Mwanafalsafa

  • HOME
Home → Habari → WAZIRI wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernad Membe, kesho Jumamosi Desemba 6 anatarajiwa Kuwa mgeni rasmi Katika Mahafali ya Pili ya Chuo Kikuu Cha Bagamoyo (UB).

WAZIRI wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernad Membe, kesho Jumamosi Desemba 6 anatarajiwa Kuwa mgeni rasmi Katika Mahafali ya Pili ya Chuo Kikuu Cha Bagamoyo (UB).

Habari
Friday, 5 December 2014



Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa kwa vyombo kwa vyombo vya Habari Dar Es
Salaam,  na Ofisa Habari wa  ( UB), Happiness Katabazi, inasema Kuwa
Membe ndiye Atakuwa mgeni rasmi Katika mahafali hayo ambayo yatafanyika Katika
Hoteli ya Kiromo  View Resort  kijijini Kiromo Wilayani Bagamoyo,Mkoani
Pwani.




Katabazi alisema jumla ya wahitimu 99 wanatarajiwa kutunukiwa Vyeti Katika
ngazi ya Shahada ya Uzamili, Shahada ya Kwanza, Diploma,  na cheti.




Wakati huo huo , Juzi Makamu wa Rais  Dk.Mohammed Gharib Bilal alishindwa
kuhudhuria sherehe za uwekwaji  wa jiwe la Msingi wa makazi ya kudumu ya
UB ikiwa ni ishara ya kuanza kwa ujenzi wa makao makuu ya UB kijijini hapo
ambapo ujenzi ukikamilia majengo hayo yatakuwa na uwezo wa kuchukua zaidi ya
wanafunzi 5000, yaliyopaswa yafanyike Katika kijijini Cha Kiromo ,Bagamoyo
Mkoani Pwani kwasababu alikuwa amebanwa na majukumu mengine ya Kitaifa na
akaomba apangiwe tarehe nyingine ya kuja kuweka jiwe Hilo la Msingi.




Akizungumza na waandishi wa Habari Katika kijijini Kiromo Juzi wakati
akiiarisha sherehe za Utiaji wa jiwe la Msingi , Makamu Mkuu wa UB, Profesa
Costa Ricky Mahalu alitoa historia fupi la shamba Hilo lililopo Kijijini Kiromo
Alisema  familia yake ililinunua rasmi Agosti 26 Mwaka 2003.





Profesa Mahalu alisema Katika shamba Hilo familia yake imeamua kukata heka 100
na kuzitoa kwa UB ili UB iweze kujenga makazi yake ya kufumu katika Kijiji cha
Kiromo na kwamba heka nyingine zilizosalia familia yake itazitoa  kwa
Taasisi nyingine za elimu ya juu  na kwamba Tayari Taasisi nne za elimu ya
juu ikiwemo Chuo Kikuu Kimoja Cha kigeni kimeishaonyesha nia ya kutaka Kuja
Kujenga Taasisi yake ya elimu Katika shamba Hilo.




Profesa Mahalu Alisema shamba hilo kabla familia yake haijalinunua lilikuwa
likimilikiwa na lililokuwa shirika la Serikali la NAFCO na baada ya kufirisika
mwaka 1990  lilichukuliwa na LART  ambaye alikuwa na jukumu la
kuchukua  kuuza Mashitaka ya serikali yalikuwa na matatizo ya kifedha.




' LART ikamkabidhi  kampuni ya PHLLIP&Ltd  iliyauza mashamba
matatu  ya NAFCO  yaliyopo Kiromo. Hayo mashamba matatu ,Moja
iliuziwa familia ya Mahalu na mkataba wa mauzo wa shamba Hilo la Mahalu na LART
ulisainiwa Agosti 26 Mwaka 2903  na baada ya hapo  umiliki wa
shamba  unachukuliwa  na familia ya Mahalu kwa mujibu wa Sheria.'
Alisema Balozi Mahalu.




Share this article :
Tweet
✚
Newer Post
Older Post
Home

HABARI ZILIZO BAMBA TOP 10

  • MAREKANI YAITUPIA LAWAMA KOREA KASKAZINI
    Marekani inatarajia kuirudisha Korea kaskazini katika orodha ya nchi zinazofadhili ugaidi. Rais Barack Obama wa Marekani amesema utawala ...
  • Mamboya whatsapp haya hapa.!!!!! (18+)
  • SIMBA Vs EXPRESS YA UGANDA ,0-0 LEO UWANJA WA TAIFA
    Katongole Henry akimtoka mshambulia wa Simba, Ramadhani Singano 'Mess'. Kipa wa The Express, Mutumba Ivan akir...
  • Ronaldo aosha vyombo baada ya kushindwa katika karata na mchezaji wa Tenisi Rafa Nadal
    Ali...
  • AKOTHEE Takes Her Beautiful Daughters TO FLY OVER ! look at these beautiful photos.
  • APIGWA MVUA YA MIAKA 60 JELA, KWA KUTOROSHA TWIGA
    HATIMAYE Mahakama ya hakimu mkazi Moshi, mkoani Kilimanjaro, imemhukumu miaka 60 jela, Kamran Ahmed, raia wa Pakistani kwa kosa la kutoro...
  • John Doar, a civil rights lawyer who was a key figure in the struggle against racial segregation in the US, has died aged 92.
    John Doar was awarded the Presidential Medal of Freedom in 2012 Mr Doar dealt with some of the most prominent civil rights ca...
  • TEKNOLOGIA:GARI LINALOWEZA KUPAKI LENYEWE KWA KUTUMIA SAA YA SMARTPHONE BILA KUWA NA DEREVA NDANI..
    Kampuni ya BMW imezindua kifaa ambacho kinawezesha gari lako kujiegesha lenyewe.. Hakuna kitu kibaya kama kusahau ulikoegesha gari lako ka...
  • Spotify's chief executive has defended its business model, saying it has paid out $2bn (£1.2bn) to the music industry to date.
      Daniel Ek pitches Spotify as a more lucrative alternative to piracy Daniel Ek's lengthy blog post follows a high profil...
  • Mapya ya Dk.Slaa kuhusu IPTL
    KATIBU Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Wilibrod Slaa, amesema fedha zilizochotwa katika Akaunti ya Tegeta ...

LABELS

  • Breaking News
  • condolonces
  • Entertainment
  • Entertainments
  • Habari
  • Majonzi
  • Michezo
  • News
  • News and Updates
  • Skendo
  • Sports and Games
Submit ExpressSEO Services & Tools

Total Pageviews

Copyright 2014 Mwanafalsafa
Template By Ridwan Hex And Game Gratis