Mwanafalsafa

  • HOME
Home → Tanpa Kategori → Kesi ya Uhuru, ICC yampa muda Fatou Bensouda ambae ni kiongozi wa mshataka katika mahakama ya kimataifa ICC

Kesi ya Uhuru, ICC yampa muda Fatou Bensouda ambae ni kiongozi wa mshataka katika mahakama ya kimataifa ICC

Thursday, 4 December 2014

Mahakama ya kimataifa kuhusu uhalifu wa kivita ICC imempa kiongozi wa mashtaka katika mahakama hiyo Fatou Bensouda muda wa wiki moja ili kutoa ushahidi dhidi ya rais wa Kenya, la sivyo aondoe mashtaka dhidi yake.
''Kucheleweshwa kwa kesi hiyo ya Rais Uhuru ni kinyume na maslahi ya haki.'' ilisema.
Rais Kenyatta ni kiongozi wa kwanza wa taifa kufika katika mahakama hiyo tangu ashtakiwe rasmi mwaka 2012 na mashtaka ya uhalifu dhidi ya binadamu,ambayo ameyakana.
Kiongozi huyo wa mashtaka ametaka kupewa muda zaidi ili kujenga kesi yake dhidi ya kiongozi huyo.
Anasema kwamba mashahidi wamehongwa na kutishiwa maisha huku serikali ya Kenya ikikataa kutoa stakhabadhi muhimu za kesi hiyo.
Bwana Kenyatta amekanusha kuchochea ghasia kufuatia mgogoro wa uchaguzi wa mwaka 2007 ili kumpatia ushindi aliyekuwa rais wa Kenya Mwai Kibaki na kusema kuwa kesi hiyo ni ya kisiasa.
Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya aliyeshtakiwa kwa mauaji katika ghasia za baada ya uchaguzi wa mwaka 2007 nchini humo. 
 
Akikataa ombi la kiongozi huyo wa mashtaka kuchelewesha kesi hiyo, majaji wa mahakama hiyo walisema kuwa wamempatia wiki moja Bensouda kusema iwapo ataitupilia mbali kesi hiyo ama ushahidi alio nao unaweza kuhimili kesi hiyo kuendelea.
Rais Kenyatta alishinda uchaguzi wa urais mwaka 2013 kupitia usaidizi wa Mwai Kibaki.
Aliitumia kesi hiyo kutafuta kuungwa mkono huku akiikashifu mahakama hiyo ya mjini Hague kwa kuingilia masuala ya Kenya.
Ameshtakiwa na mahakama hiyo kwa kuhusika moja kwa moja katika mauaji ya baada ya uchaguzi wa mwaka 2007/2008.
Takriban watu 1,200 waliuawa katika ghasia hizo huku wengine 600,000 wakiachwa bila makazi.

Share this article :
Tweet
✚
Newer Post
Older Post
Home

HABARI ZILIZO BAMBA TOP 10

  • Lorna Rutto is an entrepreneur who founded Ecopost, a Nairobi-based company that recycles plastic waste
    Lorna Rutto is an entrepreneur who founded Ecopost, a Nairobi-based company that recycles plastic waste. As part of the latest series o...
  • Ajali ya gari huko south B kenya
    There was a bizarre accident today morning in Hazina Estate, South B involving a Range Rover that crashed into 7 vehicles. The Ran...
  • Jennifer Lawrence has joined her castmates at the world premiere of the penultimate Hunger Games movie, Mockingjay Part 1, in London.
    Lawrence plays the heroine Katniss Everdeen in the hit franchise Jennifer Lawrence has joined her castmates at the w...
  • Catalonia's regional president Artur Mas says an official referendum is needed following Catalonia vote: 80% back independence - officials
    \ An informal vote on independence for Catalonia has shown more than 80% in favour, officials say. The non-binding vote went ahead after ...
  • After more than two years of tension over a territorial row,the leaders of China and Japan hold formal talks on the sidelines of a major Asian summit.
    Chinese President Xi Jinping and Japanese PM Shinzo Abe met on the sidelines of the Asia-Pacific Economic Co-operation (Apec) summit in B...
  • MAREKANI YAITUPIA LAWAMA KOREA KASKAZINI
    Marekani inatarajia kuirudisha Korea kaskazini katika orodha ya nchi zinazofadhili ugaidi. Rais Barack Obama wa Marekani amesema utawala ...
  • The poorest president, Jose Mujica gets $1m offer for his VW Beetle
    7 November 2014 Last updated at 07:04 GMT Uruguay's President Jose Mujica says he has been offered $1m (£630,000) for his vinta...
  • Report says,Fossil fuel promises are being broken,World governments have been breaking promises to phase out subsidies for fossil fuels, a report says.
    The report said G20 nations had been spending almost $90bn a year on finding more oil, g...
  • Wabunge wa Somali wameng'oa waziri mkuu
    Ni mara ya nne kwamba kura ya kutokuwa na imani dhidi yake ilipigwa baada ya majaribio ya awali kumalizika kwa ghasia. Waandishi ...
  • AJIITA KIJANA MWENYE BAHATI AKIWA KATIKATI YA WAREMBO WAWILI

LABELS

  • Breaking News
  • condolonces
  • Entertainment
  • Entertainments
  • Habari
  • Majonzi
  • Michezo
  • News
  • News and Updates
  • Skendo
  • Sports and Games
Submit ExpressSEO Services & Tools

Total Pageviews

Copyright 2014 Mwanafalsafa
Template By Ridwan Hex And Game Gratis