Mwanafalsafa

  • HOME
Home → Habari → MKUU wa Wilaya ya Mufindi mkoani Iringa, Evarista Kalalu, awashauri wananchi kujiunga na mfuko wa afya ya jamii

MKUU wa Wilaya ya Mufindi mkoani Iringa, Evarista Kalalu, awashauri wananchi kujiunga na mfuko wa afya ya jamii

Habari
Friday, 5 December 2014
MKUU wa Wilaya ya Mufindi mkoani Iringa, Evarista Kalalu, amewashauri wananchi wa vijiji vya Ukami na Chogo Kata ya Mapanda wilayani hapa na viongozi wa ngazi mbalimbali wakiwemo wenyeviti wa vitongoji, kujiunga na Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF), ikiwa ni njia ya kuondokana na gharama za matibabu kipindi hawana fedha.
Kalalu, aliyasema hayo wakati akizungumza kwenye siku ya uzinduzi wa kampeni ya kuhamasisha wananchi kujiunga na mfuko huo, ili kujihakikishia matibabu stahiki kupindi chote hata kile ambacho watakuwa hawana fedha.
Alisema kaya nyingi zinashindwa kupata matibabu pindi wanapokosa fedha, kwa kushindwa kufahamu umuhimu wa mfuko wa jamii na kujiunga nao na kuwataka kujiunga nao kwani una faida nyingi kwa wananchi wa kipato cha chini pindi wanapokosa fedha za matibabu.
“Uelimishaji unahitajika kuanzia ngazi ya vitongoji, vijiji, Kata na Tarafa kwa kufanya mikutano ya kuhamasisha na uelimishaji. Pia wenyeviti wa vitongoji, watendaji na wengineo ambao bado hawajajiunga na mfuko huu, muonyeshe mfano kwa kujiunga na kuweza kuwashawishi wananchi waliowengi katika vijiji mnavyoishi kujiunga katika Mfuko wa Afya ya Jamii kwa lengo la kuondokana na gharama nyingi zaidi,” alisema.
Aidha, Kalalu alizitaja faida za mfuko huo kuwa ni mwananchi kupata huduma ya matibabu wakati wote hata kama hana fedha na mfuko utatoa uhakika wa upatikanaji wa dawa na vifaa tiba mwaka mzima kwa kuchangia sh 5,000 kwa mwaka.
Awali, Meneja wa CHF Mkoa wa Iringa, Emmanuel Mkwabi, alisema kuwa mfuko huo ni mkombozi halisi wa Mtanzania wa kipato cha chini, kwa kuwa ni ukweli usiopingika  kwamba ugonjwa hautoi taarifa, hauchagui siku wala mtu, hivyo upo uwezekano mkubwa kumpata mtu akiwa hana fedha kabisa.

Share this article :
Tweet
✚
Newer Post
Older Post
Home

HABARI ZILIZO BAMBA TOP 10

  • Lorna Rutto is an entrepreneur who founded Ecopost, a Nairobi-based company that recycles plastic waste
    Lorna Rutto is an entrepreneur who founded Ecopost, a Nairobi-based company that recycles plastic waste. As part of the latest series o...
  • Ajali ya gari huko south B kenya
    There was a bizarre accident today morning in Hazina Estate, South B involving a Range Rover that crashed into 7 vehicles. The Ran...
  • Jennifer Lawrence has joined her castmates at the world premiere of the penultimate Hunger Games movie, Mockingjay Part 1, in London.
    Lawrence plays the heroine Katniss Everdeen in the hit franchise Jennifer Lawrence has joined her castmates at the w...
  • Catalonia's regional president Artur Mas says an official referendum is needed following Catalonia vote: 80% back independence - officials
    \ An informal vote on independence for Catalonia has shown more than 80% in favour, officials say. The non-binding vote went ahead after ...
  • After more than two years of tension over a territorial row,the leaders of China and Japan hold formal talks on the sidelines of a major Asian summit.
    Chinese President Xi Jinping and Japanese PM Shinzo Abe met on the sidelines of the Asia-Pacific Economic Co-operation (Apec) summit in B...
  • MAREKANI YAITUPIA LAWAMA KOREA KASKAZINI
    Marekani inatarajia kuirudisha Korea kaskazini katika orodha ya nchi zinazofadhili ugaidi. Rais Barack Obama wa Marekani amesema utawala ...
  • The poorest president, Jose Mujica gets $1m offer for his VW Beetle
    7 November 2014 Last updated at 07:04 GMT Uruguay's President Jose Mujica says he has been offered $1m (£630,000) for his vinta...
  • Report says,Fossil fuel promises are being broken,World governments have been breaking promises to phase out subsidies for fossil fuels, a report says.
    The report said G20 nations had been spending almost $90bn a year on finding more oil, g...
  • Wabunge wa Somali wameng'oa waziri mkuu
    Ni mara ya nne kwamba kura ya kutokuwa na imani dhidi yake ilipigwa baada ya majaribio ya awali kumalizika kwa ghasia. Waandishi ...
  • AJIITA KIJANA MWENYE BAHATI AKIWA KATIKATI YA WAREMBO WAWILI

LABELS

  • Breaking News
  • condolonces
  • Entertainment
  • Entertainments
  • Habari
  • Majonzi
  • Michezo
  • News
  • News and Updates
  • Skendo
  • Sports and Games
Submit ExpressSEO Services & Tools

Total Pageviews

Copyright 2014 Mwanafalsafa
Template By Ridwan Hex And Game Gratis