Mwanafalsafa

  • HOME
Home → Habari → MKUU wa Wilaya ya Mufindi mkoani Iringa, Evarista Kalalu, awashauri wananchi kujiunga na mfuko wa afya ya jamii

MKUU wa Wilaya ya Mufindi mkoani Iringa, Evarista Kalalu, awashauri wananchi kujiunga na mfuko wa afya ya jamii

Habari
Friday, 5 December 2014
MKUU wa Wilaya ya Mufindi mkoani Iringa, Evarista Kalalu, amewashauri wananchi wa vijiji vya Ukami na Chogo Kata ya Mapanda wilayani hapa na viongozi wa ngazi mbalimbali wakiwemo wenyeviti wa vitongoji, kujiunga na Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF), ikiwa ni njia ya kuondokana na gharama za matibabu kipindi hawana fedha.
Kalalu, aliyasema hayo wakati akizungumza kwenye siku ya uzinduzi wa kampeni ya kuhamasisha wananchi kujiunga na mfuko huo, ili kujihakikishia matibabu stahiki kupindi chote hata kile ambacho watakuwa hawana fedha.
Alisema kaya nyingi zinashindwa kupata matibabu pindi wanapokosa fedha, kwa kushindwa kufahamu umuhimu wa mfuko wa jamii na kujiunga nao na kuwataka kujiunga nao kwani una faida nyingi kwa wananchi wa kipato cha chini pindi wanapokosa fedha za matibabu.
“Uelimishaji unahitajika kuanzia ngazi ya vitongoji, vijiji, Kata na Tarafa kwa kufanya mikutano ya kuhamasisha na uelimishaji. Pia wenyeviti wa vitongoji, watendaji na wengineo ambao bado hawajajiunga na mfuko huu, muonyeshe mfano kwa kujiunga na kuweza kuwashawishi wananchi waliowengi katika vijiji mnavyoishi kujiunga katika Mfuko wa Afya ya Jamii kwa lengo la kuondokana na gharama nyingi zaidi,” alisema.
Aidha, Kalalu alizitaja faida za mfuko huo kuwa ni mwananchi kupata huduma ya matibabu wakati wote hata kama hana fedha na mfuko utatoa uhakika wa upatikanaji wa dawa na vifaa tiba mwaka mzima kwa kuchangia sh 5,000 kwa mwaka.
Awali, Meneja wa CHF Mkoa wa Iringa, Emmanuel Mkwabi, alisema kuwa mfuko huo ni mkombozi halisi wa Mtanzania wa kipato cha chini, kwa kuwa ni ukweli usiopingika  kwamba ugonjwa hautoi taarifa, hauchagui siku wala mtu, hivyo upo uwezekano mkubwa kumpata mtu akiwa hana fedha kabisa.

Share this article :
Tweet
✚
Newer Post
Older Post
Home

HABARI ZILIZO BAMBA TOP 10

  • MAREKANI YAITUPIA LAWAMA KOREA KASKAZINI
    Marekani inatarajia kuirudisha Korea kaskazini katika orodha ya nchi zinazofadhili ugaidi. Rais Barack Obama wa Marekani amesema utawala ...
  • MKUU wa Wilaya ya Mufindi mkoani Iringa, Evarista Kalalu, awashauri wananchi kujiunga na mfuko wa afya ya jamii
    MKUU wa Wilaya ya Mufindi mkoani Iringa, Evarista Kalalu, amewashauri wananchi wa vijiji vya Ukami na Chogo Kata ya Mapanda wilayani hapa...
  • KAULI YA UHURU KWENYE MTANDAOWA KIJAMII (TWITTER) KENYATTA HII HAPA
    Taarifa ya mahakama ya ICC, kutupilia mbali kesi dhidi ya Uhuru Kenyatta, imepokelwa na watu wengi nchini Kenya kwa hisia mseto. Baadhi w...
  • HAYA NDIO MAZITO ALIYO FUNGUKA YULE MSICHANA WA KAZI ALIYE MPIGA MTOTO
    Baada ya story ya yule msichana kwa anayefanya kazi za ndani Uganda kuchukua headlines katika vyombo mbalimbali vya Kimataifa Dun...
  • Ronaldo aosha vyombo baada ya kushindwa katika karata na mchezaji wa Tenisi Rafa Nadal
    Ali...
  • Wayne Goss, former premier of Queensland, kicked the bucket at 63
    Mr Goss, who was premier from 1989 to 1996, had suffered from ill health in recent years including brain tumours. He became Q...
  • IT 'S MATTER OF FEW MINUTES FOR WORLD CUP 2014 START SHINNING !!!!
    The World Cup  The 2014  Brazil™ is now just a matter of minutes away and to mark the occasion FIFA have launched an updated version of th...

LABELS

  • Breaking News
  • condolonces
  • Entertainment
  • Entertainments
  • Habari
  • Majonzi
  • Michezo
  • News
  • News and Updates
  • Skendo
  • Sports and Games
Submit ExpressSEO Services & Tools

Total Pageviews

Copyright 2014 Mwanafalsafa
Template By Ridwan Hex And Game Gratis