Mwanafalsafa

  • HOME
Home → Habari → Wapiganaji wa Islamic State katika jimbo la Anbar wafungua kambi za mafunzo Libya

Wapiganaji wa Islamic State katika jimbo la Anbar wafungua kambi za mafunzo Libya

Habari
Thursday, 4 December 2014
Wapiganaji wa kundi la Islamic State wafungua kambi za mafunzo Libya
Wapiganaji wa kundi la Islamic State wameanzisha kambi za mafunzo mashariki mwa Libya, amesema mkuu wa kamandi ya Marekani ya masuala ya Afrika.
Jenerali David Rodriguez amesema kuna mamia ya wapiganaji wa IS wanaopata mafunzo ya kijeshi kwenye kambi zake nchini Libya. Amesema kambi hizo zipo katika hatua za mwanoz kabisa, lakini Marekani imekuwa ikiyafuatilia kwa karibu kuona zinavyoendelezwa.
Wapiganaji wa Kikurd wakiwa katika mafunzo ya kijeshi kukabiliana na wapiganaji wa Islamic State Septemba 2014 nchini Iraq
Libya imekuwa katika mgogoro tangu kuangushwa kwa utawala wa Muammar Gaddafi mwaka 2011, ambapo makabila mbalimbali, wanamgambo na makundi ya kisiasa, wote wakipigania madaraka.
Makundi mbalimbali ya Kiislam yanawania madaraka mashariki mwa Libya, huku baadhi yakitangaza kuwa na ushirikiano la kundi la Islamic State, IS.
Wapiganaji kutoka kikundi cha IS wakipakia mabaki ya kile kinachosemekana kuwa mabaki ya ndege ya Marekani isiyotumia abiria baada ya kukonga katika mnara wa mawasiliano huko Raqqa Septemba 23,2014
Akizungumza mjini Washington Jumatano, Jenerali Rodriguez bado haijafahamika ukaribu uliopo kati ya watu wanaopata mafunzo hayo na kundi la IS.
"Kikubwa ni watu wanaokuja kupata mafunzo na msaada wa vifaa kwa ajili ya kambi za mafunzo kwa sasa," amesema. "kwa sasa mafunzo hayo bado ni ya hatua ya chini sana na tunafuatilia kuona namna hali inavyokwenda."
Watoto wakikimbia kando ya mlima hukumoshi ukisambaa angani kufuatia mapigano katika eneo hilo la mji wa Kobani, wakati majeshi yanayoongozwa na Marekani kushambulia wapiganaji wa Islamic State 
 
Waandishi wa habari wanasema katika kipindi cha mapinduzi yaliyomwondoa madarakani Gaddafi, wapiganaji wengi waasi waliondoka nchini humo kwenda kujiunga na vikundi vya wapiganaji nchini Syria na baadhi yao wanaaminika kuwa wamerejea nyumbani(Libya).
Serikali iliyochaguliwa imepoteza miji mikuu mitatu ya Libya huku kukiwa na mgogoro wa kisiasa.
Benghazi, mji wa pili kwa ukubwa nchini Libya, uko mikononi mwa wapiganaji wa Kiislam, na bunge linalotambuliwa kimataifa kwa sasa linaendesha vikao vyake katika mji ulioko pwani ya Tobruk mashariki mwa nchi hiyo.
Marekani imekuwa ikiongoza washirika wa kimataifa kufanya mashambulio ya anga dhidi ya IS nchini Iraq na Syria katika miezi ya karibuni.

Share this article :
Tweet
✚
Newer Post
Older Post
Home

HABARI ZILIZO BAMBA TOP 10

  • Umuhimu wa kushirikiana katika kazi hasa ya muziki
  • Wiki hii katika mtandao wa kijamii, whatsapp , Ni sheedah cheki picha kali hapa chini !
  • Mwanasheria mkuu wa serikali nchini Mexico, Jesus Murillo Karam,ametoa ahadi kuwa hakutakuwa na uonevu wowote katika kesi ya kupotea kwa wanafunzi nchi humo miezi miwili iliyopita
    . Kutoweka kwa wanafunzi hao kumesababisha maandamano ya wiki kadhaa nchini humo waandamanaji wakipinda rushwa na ukatili...
  • Ni majonzi makubwa Tazama picha za wana familia za wachimba machimbo ya kokoto waliouawa na Al Shabaab mjini Mandera
    Familia za wachimba machimbo ya kokoto waliouawa na Al Shabaab mjini Mandera leo waliwapokea wapendwa wao baada ya miili yao kufikishwa ch...
  • After more than two years of tension over a territorial row,the leaders of China and Japan hold formal talks on the sidelines of a major Asian summit.
    Chinese President Xi Jinping and Japanese PM Shinzo Abe met on the sidelines of the Asia-Pacific Economic Co-operation (Apec) summit in B...
  • CCM KUTOICHUKULIA HATUA AKAUNTI YA ESCROW
    Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye, alisema kuwa CCM haina mpango wa kuchukua hatua zozote dhidi ya wote waliotajwa kuh...
  • A hardline cleric in Pakistan is teaching the ideas of Osama Bin Laden in religious schools for about 5,000 children.
       Even while the Pakistani government fights the Taliban in the north-west of the country, it has no plans to clos...
  • Lorna Rutto is an entrepreneur who founded Ecopost, a Nairobi-based company that recycles plastic waste
    Lorna Rutto is an entrepreneur who founded Ecopost, a Nairobi-based company that recycles plastic waste. As part of the latest series o...
  • AJIITA KIJANA MWENYE BAHATI AKIWA KATIKATI YA WAREMBO WAWILI
  • The actress best known for playing the unseen role of Howard Wolowitz's mother on The Big Bang Theory has died.
      Big Bang Theory's Mrs Wolowitz dies at the age of 62 Carol Ann Susi had played the role of Mrs Wolowitz since 2007   ...

LABELS

  • Breaking News
  • condolonces
  • Entertainment
  • Entertainments
  • Habari
  • Majonzi
  • Michezo
  • News
  • News and Updates
  • Skendo
  • Sports and Games
Submit ExpressSEO Services & Tools

Total Pageviews

Copyright 2014 Mwanafalsafa
Template By Ridwan Hex And Game Gratis