Mwanafalsafa

  • HOME
Home → Habari → Majonzi → USHIRIKA WAHUSISHWA KWENYE KISA HIKI CHA MWANAMAMA KUMDUMBUKIZA MTOTO KISIMANI

USHIRIKA WAHUSISHWA KWENYE KISA HIKI CHA MWANAMAMA KUMDUMBUKIZA MTOTO KISIMANI

Habari, Majonzi
Friday, 5 December 2014


Hali ya sintofahamu imeibuka katika mtaa wa Azimio, kata ya Kihonda katika manispaa ya Morogoro, baada ya mwanamke mmoja, Veronica Madebe, kukutwa akitaka kumtumbukiza mwanaye wa kiume ambaye ni pacha, mwenye umri wa kati ya miaka mitano hadi saba kwenye kisima cha maji, kutokana na kinachosadikiwa kuwa ni imani za kishirikina.

Tukio hilo limejiri katika eneo hilo la Azimio, baada ya mwanamke huyo kukutwa na mmiliki wa nyumba kilipo kisima hicho, Dani Haji, akijaribu kumtumbukiza kisimani mmoja wa watoto wake pacha, kwa madai yaliyoelezwa huenda ni kupungukiwa akili, ama ni imani za kishirikina.

Amedai kutumwa na wakazi wawili wa eneo hilo kufanya hivyo, na wakati mwingine kudai alikuwa kwenye kifungo na alipaswa kutoa kafara ya mtoto wake kwa kumtupa kisimani ili afunguke baada ya kuokoka kiimani, jambo lililothibitishwa pia na mmoja wa wajumbe wa serikali za mitaa katika eneo hilo.

Mmoja wa familia iliyotajwa na mwanamke huyo kufanya kitendo hicho cha kikatili, kilichozuiwa na wasamaria wema, anakiri kumfahamu mwanamke huyo lakini bila kuwa na matatizo yeyote, na alishangazwa na hatua hiyo na alipomuona aliamua kumvaa yeye na mtoto aliyekuwa amembeba, bila sababu zozote, hadi alipoamuliwa na kundi la wananchi waliojitokeza.


Wananchi wa eneo hilo walipigasimu polisi kuomba msaada wa dharura na kumpeleka mama huyo katika ofisi za mtendaji wa kata ya Kihonda, ambako ulinzi mkali wa polisi uliimarishwa, na baada ya muda mwanamke huyo alitolewa na kuingizwa kwenye gari ndogo kwa nia ya kupelekwa polisi, lakini alifanya vurugu hadi polisi walipoingilia kati na kumpakiza kwenye difenda na kuondoka naye.

Share this article :
Tweet
✚
Newer Post
Older Post
Home

HABARI ZILIZO BAMBA TOP 10

  • MAREKANI YAITUPIA LAWAMA KOREA KASKAZINI
    Marekani inatarajia kuirudisha Korea kaskazini katika orodha ya nchi zinazofadhili ugaidi. Rais Barack Obama wa Marekani amesema utawala ...
  • MKUU wa Wilaya ya Mufindi mkoani Iringa, Evarista Kalalu, awashauri wananchi kujiunga na mfuko wa afya ya jamii
    MKUU wa Wilaya ya Mufindi mkoani Iringa, Evarista Kalalu, amewashauri wananchi wa vijiji vya Ukami na Chogo Kata ya Mapanda wilayani hapa...
  • KAULI YA UHURU KWENYE MTANDAOWA KIJAMII (TWITTER) KENYATTA HII HAPA
    Taarifa ya mahakama ya ICC, kutupilia mbali kesi dhidi ya Uhuru Kenyatta, imepokelwa na watu wengi nchini Kenya kwa hisia mseto. Baadhi w...
  • HAYA NDIO MAZITO ALIYO FUNGUKA YULE MSICHANA WA KAZI ALIYE MPIGA MTOTO
    Baada ya story ya yule msichana kwa anayefanya kazi za ndani Uganda kuchukua headlines katika vyombo mbalimbali vya Kimataifa Dun...
  • Ronaldo aosha vyombo baada ya kushindwa katika karata na mchezaji wa Tenisi Rafa Nadal
    Ali...
  • Wayne Goss, former premier of Queensland, kicked the bucket at 63
    Mr Goss, who was premier from 1989 to 1996, had suffered from ill health in recent years including brain tumours. He became Q...
  • IT 'S MATTER OF FEW MINUTES FOR WORLD CUP 2014 START SHINNING !!!!
    The World Cup  The 2014  Brazil™ is now just a matter of minutes away and to mark the occasion FIFA have launched an updated version of th...

LABELS

  • Breaking News
  • condolonces
  • Entertainment
  • Entertainments
  • Habari
  • Majonzi
  • Michezo
  • News
  • News and Updates
  • Skendo
  • Sports and Games
Submit ExpressSEO Services & Tools

Total Pageviews

Copyright 2014 Mwanafalsafa
Template By Ridwan Hex And Game Gratis