIWA

MAJANGA: FILE LA KESI INAYO MKABILI MAMA LWAKATALE LAIBIWA

Habari
Wednesday, 10 December 2014





Sakata la Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la Assemblies of God jijini Dar, Dk. Getrude Rwakatare (pichani) kufunguliwa kesi ya uharibifu wa mali katika Kituo cha Polisi cha Wazo Hill, limechukua sura mpya baada ya faili la kesi hiyo kupotea katika mazingira ya kutatanisha, huku ikidaiwa kwamba limeibwa.
Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la Assemblies of God jijini Dar, Dk. Getrude Rwakatare.

Kufuatia kudaiwa kuibwa kwa faili hilo lililopewa namba WH/RB/9029/ 2014, UHARIBIFU WA MALI, mlalamikaji, Grayson Justine Mghamba amemwandikia  barua mkuu wa upelelezi, Mkoa wa Kipolisi Kinondoni akilalamika kwamba anahisi kuna njama zinaendelea ili kumnyima haki yake.
 Taarifa zilizopatikana kutoka ndani ya Jeshi la Polisi, Kinondoni jijini Dar, zinadai kwamba Grayson alimwandikia barua mkuu huyo wa upelelezi Desemba 2, mwaka huu akiomba msaada kuhusu shitaka hilo aliloripoti polisi Novemba 20, 2014 akimtuhumu mama Rwakatare kumvunjia nyumba yake na kumpora kiwanja kilichopo eneo la Bunju B, Kinondoni.
 Sehemu ya barua hiyo ambayo Uwazi inayo nakala yake, inasomeka:
“Nasikitika kusema kuwa kila nifuatiliapo faili langu ili niweze kumjua mpelelezi wa kesi yangu, naambiwa kwamba halionekani wakati wao ndiyo waliniambia nifuatilie.”
Uwazi lilipomtafuta Grayson na kumuuliza kuhusu sakata hilo, alikiri kuandika barua hiyo na kusema kwamba amefuatilia zaidi ya siku tano kwenye Kituo cha Polisi cha Wazo Hill alikofungulia kesi hiyo lakini anaambiwa faili halionekani.
 “Nimejaribu kuwaambia kama hilo faili la kwanza limeibwa basi wafungue lingine lakini wamekataa,” alisema Grayson ambaye habari yake ya kuvunjiwa nyumba na mama Rwakatare iliripotiwa kwa mara ya kwanza na Gazeti la Uwazi wiki iliyopita ikiwa na kichwa cha habari: MAMA RWAKATARE AFIKISHWA POLISI.
Katika malalamiko yake, Grayson anadai kuvunjiwa nyumba yenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 20 na mchungaji huyo, ambayo aliijenga kwa fedha alizochukua mkopo kazini kwake.
Grayson alidai kwamba nyumba yake hiyo ilivunjwa na greda kipindi alipoenda Moshi kwenye msiba wa baba yake na kiwanja chake anachodai kukinunua kihalali kwa kuandikishana na aliyemuuzia kwenye Ofisi za Serikali ya Mtaa wa Bunju B, kuzungushiwa ukuta.
Uwazi lilipomtafuta Mchungaji Rwakatare na kumhoji kuhusu sakata hilo, alisema kwamba kiwanja hicho ni mali yake tangu mwaka 2005 na alivunja nyumba hiyo kwa sababu alikuwa akikifanyia usafi kiwanja hicho alichodai kilivamiwa.





Share this article :
Tweet
✚
Newer Post
Older Post
Home

HABARI ZILIZO BAMBA TOP 10

  • Lorna Rutto is an entrepreneur who founded Ecopost, a Nairobi-based company that recycles plastic waste
    Lorna Rutto is an entrepreneur who founded Ecopost, a Nairobi-based company that recycles plastic waste. As part of the latest series o...
  • Ajali ya gari huko south B kenya
    There was a bizarre accident today morning in Hazina Estate, South B involving a Range Rover that crashed into 7 vehicles. The Ran...
  • Jennifer Lawrence has joined her castmates at the world premiere of the penultimate Hunger Games movie, Mockingjay Part 1, in London.
    Lawrence plays the heroine Katniss Everdeen in the hit franchise Jennifer Lawrence has joined her castmates at the w...
  • Catalonia's regional president Artur Mas says an official referendum is needed following Catalonia vote: 80% back independence - officials
    \ An informal vote on independence for Catalonia has shown more than 80% in favour, officials say. The non-binding vote went ahead after ...
  • After more than two years of tension over a territorial row,the leaders of China and Japan hold formal talks on the sidelines of a major Asian summit.
    Chinese President Xi Jinping and Japanese PM Shinzo Abe met on the sidelines of the Asia-Pacific Economic Co-operation (Apec) summit in B...
  • MAREKANI YAITUPIA LAWAMA KOREA KASKAZINI
    Marekani inatarajia kuirudisha Korea kaskazini katika orodha ya nchi zinazofadhili ugaidi. Rais Barack Obama wa Marekani amesema utawala ...
  • The poorest president, Jose Mujica gets $1m offer for his VW Beetle
    7 November 2014 Last updated at 07:04 GMT Uruguay's President Jose Mujica says he has been offered $1m (£630,000) for his vinta...
  • Report says,Fossil fuel promises are being broken,World governments have been breaking promises to phase out subsidies for fossil fuels, a report says.
    The report said G20 nations had been spending almost $90bn a year on finding more oil, g...
  • Wabunge wa Somali wameng'oa waziri mkuu
    Ni mara ya nne kwamba kura ya kutokuwa na imani dhidi yake ilipigwa baada ya majaribio ya awali kumalizika kwa ghasia. Waandishi ...
  • AJIITA KIJANA MWENYE BAHATI AKIWA KATIKATI YA WAREMBO WAWILI

LABELS

  • Breaking News
  • condolonces
  • Entertainment
  • Entertainments
  • Habari
  • Majonzi
  • Michezo
  • News
  • News and Updates
  • Skendo
  • Sports and Games
Submit ExpressSEO Services & Tools

Total Pageviews

Copyright 2014 Mwanafalsafa
Template By Ridwan Hex And Game Gratis