Mwanafalsafa

  • HOME
Home → Habari → Ukistaajabu ya Mussa ?Nusu ya sura yake inafanana na binadamu na Nusu nyingine inafanana na CHURA, ni mtoto aliye zaliwa huko dodoma

Ukistaajabu ya Mussa ?Nusu ya sura yake inafanana na binadamu na Nusu nyingine inafanana na CHURA, ni mtoto aliye zaliwa huko dodoma

Habari
Friday, 5 December 2014
MKAZI wa kijiji cha Chibwechangula –Behelo katika wilaya ya Mpwapwa mkoani Dodoma, Ruth Matonya (26) amejifungua mtoto wa ajabu ambaye nusu ya sura yake inafanana na binadamu na nusu ikifanana na chura.
 
Mtoto huyo alizaliwa Desemba 2, mwaka huu katika Kituo cha Afya cha Mtakatifu Luka kinachomilikiwa na Kanisa la Anglikana, Dayosisi ya Mpwapwa. Alifariki dunia muda mfupi baada ya kuzaliwa.
 
Kwa mujibu wa Mganga Mfawidhi wa kituo hicho, Dk Edwin Kihura mara baada ya mama huyo kufika katika kituo hicho cha afya alikuwa na uchungu ambao haukuwa na kikomo, lakini alishindwa kujifungua kwa njia ya kawaida licha ya njia ya uzazi kufunguka.
 
Alisema kutokana na hali hiyo iliwalazimu kumfanyia upasuaji mama huyo kwa lengo la kuokoa maisha yake na mtoto.
mtoto
  
Alisema wakati mama huyo akihudhuria kliniki walipojaribu kupima miezi ya mwisho mama huyo, mkao wa mtoto ulikuwa haupatikani pamoja na mapigo ya moyo lakini mtoto alikuwa anacheza tumboni jambo ambalo lilikuwa likiwashangaza waganga na wauguzi kituoni hapo.
 
Dk Kihura alisema mara baada ya mama huyo kufanyiwa upasuaji waliweza kutoa mtoto wa jinsi ya kike ambaye alikuwa na sura isiyoeleweka na kichwa kilikuwa na sura ya binadamu na nusu ikiwa ni sura inayofanana na chura huku viungo vingine vyote vya mwili vikiwa kamili.
 
Alisema zipo sababu kadha zinazoweza kusababisha tatizo kama hili ambapo alisema kuwa ni baadhi ya akinamama kukosa baadhi ya madini mwilini na uumbaji kutokamilika kutokana na sababu za kibaiolojia.
 
Alieleza kuwa hali ya mama huyo inaendelea vizuri na kwamba mtoto huyo alikuwa ni mtoto wake wa tano

Share this article :
Tweet
✚
Newer Post
Older Post
Home

HABARI ZILIZO BAMBA TOP 10

  • Lorna Rutto is an entrepreneur who founded Ecopost, a Nairobi-based company that recycles plastic waste
    Lorna Rutto is an entrepreneur who founded Ecopost, a Nairobi-based company that recycles plastic waste. As part of the latest series o...
  • Wabunge wa Somali wameng'oa waziri mkuu
    Ni mara ya nne kwamba kura ya kutokuwa na imani dhidi yake ilipigwa baada ya majaribio ya awali kumalizika kwa ghasia. Waandishi ...
  • Chuo kikuu cha ardhi ARU chatoa zawadi kwa wanafunzi 30, mmoja, ambae ni muhitimu wa masomo ya surveying aibuka na machine ya millioni 35
    CHUO Kikuu Ardhi (ARU), kimewazawadia wanafuzi 130 wa masomo mbalimbali zawadi zenye thamani ya zaidi ya sh milioni 60 kutokana n...
  • Ajali ya gari huko south B kenya
    There was a bizarre accident today morning in Hazina Estate, South B involving a Range Rover that crashed into 7 vehicles. The Ran...
  • Jennifer Lawrence has joined her castmates at the world premiere of the penultimate Hunger Games movie, Mockingjay Part 1, in London.
    Lawrence plays the heroine Katniss Everdeen in the hit franchise Jennifer Lawrence has joined her castmates at the w...
  • Catalonia's regional president Artur Mas says an official referendum is needed following Catalonia vote: 80% back independence - officials
    \ An informal vote on independence for Catalonia has shown more than 80% in favour, officials say. The non-binding vote went ahead after ...
  • After more than two years of tension over a territorial row,the leaders of China and Japan hold formal talks on the sidelines of a major Asian summit.
    Chinese President Xi Jinping and Japanese PM Shinzo Abe met on the sidelines of the Asia-Pacific Economic Co-operation (Apec) summit in B...
  • MAREKANI YAITUPIA LAWAMA KOREA KASKAZINI
    Marekani inatarajia kuirudisha Korea kaskazini katika orodha ya nchi zinazofadhili ugaidi. Rais Barack Obama wa Marekani amesema utawala ...
  • The poorest president, Jose Mujica gets $1m offer for his VW Beetle
    7 November 2014 Last updated at 07:04 GMT Uruguay's President Jose Mujica says he has been offered $1m (£630,000) for his vinta...
  • Report says,Fossil fuel promises are being broken,World governments have been breaking promises to phase out subsidies for fossil fuels, a report says.
    The report said G20 nations had been spending almost $90bn a year on finding more oil, g...

LABELS

  • Breaking News
  • condolonces
  • Entertainment
  • Entertainments
  • Habari
  • Majonzi
  • Michezo
  • News
  • News and Updates
  • Skendo
  • Sports and Games
Submit ExpressSEO Services & Tools

Total Pageviews

Copyright 2014 Mwanafalsafa
Template By Ridwan Hex And Game Gratis