Mwanafalsafa

  • HOME
Home → Habari → Michezo → Tatizo la kuwapo bandari bubu linazidi kuongezeka.

Tatizo la kuwapo bandari bubu linazidi kuongezeka.

Habari, Michezo
Wednesday, 26 November 2014


Rais Jakaya Kikwete.PICHA|MAKTABA 

 Jeshi la Polisi mkoani Tanga juzi lilisema kwamba kuna zaidi ya bandari bubu 50 katika mkoa huo ambazo zinaingiza bidhaa ambazo hazilipiwi ushuru, huku nyingine zikiwa bandia.


Laiti Rais Jakaya Kikwete angekuwa na utaratibu wa Serikali yake kufanya tathmini endelevu ya utekelezaji wa kazi wa mawaziri katika wizara zote, angegundua kwamba zipo baadhi ya wizara ambazo viongozi wake ni mizigo isiyobebeka kutokana na kutofanya kazi, huku wakilipwa mishahara minono. Mfano hai ni Wizara ya Viwanda na Biashara, ambayo kwa muda mrefu sasa imekuwa ikilalamikiwa na wananchi kwa kutotimiza majukumu yake. Ni wizara ambayo wananchi wengi wanasema haina lolote la kujivunia, kinyume na baadhi ya wizara, ambazo utendaji kazi wa mawaziri wake siyo tu umetukuka, bali pia ni wa kutolea mfano.
Wakati wa kuzindua mpango wa Serikali wa Matokeo Makubwa Sasa (BRN) miezi kadhaa iliyopita, tuliambiwa kwamba mawaziri wote walipewa malengo ya utekelezaji wa mpango huo na kwamba kila waziri alisaini mkataba maalumu mbele ya Rais Kikwete, ‘akila kiapo’ kutekeleza majukumu hayo kwa mujibu wa mkataba huo. Vinginevyo angewajibishwa, kwa maana ya kupoteza kazi yake. Wapo mawaziri ambao wameonyesha uwajibikaji mkubwa katika utekelezaji wa malengo yaliyowekwa, lakini pia wapo mawaziri ambao wameendelea kufanya kazi kwa mazoea.
Pamoja na changamoto nyingi zinazoikabili Wizara ya Viwanda na Biashara, wananchi hawaoni nini kinafanyika katika kukabili changamoto hizo. Jana katika safu hii tulizungumzia changamoto ya ukosefu wa masoko kwa mazao ya biashara na chakula, tukisema wakulima wameachwa njia panda kwa mazao yao kutonunuliwa, huku wakibakia katika umaskini uliopitiliza.
Tunapozungumzia masoko tuna maana ya masoko ya ndani na nje ya nchi. Tani zaidi ya 16 milioni za mahindi ya wakulima zilizorundikana katika mikoa ya Morogoro, Rukwa, Katavi, Mbeya na Iringa kwa kukosa soko ni ushahidi usioacha shaka kwamba wizara inayohusika na biashara haina mbinu na mikakati ya kumaliza kero hiyo.
Ni kazi ya wizara hiyo kwa kushirikiana na wizara inayohusika na uwezeshaji kuwaunganisha wakulima na mitandao ya masoko mbalimbali. Sukari inayozalishwa nchini imelundikana katika maghala kwa kukosa soko, huku bidhaa hiyo kutoka nje ikiingizwa nchini kwa bei ndogo kwa sababu ya kutolipiwa kodi. Wizara hiyo haijui kinachoendelea, ingawa inazo habari kwamba bidhaa nyingi zisizolipiwa ushuru zinaingizwa nchini kupitia bandari nyingi bubu zilizoenea katika maeneo ya Pwani ya Bahari ya Hindi, yakiwamo maeneo ya Mbweni, Mlingotini, Ununio, Kawe, Msasani, Kunduchi, Kigamboni, Tegeta na Bagamoyo.
Tatizo la kuwapo bandari bubu linazidi kuongezeka. Jeshi la Polisi mkoani Tanga juzi lilisema kwamba kuna zaidi ya bandari bubu 50 katika mkoa huo ambazo zinaingiza bidhaa ambazo hazilipiwi ushuru, huku nyingine zikiwa bandia. Itakumbukwa kuwa, Waziri wa Biashara na Viwanda, Abdallah Kigoda alisema bungeni mwaka 2013 kuhusu kuwapo kwa bandari bubu na upitishaji wa bidhaa bandia katika maeneo mengi nchini. Kwa nini wizara husika haichukui hatua ni swali ambalo pengine linaweza kujibiwa na waziri huyo pekee.
Ndiyo maana wananchi wengi wanasema wizara hiyo ni mzigo, kwani imeshindwa siyo tu kuendeleza viwanda vidogovidogo, bali pia kuanzisha viwanda vya kusindika matunda kama nanasi, nyanya, maembe na machungwa ili wakulima wapate masoko ya mazao hayo. Ni kwa sababu hiyo tunasema wizara hiyo inahitaji waziri na watendaji wenye ubunifu na moyo wa kuwatumikia wananchi.

