Mwanafalsafa

  • HOME
Home → Habari → Michezo → Tatizo la kuwapo bandari bubu linazidi kuongezeka.

Tatizo la kuwapo bandari bubu linazidi kuongezeka.

Habari, Michezo
Wednesday, 26 November 2014


Rais Jakaya Kikwete.PICHA|MAKTABA 

 Jeshi la Polisi mkoani Tanga juzi lilisema kwamba kuna zaidi ya bandari bubu 50 katika mkoa huo ambazo zinaingiza bidhaa ambazo hazilipiwi ushuru, huku nyingine zikiwa bandia.


Laiti Rais Jakaya Kikwete angekuwa na utaratibu wa Serikali yake kufanya tathmini endelevu ya utekelezaji wa kazi wa mawaziri katika wizara zote, angegundua kwamba zipo baadhi ya wizara ambazo viongozi wake ni mizigo isiyobebeka kutokana na kutofanya kazi, huku wakilipwa mishahara minono. Mfano hai ni Wizara ya Viwanda na Biashara, ambayo kwa muda mrefu sasa imekuwa ikilalamikiwa na wananchi kwa kutotimiza majukumu yake. Ni wizara ambayo wananchi wengi wanasema haina lolote la kujivunia, kinyume na baadhi ya wizara, ambazo utendaji kazi wa mawaziri wake siyo tu umetukuka, bali pia ni wa kutolea mfano.
Wakati wa kuzindua mpango wa Serikali wa Matokeo Makubwa Sasa (BRN) miezi kadhaa iliyopita, tuliambiwa kwamba mawaziri wote walipewa malengo ya utekelezaji wa mpango huo na kwamba kila waziri alisaini mkataba maalumu mbele ya Rais Kikwete, ‘akila kiapo’ kutekeleza majukumu hayo kwa mujibu wa mkataba huo. Vinginevyo angewajibishwa, kwa maana ya kupoteza kazi yake. Wapo mawaziri ambao wameonyesha uwajibikaji mkubwa katika utekelezaji wa malengo yaliyowekwa, lakini pia wapo mawaziri ambao wameendelea kufanya kazi kwa mazoea.
Pamoja na changamoto nyingi zinazoikabili Wizara ya Viwanda na Biashara, wananchi hawaoni nini kinafanyika katika kukabili changamoto hizo. Jana katika safu hii tulizungumzia changamoto ya ukosefu wa masoko kwa mazao ya biashara na chakula, tukisema wakulima wameachwa njia panda kwa mazao yao kutonunuliwa, huku wakibakia katika umaskini uliopitiliza.
Tunapozungumzia masoko tuna maana ya masoko ya ndani na nje ya nchi. Tani zaidi ya 16 milioni za mahindi ya wakulima zilizorundikana katika mikoa ya Morogoro, Rukwa, Katavi, Mbeya na Iringa kwa kukosa soko ni ushahidi usioacha shaka kwamba wizara inayohusika na biashara haina mbinu na mikakati ya kumaliza kero hiyo.
Ni kazi ya wizara hiyo kwa kushirikiana na wizara inayohusika na uwezeshaji kuwaunganisha wakulima na mitandao ya masoko mbalimbali. Sukari inayozalishwa nchini imelundikana katika maghala kwa kukosa soko, huku bidhaa hiyo kutoka nje ikiingizwa nchini kwa bei ndogo kwa sababu ya kutolipiwa kodi. Wizara hiyo haijui kinachoendelea, ingawa inazo habari kwamba bidhaa nyingi zisizolipiwa ushuru zinaingizwa nchini kupitia bandari nyingi bubu zilizoenea katika maeneo ya Pwani ya Bahari ya Hindi, yakiwamo maeneo ya Mbweni, Mlingotini, Ununio, Kawe, Msasani, Kunduchi, Kigamboni, Tegeta na Bagamoyo.
Tatizo la kuwapo bandari bubu linazidi kuongezeka. Jeshi la Polisi mkoani Tanga juzi lilisema kwamba kuna zaidi ya bandari bubu 50 katika mkoa huo ambazo zinaingiza bidhaa ambazo hazilipiwi ushuru, huku nyingine zikiwa bandia. Itakumbukwa kuwa, Waziri wa Biashara na Viwanda, Abdallah Kigoda alisema bungeni mwaka 2013 kuhusu kuwapo kwa bandari bubu na upitishaji wa bidhaa bandia katika maeneo mengi nchini. Kwa nini wizara husika haichukui hatua ni swali ambalo pengine linaweza kujibiwa na waziri huyo pekee.
Ndiyo maana wananchi wengi wanasema wizara hiyo ni mzigo, kwani imeshindwa siyo tu kuendeleza viwanda vidogovidogo, bali pia kuanzisha viwanda vya kusindika matunda kama nanasi, nyanya, maembe na machungwa ili wakulima wapate masoko ya mazao hayo. Ni kwa sababu hiyo tunasema wizara hiyo inahitaji waziri na watendaji wenye ubunifu na moyo wa kuwatumikia wananchi.

