Mwanafalsafa

  • HOME
Home → Tanpa Kategori → Kesi ya Uhuru, ICC yampa muda Fatou Bensouda ambae ni kiongozi wa mshataka katika mahakama ya kimataifa ICC

Kesi ya Uhuru, ICC yampa muda Fatou Bensouda ambae ni kiongozi wa mshataka katika mahakama ya kimataifa ICC

Thursday, 4 December 2014

Mahakama ya kimataifa kuhusu uhalifu wa kivita ICC imempa kiongozi wa mashtaka katika mahakama hiyo Fatou Bensouda muda wa wiki moja ili kutoa ushahidi dhidi ya rais wa Kenya, la sivyo aondoe mashtaka dhidi yake.
''Kucheleweshwa kwa kesi hiyo ya Rais Uhuru ni kinyume na maslahi ya haki.'' ilisema.
Rais Kenyatta ni kiongozi wa kwanza wa taifa kufika katika mahakama hiyo tangu ashtakiwe rasmi mwaka 2012 na mashtaka ya uhalifu dhidi ya binadamu,ambayo ameyakana.
Kiongozi huyo wa mashtaka ametaka kupewa muda zaidi ili kujenga kesi yake dhidi ya kiongozi huyo.
Anasema kwamba mashahidi wamehongwa na kutishiwa maisha huku serikali ya Kenya ikikataa kutoa stakhabadhi muhimu za kesi hiyo.
Bwana Kenyatta amekanusha kuchochea ghasia kufuatia mgogoro wa uchaguzi wa mwaka 2007 ili kumpatia ushindi aliyekuwa rais wa Kenya Mwai Kibaki na kusema kuwa kesi hiyo ni ya kisiasa.
Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya aliyeshtakiwa kwa mauaji katika ghasia za baada ya uchaguzi wa mwaka 2007 nchini humo. 
 
Akikataa ombi la kiongozi huyo wa mashtaka kuchelewesha kesi hiyo, majaji wa mahakama hiyo walisema kuwa wamempatia wiki moja Bensouda kusema iwapo ataitupilia mbali kesi hiyo ama ushahidi alio nao unaweza kuhimili kesi hiyo kuendelea.
Rais Kenyatta alishinda uchaguzi wa urais mwaka 2013 kupitia usaidizi wa Mwai Kibaki.
Aliitumia kesi hiyo kutafuta kuungwa mkono huku akiikashifu mahakama hiyo ya mjini Hague kwa kuingilia masuala ya Kenya.
Ameshtakiwa na mahakama hiyo kwa kuhusika moja kwa moja katika mauaji ya baada ya uchaguzi wa mwaka 2007/2008.
Takriban watu 1,200 waliuawa katika ghasia hizo huku wengine 600,000 wakiachwa bila makazi.

Share this article :
Tweet
✚
Newer Post
Older Post
Home

HABARI ZILIZO BAMBA TOP 10

  • MAREKANI YAITUPIA LAWAMA KOREA KASKAZINI
    Marekani inatarajia kuirudisha Korea kaskazini katika orodha ya nchi zinazofadhili ugaidi. Rais Barack Obama wa Marekani amesema utawala ...
  • Mombasa based singer akothee gets naughty,Angalia hapa
  • Vita dhidi ya Ukimwi zashika kasi, mbinu madhubuti zachukuliwa !
    DESEMBA mosi, kila mwaka, watu wote duniani huadhimisha Siku ya Ukimwi Duniani. Siku hiyo ilianzishwa mwaka 1987 na hubeba maudhui mbalim...
  • ,Juncker reveals giant EU investment planJuncker said Europe needed a kick-start and the Commission was offering the jump-leads
    Mr  European Commission President Jean-Claude Juncker has given details of a €315bn (£250bn;$393bn) investment plan to kic...
  • Kwaninii serikali imewekeza katika siasa na imesahau wakulima ?
      Hata hivyo, wakulima wamekwazwa na kodi nyingi wanazotozwa kwa kila gunia inapotokea wakauza sehemu ya ...
  • Mdogo wa Zari Hassan apaka matope uhusiano wake na Diamond
    Mdogo wake na Zari Hassan aka The Bosslady, aitwaye Karim ametumia Facebook kumkosoa dada yake kwa kuwa na uhusiano na Diamond Platnumz amb...
  • DAVIDO,TIWA SWAGE,DIAMOND, MR.FLAVOUR ON THE SHOOT,CHECK THE NEW VIDEO HERE
    Africa MultiChoice has launched it’s biggest  campaign yet, to celebrate Africa’s positivity , successes and the ability to  te...
  • Wayne Goss, former premier of Queensland, kicked the bucket at 63
    Mr Goss, who was premier from 1989 to 1996, had suffered from ill health in recent years including brain tumours. He became Q...
  • Third death confirmed in Mali The Pasteur Clinic in Bamako has been placed in quarantine and is under armed guard
      A nurse and the patient he was treating have become the second and third people to die from Ebola in Mali. The patient,...
  • The poorest president, Jose Mujica gets $1m offer for his VW Beetle
    7 November 2014 Last updated at 07:04 GMT Uruguay's President Jose Mujica says he has been offered $1m (£630,000) for his vinta...

LABELS

  • Breaking News
  • condolonces
  • Entertainment
  • Entertainments
  • Habari
  • Majonzi
  • Michezo
  • News
  • News and Updates
  • Skendo
  • Sports and Games
Submit ExpressSEO Services & Tools

Total Pageviews

Copyright 2014 Mwanafalsafa
Template By Ridwan Hex And Game Gratis