Mwanafalsafa

  • HOME
Home → Habari → CCM KUTOICHUKULIA HATUA AKAUNTI YA ESCROW

CCM KUTOICHUKULIA HATUA AKAUNTI YA ESCROW

Habari
Friday, 5 December 2014





Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye, alisema kuwa CCM haina mpango wa kuchukua hatua zozote dhidi ya wote waliotajwa kuhusika na kashfa hiyo kwa sababu chama hicho hakijawahi kuwajadili kwa jambo hilo ambalo siyo la chama chao bali ni la Bunge la Tanzania.

“Suala hili lipo chini ya Bunge na hivyo chama hakijaingilia kati na kuchukua hatua wabunge wake waliotajwa,” alisema Nape. Aliongeza kuwa chama hakiwezi kuchukua hatua zozote dhidi ya wabunge wake waliobainika kula fedha hizo kwani suala hilo halijawahi kufikishwa kwenye vikao vyao. “Hatujawachukulia hatua (waliotajwa), wala hatuna mpango wa kuwachukulia hatua kwa sababu suala hili haliko ndani ya CCM... liko ndani ya bunge, labda kama litaingia ndani ya chama ndiyo tutalitolea maamuzi,” alisema Nape.

Kauli ya Nape imekuja siku chache baada ya chama hicho kutoa msimamo wake dhidi ya wabunge wa chama hicho waliohusika katika sakata hilo kuwa bunge lichukue hatua stahiki. Nape, akiwa na Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana, katika ziara ya kukagua, kuhimiza na kusukuma utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya mwaka 2010/15 mkoani Mtwara, walisema kila aliyehusika katika kashfa hiyo, abebe msalaba wake.

Nape alisema chama hakiwezi kulea maovu yanayofanywa kinyume na kanuni na taratibu za chama hicho, hivyo kama bunge limebaini waliokiuka maadili wachukuliwe hatua stahiki dhidi yao. Kwa upande wake Kinana alisema muda wa kulindana na kubebana ndani ya chama umeisha na anayekiuka taratibu na kanuni za chama hicho awajibishwe na akishindikana achie ngazi.

Wabunge kadhaa kutoka CCM wakiwamo mawaziri Sospeter Muhongo wa Nishati na Madini na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka, ni miongoni mwa vigogo waliotajwa kuhusika na kashfa hiyo na hivyo Bunge kuazimia kuwa waondoshwe.

Wabunge wengine wa CCM waliohusishwa na kashfa hiyo na kutakiwa kuondolewa kwenye nafasi zao za uenyekiti wa kamati za Bunge ni Mbunge wa Bariadi Mashariki anayeongoza Kamati ya Bajeti, Andrew Chenge , Mbunge wa Sengerema, Wiliam Ngeleja (Sheria, Katiba na Utawala) na Mbunge wa Lupa anayeongoza kamati ya Nishati na Madini, Victor Mwambalaswa.






Share this article :
Tweet
✚
Newer Post
Older Post
Home

HABARI ZILIZO BAMBA TOP 10

  • Lorna Rutto is an entrepreneur who founded Ecopost, a Nairobi-based company that recycles plastic waste
    Lorna Rutto is an entrepreneur who founded Ecopost, a Nairobi-based company that recycles plastic waste. As part of the latest series o...
  • Jennifer Lawrence has joined her castmates at the world premiere of the penultimate Hunger Games movie, Mockingjay Part 1, in London.
    Lawrence plays the heroine Katniss Everdeen in the hit franchise Jennifer Lawrence has joined her castmates at the w...
  • Catalonia's regional president Artur Mas says an official referendum is needed following Catalonia vote: 80% back independence - officials
    \ An informal vote on independence for Catalonia has shown more than 80% in favour, officials say. The non-binding vote went ahead after ...
  • After more than two years of tension over a territorial row,the leaders of China and Japan hold formal talks on the sidelines of a major Asian summit.
    Chinese President Xi Jinping and Japanese PM Shinzo Abe met on the sidelines of the Asia-Pacific Economic Co-operation (Apec) summit in B...
  • The poorest president, Jose Mujica gets $1m offer for his VW Beetle
    7 November 2014 Last updated at 07:04 GMT Uruguay's President Jose Mujica says he has been offered $1m (£630,000) for his vinta...
  • Report says,Fossil fuel promises are being broken,World governments have been breaking promises to phase out subsidies for fossil fuels, a report says.
    The report said G20 nations had been spending almost $90bn a year on finding more oil, g...
  • Wabunge wa Somali wameng'oa waziri mkuu
    Ni mara ya nne kwamba kura ya kutokuwa na imani dhidi yake ilipigwa baada ya majaribio ya awali kumalizika kwa ghasia. Waandishi ...
  • AJIITA KIJANA MWENYE BAHATI AKIWA KATIKATI YA WAREMBO WAWILI
  • Burkina Faso leaders agree transitional framework following the meeting held in Ouagadougou
      The blueprint for transition was agreed unanimously at the meeting in Ouagadougou A framework for a transitional government ...
  • John Doar, a civil rights lawyer who was a key figure in the struggle against racial segregation in the US, has died aged 92.
    John Doar was awarded the Presidential Medal of Freedom in 2012 Mr Doar dealt with some of the most prominent civil rights ca...

LABELS

  • Breaking News
  • condolonces
  • Entertainment
  • Entertainments
  • Habari
  • Majonzi
  • Michezo
  • News
  • News and Updates
  • Skendo
  • Sports and Games
Submit ExpressSEO Services & Tools

Total Pageviews

Copyright 2014 Mwanafalsafa
Template By Ridwan Hex And Game Gratis