Mwanafalsafa

  • HOME
Home → Habari → WAZIRI wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernad Membe, kesho Jumamosi Desemba 6 anatarajiwa Kuwa mgeni rasmi Katika Mahafali ya Pili ya Chuo Kikuu Cha Bagamoyo (UB).

WAZIRI wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernad Membe, kesho Jumamosi Desemba 6 anatarajiwa Kuwa mgeni rasmi Katika Mahafali ya Pili ya Chuo Kikuu Cha Bagamoyo (UB).

Habari
Friday, 5 December 2014



Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa kwa vyombo kwa vyombo vya Habari Dar Es
Salaam,  na Ofisa Habari wa  ( UB), Happiness Katabazi, inasema Kuwa
Membe ndiye Atakuwa mgeni rasmi Katika mahafali hayo ambayo yatafanyika Katika
Hoteli ya Kiromo  View Resort  kijijini Kiromo Wilayani Bagamoyo,Mkoani
Pwani.




Katabazi alisema jumla ya wahitimu 99 wanatarajiwa kutunukiwa Vyeti Katika
ngazi ya Shahada ya Uzamili, Shahada ya Kwanza, Diploma,  na cheti.




Wakati huo huo , Juzi Makamu wa Rais  Dk.Mohammed Gharib Bilal alishindwa
kuhudhuria sherehe za uwekwaji  wa jiwe la Msingi wa makazi ya kudumu ya
UB ikiwa ni ishara ya kuanza kwa ujenzi wa makao makuu ya UB kijijini hapo
ambapo ujenzi ukikamilia majengo hayo yatakuwa na uwezo wa kuchukua zaidi ya
wanafunzi 5000, yaliyopaswa yafanyike Katika kijijini Cha Kiromo ,Bagamoyo
Mkoani Pwani kwasababu alikuwa amebanwa na majukumu mengine ya Kitaifa na
akaomba apangiwe tarehe nyingine ya kuja kuweka jiwe Hilo la Msingi.




Akizungumza na waandishi wa Habari Katika kijijini Kiromo Juzi wakati
akiiarisha sherehe za Utiaji wa jiwe la Msingi , Makamu Mkuu wa UB, Profesa
Costa Ricky Mahalu alitoa historia fupi la shamba Hilo lililopo Kijijini Kiromo
Alisema  familia yake ililinunua rasmi Agosti 26 Mwaka 2003.





Profesa Mahalu alisema Katika shamba Hilo familia yake imeamua kukata heka 100
na kuzitoa kwa UB ili UB iweze kujenga makazi yake ya kufumu katika Kijiji cha
Kiromo na kwamba heka nyingine zilizosalia familia yake itazitoa  kwa
Taasisi nyingine za elimu ya juu  na kwamba Tayari Taasisi nne za elimu ya
juu ikiwemo Chuo Kikuu Kimoja Cha kigeni kimeishaonyesha nia ya kutaka Kuja
Kujenga Taasisi yake ya elimu Katika shamba Hilo.




Profesa Mahalu Alisema shamba hilo kabla familia yake haijalinunua lilikuwa
likimilikiwa na lililokuwa shirika la Serikali la NAFCO na baada ya kufirisika
mwaka 1990  lilichukuliwa na LART  ambaye alikuwa na jukumu la
kuchukua  kuuza Mashitaka ya serikali yalikuwa na matatizo ya kifedha.




' LART ikamkabidhi  kampuni ya PHLLIP&Ltd  iliyauza mashamba
matatu  ya NAFCO  yaliyopo Kiromo. Hayo mashamba matatu ,Moja
iliuziwa familia ya Mahalu na mkataba wa mauzo wa shamba Hilo la Mahalu na LART
ulisainiwa Agosti 26 Mwaka 2903  na baada ya hapo  umiliki wa
shamba  unachukuliwa  na familia ya Mahalu kwa mujibu wa Sheria.'
Alisema Balozi Mahalu.




Share this article :
Tweet
✚
Newer Post
Older Post
Home

HABARI ZILIZO BAMBA TOP 10

  • Takribani watu 15 wapata upofu baada ya upasuaji nchini India
    Wagonjwa waliofanyiwa upasuaji walisema walishindwa kuona tena baada ya kuondoa bandeji kwenye macho yao Maafisa wa utawala nchini Indiaa w...
  • Familia ya mateka yasihi Al Qaeda kumwachilia
    Marekani imeeleza kuwa ilijaribu kumwokoa raia wake mzaliwa wa Uingereza Luke Somers, anayeshikiliwa mateka na al-Qaeda nchini Yemen. ...
  • Ona kilichotokea kwa jimama hili kipindi lina jaribu kucheza jirani na swimming pool.Noii huko Kenya mida ya jana jioni
       
  • AJIITA KIJANA MWENYE BAHATI AKIWA KATIKATI YA WAREMBO WAWILI
  • BRAZIL TO EDGE OUT GERMANY IN WORLD CUP SEMI FINAL
  • KAULI YA UHURU KWENYE MTANDAOWA KIJAMII (TWITTER) KENYATTA HII HAPA
    Taarifa ya mahakama ya ICC, kutupilia mbali kesi dhidi ya Uhuru Kenyatta, imepokelwa na watu wengi nchini Kenya kwa hisia mseto. Baadhi w...
  • Maandano zidi ya kutupiliwa mbali kwa kesi ya afisa polisi mjini New York
    Maandamano mjini New York Waandamanaji wameingia katika barabara za miji mingi Nchini Marekani kwa usiku wa pili mtawalia, kupinga maamu...
  • Jennifer Lawrence has joined her castmates at the world premiere of the penultimate Hunger Games movie, Mockingjay Part 1, in London.
    Lawrence plays the heroine Katniss Everdeen in the hit franchise Jennifer Lawrence has joined her castmates at the w...
  • MORE THAN 10,000 GRADUATES TURN UP FOR SEVENTY JOB VACANCIES IN DAR ES SLAAM.
    According to the list of names seen by The Guardian yesterday morning, the department listed 10,816 candidates to perform the interview tha...
  • Mshindi wa Nishani ya Nobel bint Malala amenukuliwa akisema "Nataka kuwa Waziri mkuu''
    Mshindi wa Nishani ya Nobel bint Malala Yousafzai raia wa Pakistani amesema kuwa siku zijazo anatarajia kuwa mwanasiasa. Malala a...

LABELS

  • Breaking News
  • condolonces
  • Entertainment
  • Entertainments
  • Habari
  • Majonzi
  • Michezo
  • News
  • News and Updates
  • Skendo
  • Sports and Games
Submit ExpressSEO Services & Tools

Total Pageviews

Copyright 2014 Mwanafalsafa
Template By Ridwan Hex And Game Gratis