Mwanafalsafa

  • HOME
Home → Habari → Maandano zidi ya kutupiliwa mbali kwa kesi ya afisa polisi mjini New York

Maandano zidi ya kutupiliwa mbali kwa kesi ya afisa polisi mjini New York

Habari
Friday, 5 December 2014

Maandamano mjini New York
Waandamanaji wameingia katika barabara za miji mingi Nchini Marekani kwa usiku wa pili mtawalia, kupinga maamuzi ya majaji kutupilia mbali kesi dhidi ya afisa wa polisi aliyedaiwa kumuua raia mmarekani mweusi nchini humo Eric Garner.
Mjini New York, waandamanaji wameonekana wakibeaba kaburi bandia wakivuka daraja la Brooklyn Bridge huku wakitatiza msongamano wa magari barabarani mjini New York.
Meya wa jiji hilo, Bill de Blasio, amewaambia wanahabari kuwa uhusiano kati ya maofisa wa polisi na raia wa Marekani, unafaa kubadilika, na watu wanafaa kufahamu kuwa maisha ya watu weusi ni sawa na ya watu weupe.
Mnamo Jumatano, Polisi jijini New York waliwatia mbaroni watu 83 baada ya maandamano mengine kutokea siku ambayo maandamano hayo yalianza baada ya mahakama kutupilia mbali kesi dhidi ya askari mzungu kwa kumuua Eric Garner.
Wanaharakati wa kutetea haki za binadamu, wameweka matumaini yao katika maafisa wa polisi watakaoufanyia kesi hio uchunguzi zaidi.
Meya wa New York, Bill de Blasio, amenukuliwa akisema kuwa polisi 22,000 walioko mjini humo watapewa mafunzo zaidi kuhusu namna ya wanavyowakamata wahalifu au washukiwa wa uhalifu.
Rais Barack Obama amesifu tamko la Meya akisema kuwa wamarekani wengine wanahisi kutokuwepo usawa katika sheria na ambavyo inatekelezwa.

Share this article :
Tweet
✚
Newer Post
Older Post
Home

HABARI ZILIZO BAMBA TOP 10

  • Takribani watu 15 wapata upofu baada ya upasuaji nchini India
    Wagonjwa waliofanyiwa upasuaji walisema walishindwa kuona tena baada ya kuondoa bandeji kwenye macho yao Maafisa wa utawala nchini Indiaa w...
  • Familia ya mateka yasihi Al Qaeda kumwachilia
    Marekani imeeleza kuwa ilijaribu kumwokoa raia wake mzaliwa wa Uingereza Luke Somers, anayeshikiliwa mateka na al-Qaeda nchini Yemen. ...
  • Ona kilichotokea kwa jimama hili kipindi lina jaribu kucheza jirani na swimming pool.Noii huko Kenya mida ya jana jioni
       
  • AJIITA KIJANA MWENYE BAHATI AKIWA KATIKATI YA WAREMBO WAWILI
  • BRAZIL TO EDGE OUT GERMANY IN WORLD CUP SEMI FINAL
  • KAULI YA UHURU KWENYE MTANDAOWA KIJAMII (TWITTER) KENYATTA HII HAPA
    Taarifa ya mahakama ya ICC, kutupilia mbali kesi dhidi ya Uhuru Kenyatta, imepokelwa na watu wengi nchini Kenya kwa hisia mseto. Baadhi w...
  • Maandano zidi ya kutupiliwa mbali kwa kesi ya afisa polisi mjini New York
    Maandamano mjini New York Waandamanaji wameingia katika barabara za miji mingi Nchini Marekani kwa usiku wa pili mtawalia, kupinga maamu...
  • Jennifer Lawrence has joined her castmates at the world premiere of the penultimate Hunger Games movie, Mockingjay Part 1, in London.
    Lawrence plays the heroine Katniss Everdeen in the hit franchise Jennifer Lawrence has joined her castmates at the w...
  • MORE THAN 10,000 GRADUATES TURN UP FOR SEVENTY JOB VACANCIES IN DAR ES SLAAM.
    According to the list of names seen by The Guardian yesterday morning, the department listed 10,816 candidates to perform the interview tha...
  • Mshindi wa Nishani ya Nobel bint Malala amenukuliwa akisema "Nataka kuwa Waziri mkuu''
    Mshindi wa Nishani ya Nobel bint Malala Yousafzai raia wa Pakistani amesema kuwa siku zijazo anatarajia kuwa mwanasiasa. Malala a...

LABELS

  • Breaking News
  • condolonces
  • Entertainment
  • Entertainments
  • Habari
  • Majonzi
  • Michezo
  • News
  • News and Updates
  • Skendo
  • Sports and Games
Submit ExpressSEO Services & Tools

Total Pageviews

Copyright 2014 Mwanafalsafa
Template By Ridwan Hex And Game Gratis