Mwanafalsafa

  • HOME
Home → Habari → VIJANA WAMVAA MIZENGO PINDA

VIJANA WAMVAA MIZENGO PINDA

Habari
Tuesday, 9 December 2014







BARAZA la Vijana la CHADEMA (BAVICHA), limeitaka Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa (Tamisemi), kutoa majibu ya haraka juu ya kuenguliwa kwa wagombea wa chama hicho katika uchaguzi wa serikali za mitaa unaotarajiwa kufanyika Desemba 14 mwaka huu.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Katibu Mkuu wa BAVICHA, Julius Mwita, alisema kuwa wagombea wa chama chao wameenguliwa katika kinyang’anyiro hicho kwa sababu zisizokuwa za kimsingi.
Alifafanua kuwa, hizo ni mbinu za Chama Cha Mapinduzi (CCM), kwa kutumia viongozi walioko madarakani kutaka kuwapitisha wagombea wao ili kuwasaidia katika uchaguzi mkuu ujao.
“BAVICHA hatuko tayari kuona uonevu wa kiasi hiki tunaufumbia macho, tunamtaka Waziri Mkuu Mizengo Pinda kutoa majibu ya haraka kuhusiana na hili kabla ya siku ya uchaguzi,” alisema Mwita.
Alitaja baadhi ya maeneo aliyopata taarifa kuwa Kamati ya Rufaa imewaengua wagombea wao ni Same, Vunjo, Njombe, Simanjiro na Mwanza.
Aliongeza kuwa, kuna baadhi ya maeneo ambayo wabunge wa CCM wanawalazimisha wakurugenzi wawaengue wagombea wa CHADEMA.
Akizungumzia miaka 53 ya Uhuru wa Tanganyika, Mwita aliwataka vijana kuadhimisha kwa kutafakari hali yao kimaisha, kwani Watanzania walio wengi bado ni masikini, hivyo ni wakati wa kufanya mabadiliko kuanzia kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa.
“Kesho ni sikukuu ya uhuru wa Tanganyika, ni wakati muafaka wa kuangalia je ndani ya miaka 53 tumeweza kupigana na adui umasikini, ujinga na maradhi huku jingine limeongezeka rushwa, hivyo basi ni wakati muafaka kwa Watanzania kufanya mabadiliko kuanzia ngazi ya kata,” alisema.






Share this article :
Tweet
✚
Newer Post
Older Post
Home

HABARI ZILIZO BAMBA TOP 10

  • Takribani watu 15 wapata upofu baada ya upasuaji nchini India
    Wagonjwa waliofanyiwa upasuaji walisema walishindwa kuona tena baada ya kuondoa bandeji kwenye macho yao Maafisa wa utawala nchini Indiaa w...
  • Familia ya mateka yasihi Al Qaeda kumwachilia
    Marekani imeeleza kuwa ilijaribu kumwokoa raia wake mzaliwa wa Uingereza Luke Somers, anayeshikiliwa mateka na al-Qaeda nchini Yemen. ...
  • Ona kilichotokea kwa jimama hili kipindi lina jaribu kucheza jirani na swimming pool.Noii huko Kenya mida ya jana jioni
       
  • AJIITA KIJANA MWENYE BAHATI AKIWA KATIKATI YA WAREMBO WAWILI
  • BRAZIL TO EDGE OUT GERMANY IN WORLD CUP SEMI FINAL
  • KAULI YA UHURU KWENYE MTANDAOWA KIJAMII (TWITTER) KENYATTA HII HAPA
    Taarifa ya mahakama ya ICC, kutupilia mbali kesi dhidi ya Uhuru Kenyatta, imepokelwa na watu wengi nchini Kenya kwa hisia mseto. Baadhi w...
  • Maandano zidi ya kutupiliwa mbali kwa kesi ya afisa polisi mjini New York
    Maandamano mjini New York Waandamanaji wameingia katika barabara za miji mingi Nchini Marekani kwa usiku wa pili mtawalia, kupinga maamu...
  • Jennifer Lawrence has joined her castmates at the world premiere of the penultimate Hunger Games movie, Mockingjay Part 1, in London.
    Lawrence plays the heroine Katniss Everdeen in the hit franchise Jennifer Lawrence has joined her castmates at the w...
  • MORE THAN 10,000 GRADUATES TURN UP FOR SEVENTY JOB VACANCIES IN DAR ES SLAAM.
    According to the list of names seen by The Guardian yesterday morning, the department listed 10,816 candidates to perform the interview tha...
  • Mshindi wa Nishani ya Nobel bint Malala amenukuliwa akisema "Nataka kuwa Waziri mkuu''
    Mshindi wa Nishani ya Nobel bint Malala Yousafzai raia wa Pakistani amesema kuwa siku zijazo anatarajia kuwa mwanasiasa. Malala a...

LABELS

  • Breaking News
  • condolonces
  • Entertainment
  • Entertainments
  • Habari
  • Majonzi
  • Michezo
  • News
  • News and Updates
  • Skendo
  • Sports and Games
Submit ExpressSEO Services & Tools

Total Pageviews

Copyright 2014 Mwanafalsafa
Template By Ridwan Hex And Game Gratis