Mwanafalsafa

  • HOME
Home → Habari → Michezo → Tatizo la kuwapo bandari bubu linazidi kuongezeka.

Tatizo la kuwapo bandari bubu linazidi kuongezeka.

Habari, Michezo
Wednesday, 26 November 2014


Rais Jakaya Kikwete.PICHA|MAKTABA 

 Jeshi la Polisi mkoani Tanga juzi lilisema kwamba kuna zaidi ya bandari bubu 50 katika mkoa huo ambazo zinaingiza bidhaa ambazo hazilipiwi ushuru, huku nyingine zikiwa bandia.


Laiti Rais Jakaya Kikwete angekuwa na utaratibu wa Serikali yake kufanya tathmini endelevu ya utekelezaji wa kazi wa mawaziri katika wizara zote, angegundua kwamba zipo baadhi ya wizara ambazo viongozi wake ni mizigo isiyobebeka kutokana na kutofanya kazi, huku wakilipwa mishahara minono. Mfano hai ni Wizara ya Viwanda na Biashara, ambayo kwa muda mrefu sasa imekuwa ikilalamikiwa na wananchi kwa kutotimiza majukumu yake. Ni wizara ambayo wananchi wengi wanasema haina lolote la kujivunia, kinyume na baadhi ya wizara, ambazo utendaji kazi wa mawaziri wake siyo tu umetukuka, bali pia ni wa kutolea mfano.
Wakati wa kuzindua mpango wa Serikali wa Matokeo Makubwa Sasa (BRN) miezi kadhaa iliyopita, tuliambiwa kwamba mawaziri wote walipewa malengo ya utekelezaji wa mpango huo na kwamba kila waziri alisaini mkataba maalumu mbele ya Rais Kikwete, ‘akila kiapo’ kutekeleza majukumu hayo kwa mujibu wa mkataba huo. Vinginevyo angewajibishwa, kwa maana ya kupoteza kazi yake. Wapo mawaziri ambao wameonyesha uwajibikaji mkubwa katika utekelezaji wa malengo yaliyowekwa, lakini pia wapo mawaziri ambao wameendelea kufanya kazi kwa mazoea.
Pamoja na changamoto nyingi zinazoikabili Wizara ya Viwanda na Biashara, wananchi hawaoni nini kinafanyika katika kukabili changamoto hizo. Jana katika safu hii tulizungumzia changamoto ya ukosefu wa masoko kwa mazao ya biashara na chakula, tukisema wakulima wameachwa njia panda kwa mazao yao kutonunuliwa, huku wakibakia katika umaskini uliopitiliza.
Tunapozungumzia masoko tuna maana ya masoko ya ndani na nje ya nchi. Tani zaidi ya 16 milioni za mahindi ya wakulima zilizorundikana katika mikoa ya Morogoro, Rukwa, Katavi, Mbeya na Iringa kwa kukosa soko ni ushahidi usioacha shaka kwamba wizara inayohusika na biashara haina mbinu na mikakati ya kumaliza kero hiyo.
Ni kazi ya wizara hiyo kwa kushirikiana na wizara inayohusika na uwezeshaji kuwaunganisha wakulima na mitandao ya masoko mbalimbali. Sukari inayozalishwa nchini imelundikana katika maghala kwa kukosa soko, huku bidhaa hiyo kutoka nje ikiingizwa nchini kwa bei ndogo kwa sababu ya kutolipiwa kodi. Wizara hiyo haijui kinachoendelea, ingawa inazo habari kwamba bidhaa nyingi zisizolipiwa ushuru zinaingizwa nchini kupitia bandari nyingi bubu zilizoenea katika maeneo ya Pwani ya Bahari ya Hindi, yakiwamo maeneo ya Mbweni, Mlingotini, Ununio, Kawe, Msasani, Kunduchi, Kigamboni, Tegeta na Bagamoyo.
Tatizo la kuwapo bandari bubu linazidi kuongezeka. Jeshi la Polisi mkoani Tanga juzi lilisema kwamba kuna zaidi ya bandari bubu 50 katika mkoa huo ambazo zinaingiza bidhaa ambazo hazilipiwi ushuru, huku nyingine zikiwa bandia. Itakumbukwa kuwa, Waziri wa Biashara na Viwanda, Abdallah Kigoda alisema bungeni mwaka 2013 kuhusu kuwapo kwa bandari bubu na upitishaji wa bidhaa bandia katika maeneo mengi nchini. Kwa nini wizara husika haichukui hatua ni swali ambalo pengine linaweza kujibiwa na waziri huyo pekee.
Ndiyo maana wananchi wengi wanasema wizara hiyo ni mzigo, kwani imeshindwa siyo tu kuendeleza viwanda vidogovidogo, bali pia kuanzisha viwanda vya kusindika matunda kama nanasi, nyanya, maembe na machungwa ili wakulima wapate masoko ya mazao hayo. Ni kwa sababu hiyo tunasema wizara hiyo inahitaji waziri na watendaji wenye ubunifu na moyo wa kuwatumikia wananchi.