Share this article :
Tweet
✚
Newer Post
Older Post
Home

HABARI ZILIZO BAMBA TOP 10

  • Umuhimu wa kushirikiana katika kazi hasa ya muziki
  • Wiki hii katika mtandao wa kijamii, whatsapp , Ni sheedah cheki picha kali hapa chini !
  • Mwanasheria mkuu wa serikali nchini Mexico, Jesus Murillo Karam,ametoa ahadi kuwa hakutakuwa na uonevu wowote katika kesi ya kupotea kwa wanafunzi nchi humo miezi miwili iliyopita
    . Kutoweka kwa wanafunzi hao kumesababisha maandamano ya wiki kadhaa nchini humo waandamanaji wakipinda rushwa na ukatili...
  • Ni majonzi makubwa Tazama picha za wana familia za wachimba machimbo ya kokoto waliouawa na Al Shabaab mjini Mandera
    Familia za wachimba machimbo ya kokoto waliouawa na Al Shabaab mjini Mandera leo waliwapokea wapendwa wao baada ya miili yao kufikishwa ch...
  • After more than two years of tension over a territorial row,the leaders of China and Japan hold formal talks on the sidelines of a major Asian summit.
    Chinese President Xi Jinping and Japanese PM Shinzo Abe met on the sidelines of the Asia-Pacific Economic Co-operation (Apec) summit in B...
  • CCM KUTOICHUKULIA HATUA AKAUNTI YA ESCROW
    Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye, alisema kuwa CCM haina mpango wa kuchukua hatua zozote dhidi ya wote waliotajwa kuh...
  • A hardline cleric in Pakistan is teaching the ideas of Osama Bin Laden in religious schools for about 5,000 children.
       Even while the Pakistani government fights the Taliban in the north-west of the country, it has no plans to clos...
  • Lorna Rutto is an entrepreneur who founded Ecopost, a Nairobi-based company that recycles plastic waste
    Lorna Rutto is an entrepreneur who founded Ecopost, a Nairobi-based company that recycles plastic waste. As part of the latest series o...
  • AJIITA KIJANA MWENYE BAHATI AKIWA KATIKATI YA WAREMBO WAWILI
  • The actress best known for playing the unseen role of Howard Wolowitz's mother on The Big Bang Theory has died.
      Big Bang Theory's Mrs Wolowitz dies at the age of 62 Carol Ann Susi had played the role of Mrs Wolowitz since 2007   ...

LABELS

  • Breaking News
  • condolonces
  • Entertainment
  • Entertainments
  • Habari
  • Majonzi
  • Michezo
  • News
  • News and Updates
  • Skendo
  • Sports and Games
Submit ExpressSEO Services & Tools

Total Pageviews

Copyright 2014 Mwanafalsafa
Template By Ridwan Hex And Game Gratis