Mwanafalsafa

  • HOME
Home → Michezo → BINGWA MBIO ZA MOTUMBWI KULAMBA KITITA CHA TSH. 2,700,000

BINGWA MBIO ZA MOTUMBWI KULAMBA KITITA CHA TSH. 2,700,000

Michezo
Friday, 5 December 2014


Meneja wa Bia ya Balimi Extra Lager, Edith Bebwa (katikati) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa kutangaza zawadi za fainali za Kanda za mashindano ya bio za makasia zijulikanazo kama “Balimi Boat Race” zinazo dhaminiwa na bia ya Balimi Extara Lager zinazo tarajiwa kufanyika katika ufukwe wa Mwaloni jijini Mwanza leo.
BINGWA  MBIO ZA MITUMBWI KANDA YA ZIWA KUONDOKA NA 2,700,000/=
Na Mwandishi Wetu.Mwanza
Bingwa wa fainali za mashindano ya mbio za makasia Wanaume, chini ya udhamini wa Bia ya Balimi Extra Lager yajulikanayo kama “Balimi Boat Race 2014” anatarajia kujinyakulia kitita cha pesa taslimu Shilingi Milioni 2,700,000/=,Kikombe pamoja na medali za dhahabu kwa wanakikundi hicho.

Akizungumza na waandishi wa habari, Meneja wa Bia ya Balimi Exra Lager, Edith Bebwa alisema fainali hizo zitaanza majira ya saa tatu na asubuhi na kuendelea katika ufukwe wa Mwaloni jijini Mwanza ambapo jumla ya vikundi 15 vya Wanaume kutoka katika mikoa mitano ya Kanda ya ziwa vitachuana kumtafuta bingwa wa Kanda kwa mwaka 2014 na vikundi 11 upande wa Wanawake.
Edith alisema mikoa ya Kanda ya Ziwa inayoshiriki ni Kigoma,Kagera,Mwanza,Musoma na Kisiwa cha Ukerewe ambacho kinabeba hadhi ya Mkoa.

Mshindi wa pili Wanaume atazawadiwa pesa taslimu Shilingi 2,300,000/=,mshindi wa tatu Shilingi 1,700,000/= na wa nne 900,000/=.Wakati mshindi wa tano hadi wa kumi watapata kifuta jasho cha pesa taslimu Shilingi 400,000/= kila kikundi alisema Edihi.

Upande wa wanawake bingwa wa mwaka 2014 ataibuka na kitita cha pesa taslimu Shilingi 2,300,000/=,kikombe na medali za dhahabu kwa wanakikundi wote.Mshindi wa tatu atazawadiwa Shilingi 1,700,000/=,wa tatu Shilingi 900,000/= na wa nne 700,000/= wakati mshindi wa 5 hadi wa 10 watazawadiwa kifuta jasho cha pesa taslimu Shilingi 250,000/= kila kikundi.

Nae Meneja wa Kampuni ya Bia nchini Kanda ya Ziwa, Malaki Sitaki aliwaomba wakazi wa jiji la Mwanza na vijiji jirani kujitokeza kwa wingi katika ufukwa wa Mwaloni kushuhudia fainali hizo zenye mvuto wa pekee na mwisho wafahamu nani atachukua ubingwa wa mbio hizo kwa mwaka 2014.


Meneja matukio wa TBL Kanda ya Ziwa, Erick Mwayela alisema vikundi vyote vimeshawasili jijini Mwanza tayari kwa mpambano wa kumpata bingwa wa mwaka huu na maandalizi kwa ujumla yamesha kamilika hivyo nae aliwaomba watu wajitokeze kushuhudia mbio hizo.


Share this article :
Tweet
✚
Newer Post
Older Post
Home

HABARI ZILIZO BAMBA TOP 10

  • Lorna Rutto is an entrepreneur who founded Ecopost, a Nairobi-based company that recycles plastic waste
    Lorna Rutto is an entrepreneur who founded Ecopost, a Nairobi-based company that recycles plastic waste. As part of the latest series o...
  • Catalonia's regional president Artur Mas says an official referendum is needed following Catalonia vote: 80% back independence - officials
    \ An informal vote on independence for Catalonia has shown more than 80% in favour, officials say. The non-binding vote went ahead after ...
  • After more than two years of tension over a territorial row,the leaders of China and Japan hold formal talks on the sidelines of a major Asian summit.
    Chinese President Xi Jinping and Japanese PM Shinzo Abe met on the sidelines of the Asia-Pacific Economic Co-operation (Apec) summit in B...
  • Report says,Fossil fuel promises are being broken,World governments have been breaking promises to phase out subsidies for fossil fuels, a report says.
    The report said G20 nations had been spending almost $90bn a year on finding more oil, g...
  • Wabunge wa Somali wameng'oa waziri mkuu
    Ni mara ya nne kwamba kura ya kutokuwa na imani dhidi yake ilipigwa baada ya majaribio ya awali kumalizika kwa ghasia. Waandishi ...
  • Burkina Faso leaders agree transitional framework following the meeting held in Ouagadougou
      The blueprint for transition was agreed unanimously at the meeting in Ouagadougou A framework for a transitional government ...
  • John Doar, a civil rights lawyer who was a key figure in the struggle against racial segregation in the US, has died aged 92.
    John Doar was awarded the Presidential Medal of Freedom in 2012 Mr Doar dealt with some of the most prominent civil rights ca...
  • Kiungo mpya wa Azam, Amri Kiemba akiwa katika jezi ya timu hiyo kwenye Uwanja wa Chamazi, Dar es Salaam jana
       Klabu ya Yanga imemleta nchini kwa majaribio mshambuliaji raia wa Zambia, Jonas Sakuwaha ...
  • Spotify's chief executive has defended its business model, saying it has paid out $2bn (£1.2bn) to the music industry to date.
      Daniel Ek pitches Spotify as a more lucrative alternative to piracy Daniel Ek's lengthy blog post follows a high profil...
  • The actress best known for playing the unseen role of Howard Wolowitz's mother on The Big Bang Theory has died.
      Big Bang Theory's Mrs Wolowitz dies at the age of 62 Carol Ann Susi had played the role of Mrs Wolowitz since 2007   ...

LABELS

  • Breaking News
  • condolonces
  • Entertainment
  • Entertainments
  • Habari
  • Majonzi
  • Michezo
  • News
  • News and Updates
  • Skendo
  • Sports and Games
Submit ExpressSEO Services & Tools

Total Pageviews

Copyright 2014 Mwanafalsafa
Template By Ridwan Hex And Game Gratis