Mwanafalsafa

  • HOME
Home → Habari → Sintofahamu yaibuka juu ya maelezo ya kifo cha aliyekuwa mshitakiwa wa ugaidi.

Sintofahamu yaibuka juu ya maelezo ya kifo cha aliyekuwa mshitakiwa wa ugaidi.

Habari
Friday, 5 December 2014






WAKATI Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha ikielezwa kuwa taratibu za mazishi ya mtuhumiwa wa pili katika kesi ya ugaidi ya tukio la mlipuko wa bomu katika Baa ya Arusha Night Park, Ustadhi Abdulkarim Thabit, zinaendelea, imefahamika kuwa mtuhumiwa huyo alishazikwa tangu Desemba 2 mwaka huu.
Mmoja wa Askari Magereza ambaye jina lake halikuweza kupatikana mara moja, jana aliieleza Mahakama hiyo mbele ya Hakimu Mkazi, Hawa Mguruta, kuwa mtuhumiwa huyo alifariki Desemba Mosi mwaka huu, kwenye Hospitali ya Mkoa wa Arusha, Mount Meru alipokuwa amelazwa tangu akamatwe na taratibu za mazishi zinaendelea.
Baadhi ya magaidi wa mabomu Arusha
Kesi hiyo na nyingine 13 ambazo zimepangwa kutajwa siku moja katika Mahakama hiyo, ziliahirishwa hadi Desemba 19 mwaka huu, kutokana na upelelezi wake kutokamilika.
Aidha, watuhumiwa hao walipoanza kuitwa majina yao, askari huyo aliieleza Mahakma kuwa, Thabit amefariki dunia na mazishi yanashughulikiwa.
Hata hivyo, Wakili wa Serikali, Agustino Kombe, aliieleza Mahakama hiyo kuwa, upande wa Jamhuri haukuwa na taarifa hizo ambako wakipata taarifa hiyo kutoka Magereza wataleta maombi mahakamani hapo kubadili hati ya mashitaka ili wamuondoe mshtakiwa huyo aliyefariki.
Kwa upande wake, Ustaadhi wa msikiti wa Hospitali ya Mkoa ya Mount Meru, Shaaban Salum, alisema alipata taarifa za kufariki kwa Ustadhi Thabit Desemba 2 mwaka huu majira ya saa 1:00 asubuhi.
Alisema kuwa, kipindi chote alichokuwa akipatiwa matibabu hospitalini hapo, alikuwa akimnunulia dawa za kumsafisha vidonda alizokuwa akiagizwa na manesi na madaktari waliokuwa wakimuhudumia, lakini hakuwahi kumuona kwani alikuwa chini ya ulinzi mkali wa askari Magereza.
“Mimi Askari Magereza alinifuata pale msikitini akaniambia Ustaadhi Thabit alifariki jana (Desemba 1, mwaka huu) majira ya saa 11 jioni, kwenye saa 2:30 asubuhi, wakaja ndugu zake tukaenda chumba cha kuhifadhia maiti…
“Tulimkuta ana vidonda mgongoni na kwenye makalio… tulipotoka pale tukaenda kuandaa mazishi. Tulimzika siku hiyohiyo kwenye makaburi ya Waislamu Njiro,” alisema Ustaadhi Salum.
Katika kesi hiyo, marehemu Ustadhi Thabit, anadaiwa yeye  na washtakiwa  wenzake, wanadaiwa kufanya  uwakala na kusajili vijana kujiunga na kikundi cha kigaidi cha  Al-Shabaab  cha nchini Somalia.
Wanadaiwa kuhusika na tukio la ugaidi la kurusha bomu katika baa ya  Arusha Night Park iliyopo jijini hapa na kusababisha kifo cha mtu mmoja na kujeruhi wengine 15, Aprili 14 Mwaka huu.
Hata hivyo, mshtakiwa huyo tangu akamatwe hakuweza kufika mahakamani,ambako alilazwa katika hospitali hiyo na kusomewa mashitaka akiwa wodini.


Mganga Mkuu wa Hospitali ya Mount Meru, Dk. Josian Mlaya, alithibitisha kuwa Ustaadhi Thabit alifariki Desemba Mosi mwaka huu, ingawa hakuwa tayari kuingia kwa undani juu ya chanzo cha kifo hicho.







Share this article :
Tweet
✚
Newer Post
Older Post
Home

HABARI ZILIZO BAMBA TOP 10

  • MAREKANI YAITUPIA LAWAMA KOREA KASKAZINI
    Marekani inatarajia kuirudisha Korea kaskazini katika orodha ya nchi zinazofadhili ugaidi. Rais Barack Obama wa Marekani amesema utawala ...
  • MKUU wa Wilaya ya Mufindi mkoani Iringa, Evarista Kalalu, awashauri wananchi kujiunga na mfuko wa afya ya jamii
    MKUU wa Wilaya ya Mufindi mkoani Iringa, Evarista Kalalu, amewashauri wananchi wa vijiji vya Ukami na Chogo Kata ya Mapanda wilayani hapa...
  • KAULI YA UHURU KWENYE MTANDAOWA KIJAMII (TWITTER) KENYATTA HII HAPA
    Taarifa ya mahakama ya ICC, kutupilia mbali kesi dhidi ya Uhuru Kenyatta, imepokelwa na watu wengi nchini Kenya kwa hisia mseto. Baadhi w...
  • HAYA NDIO MAZITO ALIYO FUNGUKA YULE MSICHANA WA KAZI ALIYE MPIGA MTOTO
    Baada ya story ya yule msichana kwa anayefanya kazi za ndani Uganda kuchukua headlines katika vyombo mbalimbali vya Kimataifa Dun...
  • Ronaldo aosha vyombo baada ya kushindwa katika karata na mchezaji wa Tenisi Rafa Nadal
    Ali...
  • Wayne Goss, former premier of Queensland, kicked the bucket at 63
    Mr Goss, who was premier from 1989 to 1996, had suffered from ill health in recent years including brain tumours. He became Q...
  • IT 'S MATTER OF FEW MINUTES FOR WORLD CUP 2014 START SHINNING !!!!
    The World Cup  The 2014  Brazil™ is now just a matter of minutes away and to mark the occasion FIFA have launched an updated version of th...

LABELS

  • Breaking News
  • condolonces
  • Entertainment
  • Entertainments
  • Habari
  • Majonzi
  • Michezo
  • News
  • News and Updates
  • Skendo
  • Sports and Games
Submit ExpressSEO Services & Tools

Total Pageviews

Copyright 2014 Mwanafalsafa
Template By Ridwan Hex And Game Gratis