Share this article :
Tweet
✚
Newer Post
Older Post
Home

HABARI ZILIZO BAMBA TOP 10

  • The World leaders are arriving in Australia for this weekend's G20 summit in the Queensland city of Brisbane.
      The two-day summit, attended by the US, Chinese and Russian leaders among others, will focus on promoting growth. Australian Pri...
  • Ronaldo aosha vyombo baada ya kushindwa katika karata na mchezaji wa Tenisi Rafa Nadal
    Ali...
  • In long, dimly lit hallways, clusters of people wait anxiously outside courtrooms for their cases to come before a judge.
    The New York Immigration Court is an extraordinarily busy place. In long, dimly lit hallways, clusters of people wait anxiously outside co...
  • Chinese leader Xi Jinping has urged Asia-Pacific nations to accelerate economic integration to spur global growth, on day two of the Apec summit.
    The high-level meeting includes the leaders of the US, Russia, China, Japan and others He spoke as leaders from the 21-na...
  • John Doar, a civil rights lawyer who was a key figure in the struggle against racial segregation in the US, has died aged 92.
    John Doar was awarded the Presidential Medal of Freedom in 2012 Mr Doar dealt with some of the most prominent civil rights ca...
  • Ukweli kuhusu umoja wa fedha,Jumuiya ya Afrika Mashariki.
      OKTOBA 20 hadi 24 mwaka  huu, Benki Kuu ya Tanzania (BoT) iliandaa semi...
  • Kiungo mpya wa Azam, Amri Kiemba akiwa katika jezi ya timu hiyo kwenye Uwanja wa Chamazi, Dar es Salaam jana
       Klabu ya Yanga imemleta nchini kwa majaribio mshambuliaji raia wa Zambia, Jonas Sakuwaha ...
  • Rais wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa ametunukiwa Tuzo ya Mafanikio Katika Utumishi wa Umma kutokana na mchango alioutoa kwenye uchumi wakati wa utawala wake.
      Kwa ufupi Kufanya kazi bila kuchoka, kusisitiza uwazi na ukweli katika kuboresha uchumi katika kipindi chake kwampaisha....
  • Dies aged 87,singing legend, Sabah, Lebanese
      Sabah was nicknamed "Shahroura", Arabic for "singing bird" by her mil...
  • Tatizo la kuwapo bandari bubu linazidi kuongezeka.
    Rais Jakaya Kikwete.PICHA|MAKTABA   Jeshi la Polisi mkoani Tanga ju...

LABELS

  • Breaking News
  • condolonces
  • Entertainment
  • Entertainments
  • Habari
  • Majonzi
  • Michezo
  • News
  • News and Updates
  • Skendo
  • Sports and Games
Submit ExpressSEO Services & Tools

Total Pageviews

Copyright 2014 Mwanafalsafa
Template By Ridwan Hex And Game Gratis