Share this article :
Tweet
✚
Newer Post
Older Post
Home

HABARI ZILIZO BAMBA TOP 10

  • MAREKANI YAITUPIA LAWAMA KOREA KASKAZINI
    Marekani inatarajia kuirudisha Korea kaskazini katika orodha ya nchi zinazofadhili ugaidi. Rais Barack Obama wa Marekani amesema utawala ...
  • Mombasa based singer akothee gets naughty,Angalia hapa
  • Vita dhidi ya Ukimwi zashika kasi, mbinu madhubuti zachukuliwa !
    DESEMBA mosi, kila mwaka, watu wote duniani huadhimisha Siku ya Ukimwi Duniani. Siku hiyo ilianzishwa mwaka 1987 na hubeba maudhui mbalim...
  • ,Juncker reveals giant EU investment planJuncker said Europe needed a kick-start and the Commission was offering the jump-leads
    Mr  European Commission President Jean-Claude Juncker has given details of a €315bn (£250bn;$393bn) investment plan to kic...
  • Kwaninii serikali imewekeza katika siasa na imesahau wakulima ?
      Hata hivyo, wakulima wamekwazwa na kodi nyingi wanazotozwa kwa kila gunia inapotokea wakauza sehemu ya ...
  • Mdogo wa Zari Hassan apaka matope uhusiano wake na Diamond
    Mdogo wake na Zari Hassan aka The Bosslady, aitwaye Karim ametumia Facebook kumkosoa dada yake kwa kuwa na uhusiano na Diamond Platnumz amb...
  • DAVIDO,TIWA SWAGE,DIAMOND, MR.FLAVOUR ON THE SHOOT,CHECK THE NEW VIDEO HERE
    Africa MultiChoice has launched it’s biggest  campaign yet, to celebrate Africa’s positivity , successes and the ability to  te...
  • Wayne Goss, former premier of Queensland, kicked the bucket at 63
    Mr Goss, who was premier from 1989 to 1996, had suffered from ill health in recent years including brain tumours. He became Q...
  • Third death confirmed in Mali The Pasteur Clinic in Bamako has been placed in quarantine and is under armed guard
      A nurse and the patient he was treating have become the second and third people to die from Ebola in Mali. The patient,...
  • The poorest president, Jose Mujica gets $1m offer for his VW Beetle
    7 November 2014 Last updated at 07:04 GMT Uruguay's President Jose Mujica says he has been offered $1m (£630,000) for his vinta...

LABELS

  • Breaking News
  • condolonces
  • Entertainment
  • Entertainments
  • Habari
  • Majonzi
  • Michezo
  • News
  • News and Updates
  • Skendo
  • Sports and Games
Submit ExpressSEO Services & Tools

Total Pageviews

Copyright 2014 Mwanafalsafa
Template By Ridwan Hex And Game Gratis