Mwanafalsafa

  • HOME
Home → Michezo → BINGWA MBIO ZA MOTUMBWI KULAMBA KITITA CHA TSH. 2,700,000

BINGWA MBIO ZA MOTUMBWI KULAMBA KITITA CHA TSH. 2,700,000

Michezo
Friday, 5 December 2014


Meneja wa Bia ya Balimi Extra Lager, Edith Bebwa (katikati) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa kutangaza zawadi za fainali za Kanda za mashindano ya bio za makasia zijulikanazo kama “Balimi Boat Race” zinazo dhaminiwa na bia ya Balimi Extara Lager zinazo tarajiwa kufanyika katika ufukwe wa Mwaloni jijini Mwanza leo.
BINGWA  MBIO ZA MITUMBWI KANDA YA ZIWA KUONDOKA NA 2,700,000/=
Na Mwandishi Wetu.Mwanza
Bingwa wa fainali za mashindano ya mbio za makasia Wanaume, chini ya udhamini wa Bia ya Balimi Extra Lager yajulikanayo kama “Balimi Boat Race 2014” anatarajia kujinyakulia kitita cha pesa taslimu Shilingi Milioni 2,700,000/=,Kikombe pamoja na medali za dhahabu kwa wanakikundi hicho.

Akizungumza na waandishi wa habari, Meneja wa Bia ya Balimi Exra Lager, Edith Bebwa alisema fainali hizo zitaanza majira ya saa tatu na asubuhi na kuendelea katika ufukwe wa Mwaloni jijini Mwanza ambapo jumla ya vikundi 15 vya Wanaume kutoka katika mikoa mitano ya Kanda ya ziwa vitachuana kumtafuta bingwa wa Kanda kwa mwaka 2014 na vikundi 11 upande wa Wanawake.
Edith alisema mikoa ya Kanda ya Ziwa inayoshiriki ni Kigoma,Kagera,Mwanza,Musoma na Kisiwa cha Ukerewe ambacho kinabeba hadhi ya Mkoa.

Mshindi wa pili Wanaume atazawadiwa pesa taslimu Shilingi 2,300,000/=,mshindi wa tatu Shilingi 1,700,000/= na wa nne 900,000/=.Wakati mshindi wa tano hadi wa kumi watapata kifuta jasho cha pesa taslimu Shilingi 400,000/= kila kikundi alisema Edihi.

Upande wa wanawake bingwa wa mwaka 2014 ataibuka na kitita cha pesa taslimu Shilingi 2,300,000/=,kikombe na medali za dhahabu kwa wanakikundi wote.Mshindi wa tatu atazawadiwa Shilingi 1,700,000/=,wa tatu Shilingi 900,000/= na wa nne 700,000/= wakati mshindi wa 5 hadi wa 10 watazawadiwa kifuta jasho cha pesa taslimu Shilingi 250,000/= kila kikundi.

Nae Meneja wa Kampuni ya Bia nchini Kanda ya Ziwa, Malaki Sitaki aliwaomba wakazi wa jiji la Mwanza na vijiji jirani kujitokeza kwa wingi katika ufukwa wa Mwaloni kushuhudia fainali hizo zenye mvuto wa pekee na mwisho wafahamu nani atachukua ubingwa wa mbio hizo kwa mwaka 2014.


Meneja matukio wa TBL Kanda ya Ziwa, Erick Mwayela alisema vikundi vyote vimeshawasili jijini Mwanza tayari kwa mpambano wa kumpata bingwa wa mwaka huu na maandalizi kwa ujumla yamesha kamilika hivyo nae aliwaomba watu wajitokeze kushuhudia mbio hizo.


Share this article :
Tweet
✚
Newer Post
Older Post
Home

HABARI ZILIZO BAMBA TOP 10

  • Umuhimu wa kushirikiana katika kazi hasa ya muziki
  • Wiki hii katika mtandao wa kijamii, whatsapp , Ni sheedah cheki picha kali hapa chini !
  • Mwanasheria mkuu wa serikali nchini Mexico, Jesus Murillo Karam,ametoa ahadi kuwa hakutakuwa na uonevu wowote katika kesi ya kupotea kwa wanafunzi nchi humo miezi miwili iliyopita
    . Kutoweka kwa wanafunzi hao kumesababisha maandamano ya wiki kadhaa nchini humo waandamanaji wakipinda rushwa na ukatili...
  • Ni majonzi makubwa Tazama picha za wana familia za wachimba machimbo ya kokoto waliouawa na Al Shabaab mjini Mandera
    Familia za wachimba machimbo ya kokoto waliouawa na Al Shabaab mjini Mandera leo waliwapokea wapendwa wao baada ya miili yao kufikishwa ch...
  • After more than two years of tension over a territorial row,the leaders of China and Japan hold formal talks on the sidelines of a major Asian summit.
    Chinese President Xi Jinping and Japanese PM Shinzo Abe met on the sidelines of the Asia-Pacific Economic Co-operation (Apec) summit in B...
  • CCM KUTOICHUKULIA HATUA AKAUNTI YA ESCROW
    Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye, alisema kuwa CCM haina mpango wa kuchukua hatua zozote dhidi ya wote waliotajwa kuh...
  • A hardline cleric in Pakistan is teaching the ideas of Osama Bin Laden in religious schools for about 5,000 children.
       Even while the Pakistani government fights the Taliban in the north-west of the country, it has no plans to clos...
  • Lorna Rutto is an entrepreneur who founded Ecopost, a Nairobi-based company that recycles plastic waste
    Lorna Rutto is an entrepreneur who founded Ecopost, a Nairobi-based company that recycles plastic waste. As part of the latest series o...
  • AJIITA KIJANA MWENYE BAHATI AKIWA KATIKATI YA WAREMBO WAWILI
  • HIVI NDIVYO Gangnam Walivyovunja rekodi huko YouTube
    Jump media player Media player help Out of media player. Press enter to return or tab to continue. Na Kim Kardashian a...

LABELS

  • Breaking News
  • condolonces
  • Entertainment
  • Entertainments
  • Habari
  • Majonzi
  • Michezo
  • News
  • News and Updates
  • Skendo
  • Sports and Games
Submit ExpressSEO Services & Tools

Total Pageviews

Copyright 2014 Mwanafalsafa
Template By Ridwan Hex And Game Gratis