Mwanafalsafa

  • HOME
Home → Habari → MKUU wa Wilaya ya Mufindi mkoani Iringa, Evarista Kalalu, awashauri wananchi kujiunga na mfuko wa afya ya jamii

MKUU wa Wilaya ya Mufindi mkoani Iringa, Evarista Kalalu, awashauri wananchi kujiunga na mfuko wa afya ya jamii

Habari
Friday, 5 December 2014
MKUU wa Wilaya ya Mufindi mkoani Iringa, Evarista Kalalu, amewashauri wananchi wa vijiji vya Ukami na Chogo Kata ya Mapanda wilayani hapa na viongozi wa ngazi mbalimbali wakiwemo wenyeviti wa vitongoji, kujiunga na Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF), ikiwa ni njia ya kuondokana na gharama za matibabu kipindi hawana fedha.
Kalalu, aliyasema hayo wakati akizungumza kwenye siku ya uzinduzi wa kampeni ya kuhamasisha wananchi kujiunga na mfuko huo, ili kujihakikishia matibabu stahiki kupindi chote hata kile ambacho watakuwa hawana fedha.
Alisema kaya nyingi zinashindwa kupata matibabu pindi wanapokosa fedha, kwa kushindwa kufahamu umuhimu wa mfuko wa jamii na kujiunga nao na kuwataka kujiunga nao kwani una faida nyingi kwa wananchi wa kipato cha chini pindi wanapokosa fedha za matibabu.
“Uelimishaji unahitajika kuanzia ngazi ya vitongoji, vijiji, Kata na Tarafa kwa kufanya mikutano ya kuhamasisha na uelimishaji. Pia wenyeviti wa vitongoji, watendaji na wengineo ambao bado hawajajiunga na mfuko huu, muonyeshe mfano kwa kujiunga na kuweza kuwashawishi wananchi waliowengi katika vijiji mnavyoishi kujiunga katika Mfuko wa Afya ya Jamii kwa lengo la kuondokana na gharama nyingi zaidi,” alisema.
Aidha, Kalalu alizitaja faida za mfuko huo kuwa ni mwananchi kupata huduma ya matibabu wakati wote hata kama hana fedha na mfuko utatoa uhakika wa upatikanaji wa dawa na vifaa tiba mwaka mzima kwa kuchangia sh 5,000 kwa mwaka.
Awali, Meneja wa CHF Mkoa wa Iringa, Emmanuel Mkwabi, alisema kuwa mfuko huo ni mkombozi halisi wa Mtanzania wa kipato cha chini, kwa kuwa ni ukweli usiopingika  kwamba ugonjwa hautoi taarifa, hauchagui siku wala mtu, hivyo upo uwezekano mkubwa kumpata mtu akiwa hana fedha kabisa.

Share this article :
Tweet
✚
Newer Post
Older Post
Home

HABARI ZILIZO BAMBA TOP 10

  • Takribani watu 15 wapata upofu baada ya upasuaji nchini India
    Wagonjwa waliofanyiwa upasuaji walisema walishindwa kuona tena baada ya kuondoa bandeji kwenye macho yao Maafisa wa utawala nchini Indiaa w...
  • Familia ya mateka yasihi Al Qaeda kumwachilia
    Marekani imeeleza kuwa ilijaribu kumwokoa raia wake mzaliwa wa Uingereza Luke Somers, anayeshikiliwa mateka na al-Qaeda nchini Yemen. ...
  • Ona kilichotokea kwa jimama hili kipindi lina jaribu kucheza jirani na swimming pool.Noii huko Kenya mida ya jana jioni
       
  • AJIITA KIJANA MWENYE BAHATI AKIWA KATIKATI YA WAREMBO WAWILI
  • BRAZIL TO EDGE OUT GERMANY IN WORLD CUP SEMI FINAL
  • KAULI YA UHURU KWENYE MTANDAOWA KIJAMII (TWITTER) KENYATTA HII HAPA
    Taarifa ya mahakama ya ICC, kutupilia mbali kesi dhidi ya Uhuru Kenyatta, imepokelwa na watu wengi nchini Kenya kwa hisia mseto. Baadhi w...
  • Maandano zidi ya kutupiliwa mbali kwa kesi ya afisa polisi mjini New York
    Maandamano mjini New York Waandamanaji wameingia katika barabara za miji mingi Nchini Marekani kwa usiku wa pili mtawalia, kupinga maamu...
  • Jennifer Lawrence has joined her castmates at the world premiere of the penultimate Hunger Games movie, Mockingjay Part 1, in London.
    Lawrence plays the heroine Katniss Everdeen in the hit franchise Jennifer Lawrence has joined her castmates at the w...
  • MORE THAN 10,000 GRADUATES TURN UP FOR SEVENTY JOB VACANCIES IN DAR ES SLAAM.
    According to the list of names seen by The Guardian yesterday morning, the department listed 10,816 candidates to perform the interview tha...
  • Mshindi wa Nishani ya Nobel bint Malala amenukuliwa akisema "Nataka kuwa Waziri mkuu''
    Mshindi wa Nishani ya Nobel bint Malala Yousafzai raia wa Pakistani amesema kuwa siku zijazo anatarajia kuwa mwanasiasa. Malala a...

LABELS

  • Breaking News
  • condolonces
  • Entertainment
  • Entertainments
  • Habari
  • Majonzi
  • Michezo
  • News
  • News and Updates
  • Skendo
  • Sports and Games
Submit ExpressSEO Services & Tools

Total Pageviews

Copyright 2014 Mwanafalsafa
Template By Ridwan Hex And Game Gratis