Mwanafalsafa

  • HOME
Home → Habari → Sintofahamu yaibuka juu ya maelezo ya kifo cha aliyekuwa mshitakiwa wa ugaidi.

Sintofahamu yaibuka juu ya maelezo ya kifo cha aliyekuwa mshitakiwa wa ugaidi.

Habari
Friday, 5 December 2014






WAKATI Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha ikielezwa kuwa taratibu za mazishi ya mtuhumiwa wa pili katika kesi ya ugaidi ya tukio la mlipuko wa bomu katika Baa ya Arusha Night Park, Ustadhi Abdulkarim Thabit, zinaendelea, imefahamika kuwa mtuhumiwa huyo alishazikwa tangu Desemba 2 mwaka huu.
Mmoja wa Askari Magereza ambaye jina lake halikuweza kupatikana mara moja, jana aliieleza Mahakama hiyo mbele ya Hakimu Mkazi, Hawa Mguruta, kuwa mtuhumiwa huyo alifariki Desemba Mosi mwaka huu, kwenye Hospitali ya Mkoa wa Arusha, Mount Meru alipokuwa amelazwa tangu akamatwe na taratibu za mazishi zinaendelea.
Baadhi ya magaidi wa mabomu Arusha
Kesi hiyo na nyingine 13 ambazo zimepangwa kutajwa siku moja katika Mahakama hiyo, ziliahirishwa hadi Desemba 19 mwaka huu, kutokana na upelelezi wake kutokamilika.
Aidha, watuhumiwa hao walipoanza kuitwa majina yao, askari huyo aliieleza Mahakma kuwa, Thabit amefariki dunia na mazishi yanashughulikiwa.
Hata hivyo, Wakili wa Serikali, Agustino Kombe, aliieleza Mahakama hiyo kuwa, upande wa Jamhuri haukuwa na taarifa hizo ambako wakipata taarifa hiyo kutoka Magereza wataleta maombi mahakamani hapo kubadili hati ya mashitaka ili wamuondoe mshtakiwa huyo aliyefariki.
Kwa upande wake, Ustaadhi wa msikiti wa Hospitali ya Mkoa ya Mount Meru, Shaaban Salum, alisema alipata taarifa za kufariki kwa Ustadhi Thabit Desemba 2 mwaka huu majira ya saa 1:00 asubuhi.
Alisema kuwa, kipindi chote alichokuwa akipatiwa matibabu hospitalini hapo, alikuwa akimnunulia dawa za kumsafisha vidonda alizokuwa akiagizwa na manesi na madaktari waliokuwa wakimuhudumia, lakini hakuwahi kumuona kwani alikuwa chini ya ulinzi mkali wa askari Magereza.
“Mimi Askari Magereza alinifuata pale msikitini akaniambia Ustaadhi Thabit alifariki jana (Desemba 1, mwaka huu) majira ya saa 11 jioni, kwenye saa 2:30 asubuhi, wakaja ndugu zake tukaenda chumba cha kuhifadhia maiti…
“Tulimkuta ana vidonda mgongoni na kwenye makalio… tulipotoka pale tukaenda kuandaa mazishi. Tulimzika siku hiyohiyo kwenye makaburi ya Waislamu Njiro,” alisema Ustaadhi Salum.
Katika kesi hiyo, marehemu Ustadhi Thabit, anadaiwa yeye  na washtakiwa  wenzake, wanadaiwa kufanya  uwakala na kusajili vijana kujiunga na kikundi cha kigaidi cha  Al-Shabaab  cha nchini Somalia.
Wanadaiwa kuhusika na tukio la ugaidi la kurusha bomu katika baa ya  Arusha Night Park iliyopo jijini hapa na kusababisha kifo cha mtu mmoja na kujeruhi wengine 15, Aprili 14 Mwaka huu.
Hata hivyo, mshtakiwa huyo tangu akamatwe hakuweza kufika mahakamani,ambako alilazwa katika hospitali hiyo na kusomewa mashitaka akiwa wodini.


Mganga Mkuu wa Hospitali ya Mount Meru, Dk. Josian Mlaya, alithibitisha kuwa Ustaadhi Thabit alifariki Desemba Mosi mwaka huu, ingawa hakuwa tayari kuingia kwa undani juu ya chanzo cha kifo hicho.







Share this article :
Tweet
✚
Newer Post
Older Post
Home

HABARI ZILIZO BAMBA TOP 10

  • MAREKANI YAITUPIA LAWAMA KOREA KASKAZINI
    Marekani inatarajia kuirudisha Korea kaskazini katika orodha ya nchi zinazofadhili ugaidi. Rais Barack Obama wa Marekani amesema utawala ...
  • Mamboya whatsapp haya hapa.!!!!! (18+)
  • SIMBA Vs EXPRESS YA UGANDA ,0-0 LEO UWANJA WA TAIFA
    Katongole Henry akimtoka mshambulia wa Simba, Ramadhani Singano 'Mess'. Kipa wa The Express, Mutumba Ivan akir...
  • Ronaldo aosha vyombo baada ya kushindwa katika karata na mchezaji wa Tenisi Rafa Nadal
    Ali...
  • AKOTHEE Takes Her Beautiful Daughters TO FLY OVER ! look at these beautiful photos.
  • APIGWA MVUA YA MIAKA 60 JELA, KWA KUTOROSHA TWIGA
    HATIMAYE Mahakama ya hakimu mkazi Moshi, mkoani Kilimanjaro, imemhukumu miaka 60 jela, Kamran Ahmed, raia wa Pakistani kwa kosa la kutoro...
  • John Doar, a civil rights lawyer who was a key figure in the struggle against racial segregation in the US, has died aged 92.
    John Doar was awarded the Presidential Medal of Freedom in 2012 Mr Doar dealt with some of the most prominent civil rights ca...
  • TEKNOLOGIA:GARI LINALOWEZA KUPAKI LENYEWE KWA KUTUMIA SAA YA SMARTPHONE BILA KUWA NA DEREVA NDANI..
    Kampuni ya BMW imezindua kifaa ambacho kinawezesha gari lako kujiegesha lenyewe.. Hakuna kitu kibaya kama kusahau ulikoegesha gari lako ka...
  • Spotify's chief executive has defended its business model, saying it has paid out $2bn (£1.2bn) to the music industry to date.
      Daniel Ek pitches Spotify as a more lucrative alternative to piracy Daniel Ek's lengthy blog post follows a high profil...
  • Mapya ya Dk.Slaa kuhusu IPTL
    KATIBU Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Wilibrod Slaa, amesema fedha zilizochotwa katika Akaunti ya Tegeta ...

LABELS

  • Breaking News
  • condolonces
  • Entertainment
  • Entertainments
  • Habari
  • Majonzi
  • Michezo
  • News
  • News and Updates
  • Skendo
  • Sports and Games
Submit ExpressSEO Services & Tools

Total Pageviews

Copyright 2014 Mwanafalsafa
Template By Ridwan Hex And Game Gratis