Mwanafalsafa

  • HOME
Home → Habari → Sintofahamu yaibuka juu ya maelezo ya kifo cha aliyekuwa mshitakiwa wa ugaidi.

Sintofahamu yaibuka juu ya maelezo ya kifo cha aliyekuwa mshitakiwa wa ugaidi.

Habari
Friday, 5 December 2014






WAKATI Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha ikielezwa kuwa taratibu za mazishi ya mtuhumiwa wa pili katika kesi ya ugaidi ya tukio la mlipuko wa bomu katika Baa ya Arusha Night Park, Ustadhi Abdulkarim Thabit, zinaendelea, imefahamika kuwa mtuhumiwa huyo alishazikwa tangu Desemba 2 mwaka huu.
Mmoja wa Askari Magereza ambaye jina lake halikuweza kupatikana mara moja, jana aliieleza Mahakama hiyo mbele ya Hakimu Mkazi, Hawa Mguruta, kuwa mtuhumiwa huyo alifariki Desemba Mosi mwaka huu, kwenye Hospitali ya Mkoa wa Arusha, Mount Meru alipokuwa amelazwa tangu akamatwe na taratibu za mazishi zinaendelea.
Baadhi ya magaidi wa mabomu Arusha
Kesi hiyo na nyingine 13 ambazo zimepangwa kutajwa siku moja katika Mahakama hiyo, ziliahirishwa hadi Desemba 19 mwaka huu, kutokana na upelelezi wake kutokamilika.
Aidha, watuhumiwa hao walipoanza kuitwa majina yao, askari huyo aliieleza Mahakma kuwa, Thabit amefariki dunia na mazishi yanashughulikiwa.
Hata hivyo, Wakili wa Serikali, Agustino Kombe, aliieleza Mahakama hiyo kuwa, upande wa Jamhuri haukuwa na taarifa hizo ambako wakipata taarifa hiyo kutoka Magereza wataleta maombi mahakamani hapo kubadili hati ya mashitaka ili wamuondoe mshtakiwa huyo aliyefariki.
Kwa upande wake, Ustaadhi wa msikiti wa Hospitali ya Mkoa ya Mount Meru, Shaaban Salum, alisema alipata taarifa za kufariki kwa Ustadhi Thabit Desemba 2 mwaka huu majira ya saa 1:00 asubuhi.
Alisema kuwa, kipindi chote alichokuwa akipatiwa matibabu hospitalini hapo, alikuwa akimnunulia dawa za kumsafisha vidonda alizokuwa akiagizwa na manesi na madaktari waliokuwa wakimuhudumia, lakini hakuwahi kumuona kwani alikuwa chini ya ulinzi mkali wa askari Magereza.
“Mimi Askari Magereza alinifuata pale msikitini akaniambia Ustaadhi Thabit alifariki jana (Desemba 1, mwaka huu) majira ya saa 11 jioni, kwenye saa 2:30 asubuhi, wakaja ndugu zake tukaenda chumba cha kuhifadhia maiti…
“Tulimkuta ana vidonda mgongoni na kwenye makalio… tulipotoka pale tukaenda kuandaa mazishi. Tulimzika siku hiyohiyo kwenye makaburi ya Waislamu Njiro,” alisema Ustaadhi Salum.
Katika kesi hiyo, marehemu Ustadhi Thabit, anadaiwa yeye  na washtakiwa  wenzake, wanadaiwa kufanya  uwakala na kusajili vijana kujiunga na kikundi cha kigaidi cha  Al-Shabaab  cha nchini Somalia.
Wanadaiwa kuhusika na tukio la ugaidi la kurusha bomu katika baa ya  Arusha Night Park iliyopo jijini hapa na kusababisha kifo cha mtu mmoja na kujeruhi wengine 15, Aprili 14 Mwaka huu.
Hata hivyo, mshtakiwa huyo tangu akamatwe hakuweza kufika mahakamani,ambako alilazwa katika hospitali hiyo na kusomewa mashitaka akiwa wodini.


Mganga Mkuu wa Hospitali ya Mount Meru, Dk. Josian Mlaya, alithibitisha kuwa Ustaadhi Thabit alifariki Desemba Mosi mwaka huu, ingawa hakuwa tayari kuingia kwa undani juu ya chanzo cha kifo hicho.







Share this article :
Tweet
✚
Newer Post
Older Post
Home

HABARI ZILIZO BAMBA TOP 10

  • Lorna Rutto is an entrepreneur who founded Ecopost, a Nairobi-based company that recycles plastic waste
    Lorna Rutto is an entrepreneur who founded Ecopost, a Nairobi-based company that recycles plastic waste. As part of the latest series o...
  • The poorest president, Jose Mujica gets $1m offer for his VW Beetle
    7 November 2014 Last updated at 07:04 GMT Uruguay's President Jose Mujica says he has been offered $1m (£630,000) for his vinta...
  • Report says,Fossil fuel promises are being broken,World governments have been breaking promises to phase out subsidies for fossil fuels, a report says.
    The report said G20 nations had been spending almost $90bn a year on finding more oil, g...
  • Wabunge wa Somali wameng'oa waziri mkuu
    Ni mara ya nne kwamba kura ya kutokuwa na imani dhidi yake ilipigwa baada ya majaribio ya awali kumalizika kwa ghasia. Waandishi ...
  • AJIITA KIJANA MWENYE BAHATI AKIWA KATIKATI YA WAREMBO WAWILI
  • John Doar, a civil rights lawyer who was a key figure in the struggle against racial segregation in the US, has died aged 92.
    John Doar was awarded the Presidential Medal of Freedom in 2012 Mr Doar dealt with some of the most prominent civil rights ca...
  • Ukweli kuhusu umoja wa fedha,Jumuiya ya Afrika Mashariki.
      OKTOBA 20 hadi 24 mwaka  huu, Benki Kuu ya Tanzania (BoT) iliandaa semi...
  • BRAZIL TO EDGE OUT GERMANY IN WORLD CUP SEMI FINAL
  • Kiungo mpya wa Azam, Amri Kiemba akiwa katika jezi ya timu hiyo kwenye Uwanja wa Chamazi, Dar es Salaam jana
       Klabu ya Yanga imemleta nchini kwa majaribio mshambuliaji raia wa Zambia, Jonas Sakuwaha ...
  • Spotify's chief executive has defended its business model, saying it has paid out $2bn (£1.2bn) to the music industry to date.
      Daniel Ek pitches Spotify as a more lucrative alternative to piracy Daniel Ek's lengthy blog post follows a high profil...

LABELS

  • Breaking News
  • condolonces
  • Entertainment
  • Entertainments
  • Habari
  • Majonzi
  • Michezo
  • News
  • News and Updates
  • Skendo
  • Sports and Games
Submit ExpressSEO Services & Tools

Total Pageviews

Copyright 2014 Mwanafalsafa
Template By Ridwan Hex And Game Gratis