Mwanafalsafa

  • HOME
Home → Michezo → BINGWA MBIO ZA MOTUMBWI KULAMBA KITITA CHA TSH. 2,700,000

BINGWA MBIO ZA MOTUMBWI KULAMBA KITITA CHA TSH. 2,700,000

Michezo
Friday, 5 December 2014


Meneja wa Bia ya Balimi Extra Lager, Edith Bebwa (katikati) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa kutangaza zawadi za fainali za Kanda za mashindano ya bio za makasia zijulikanazo kama “Balimi Boat Race” zinazo dhaminiwa na bia ya Balimi Extara Lager zinazo tarajiwa kufanyika katika ufukwe wa Mwaloni jijini Mwanza leo.
BINGWA  MBIO ZA MITUMBWI KANDA YA ZIWA KUONDOKA NA 2,700,000/=
Na Mwandishi Wetu.Mwanza
Bingwa wa fainali za mashindano ya mbio za makasia Wanaume, chini ya udhamini wa Bia ya Balimi Extra Lager yajulikanayo kama “Balimi Boat Race 2014” anatarajia kujinyakulia kitita cha pesa taslimu Shilingi Milioni 2,700,000/=,Kikombe pamoja na medali za dhahabu kwa wanakikundi hicho.

Akizungumza na waandishi wa habari, Meneja wa Bia ya Balimi Exra Lager, Edith Bebwa alisema fainali hizo zitaanza majira ya saa tatu na asubuhi na kuendelea katika ufukwe wa Mwaloni jijini Mwanza ambapo jumla ya vikundi 15 vya Wanaume kutoka katika mikoa mitano ya Kanda ya ziwa vitachuana kumtafuta bingwa wa Kanda kwa mwaka 2014 na vikundi 11 upande wa Wanawake.
Edith alisema mikoa ya Kanda ya Ziwa inayoshiriki ni Kigoma,Kagera,Mwanza,Musoma na Kisiwa cha Ukerewe ambacho kinabeba hadhi ya Mkoa.

Mshindi wa pili Wanaume atazawadiwa pesa taslimu Shilingi 2,300,000/=,mshindi wa tatu Shilingi 1,700,000/= na wa nne 900,000/=.Wakati mshindi wa tano hadi wa kumi watapata kifuta jasho cha pesa taslimu Shilingi 400,000/= kila kikundi alisema Edihi.

Upande wa wanawake bingwa wa mwaka 2014 ataibuka na kitita cha pesa taslimu Shilingi 2,300,000/=,kikombe na medali za dhahabu kwa wanakikundi wote.Mshindi wa tatu atazawadiwa Shilingi 1,700,000/=,wa tatu Shilingi 900,000/= na wa nne 700,000/= wakati mshindi wa 5 hadi wa 10 watazawadiwa kifuta jasho cha pesa taslimu Shilingi 250,000/= kila kikundi.

Nae Meneja wa Kampuni ya Bia nchini Kanda ya Ziwa, Malaki Sitaki aliwaomba wakazi wa jiji la Mwanza na vijiji jirani kujitokeza kwa wingi katika ufukwa wa Mwaloni kushuhudia fainali hizo zenye mvuto wa pekee na mwisho wafahamu nani atachukua ubingwa wa mbio hizo kwa mwaka 2014.


Meneja matukio wa TBL Kanda ya Ziwa, Erick Mwayela alisema vikundi vyote vimeshawasili jijini Mwanza tayari kwa mpambano wa kumpata bingwa wa mwaka huu na maandalizi kwa ujumla yamesha kamilika hivyo nae aliwaomba watu wajitokeze kushuhudia mbio hizo.


Share this article :
Tweet
✚
Newer Post
Older Post
Home

HABARI ZILIZO BAMBA TOP 10

  • MAREKANI YAITUPIA LAWAMA KOREA KASKAZINI
    Marekani inatarajia kuirudisha Korea kaskazini katika orodha ya nchi zinazofadhili ugaidi. Rais Barack Obama wa Marekani amesema utawala ...
  • Mamboya whatsapp haya hapa.!!!!! (18+)
  • SIMBA Vs EXPRESS YA UGANDA ,0-0 LEO UWANJA WA TAIFA
    Katongole Henry akimtoka mshambulia wa Simba, Ramadhani Singano 'Mess'. Kipa wa The Express, Mutumba Ivan akir...
  • AKOTHEE Takes Her Beautiful Daughters TO FLY OVER ! look at these beautiful photos.
  • APIGWA MVUA YA MIAKA 60 JELA, KWA KUTOROSHA TWIGA
    HATIMAYE Mahakama ya hakimu mkazi Moshi, mkoani Kilimanjaro, imemhukumu miaka 60 jela, Kamran Ahmed, raia wa Pakistani kwa kosa la kutoro...
  • TEKNOLOGIA:GARI LINALOWEZA KUPAKI LENYEWE KWA KUTUMIA SAA YA SMARTPHONE BILA KUWA NA DEREVA NDANI..
    Kampuni ya BMW imezindua kifaa ambacho kinawezesha gari lako kujiegesha lenyewe.. Hakuna kitu kibaya kama kusahau ulikoegesha gari lako ka...
  • Spotify's chief executive has defended its business model, saying it has paid out $2bn (£1.2bn) to the music industry to date.
      Daniel Ek pitches Spotify as a more lucrative alternative to piracy Daniel Ek's lengthy blog post follows a high profil...
  • Mombasa based singer akothee gets naughty,Angalia hapa
  • ,Juncker reveals giant EU investment planJuncker said Europe needed a kick-start and the Commission was offering the jump-leads
    Mr  European Commission President Jean-Claude Juncker has given details of a €315bn (£250bn;$393bn) investment plan to kic...
  • HILI NDILO BALAA LA MAFURIKO YALIYOTOKEA HUKO MWANZA
    Kivuko asilia ni ajira kwa wengine. Wanajeshi wa Kikosi cha zimamoto Mwanza wakimvusha mama huyu kutoka juu ya paa la nyumba moja had...

LABELS

  • Breaking News
  • condolonces
  • Entertainment
  • Entertainments
  • Habari
  • Majonzi
  • Michezo
  • News
  • News and Updates
  • Skendo
  • Sports and Games
Submit ExpressSEO Services & Tools

Total Pageviews

Copyright 2014 Mwanafalsafa
Template By Ridwan Hex And Game Gratis