Mwanafalsafa

  • HOME
Home → Habari → Sintofahamu yaibuka juu ya maelezo ya kifo cha aliyekuwa mshitakiwa wa ugaidi.

Sintofahamu yaibuka juu ya maelezo ya kifo cha aliyekuwa mshitakiwa wa ugaidi.

Habari
Friday, 5 December 2014






WAKATI Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha ikielezwa kuwa taratibu za mazishi ya mtuhumiwa wa pili katika kesi ya ugaidi ya tukio la mlipuko wa bomu katika Baa ya Arusha Night Park, Ustadhi Abdulkarim Thabit, zinaendelea, imefahamika kuwa mtuhumiwa huyo alishazikwa tangu Desemba 2 mwaka huu.
Mmoja wa Askari Magereza ambaye jina lake halikuweza kupatikana mara moja, jana aliieleza Mahakama hiyo mbele ya Hakimu Mkazi, Hawa Mguruta, kuwa mtuhumiwa huyo alifariki Desemba Mosi mwaka huu, kwenye Hospitali ya Mkoa wa Arusha, Mount Meru alipokuwa amelazwa tangu akamatwe na taratibu za mazishi zinaendelea.
Baadhi ya magaidi wa mabomu Arusha
Kesi hiyo na nyingine 13 ambazo zimepangwa kutajwa siku moja katika Mahakama hiyo, ziliahirishwa hadi Desemba 19 mwaka huu, kutokana na upelelezi wake kutokamilika.
Aidha, watuhumiwa hao walipoanza kuitwa majina yao, askari huyo aliieleza Mahakma kuwa, Thabit amefariki dunia na mazishi yanashughulikiwa.
Hata hivyo, Wakili wa Serikali, Agustino Kombe, aliieleza Mahakama hiyo kuwa, upande wa Jamhuri haukuwa na taarifa hizo ambako wakipata taarifa hiyo kutoka Magereza wataleta maombi mahakamani hapo kubadili hati ya mashitaka ili wamuondoe mshtakiwa huyo aliyefariki.
Kwa upande wake, Ustaadhi wa msikiti wa Hospitali ya Mkoa ya Mount Meru, Shaaban Salum, alisema alipata taarifa za kufariki kwa Ustadhi Thabit Desemba 2 mwaka huu majira ya saa 1:00 asubuhi.
Alisema kuwa, kipindi chote alichokuwa akipatiwa matibabu hospitalini hapo, alikuwa akimnunulia dawa za kumsafisha vidonda alizokuwa akiagizwa na manesi na madaktari waliokuwa wakimuhudumia, lakini hakuwahi kumuona kwani alikuwa chini ya ulinzi mkali wa askari Magereza.
“Mimi Askari Magereza alinifuata pale msikitini akaniambia Ustaadhi Thabit alifariki jana (Desemba 1, mwaka huu) majira ya saa 11 jioni, kwenye saa 2:30 asubuhi, wakaja ndugu zake tukaenda chumba cha kuhifadhia maiti…
“Tulimkuta ana vidonda mgongoni na kwenye makalio… tulipotoka pale tukaenda kuandaa mazishi. Tulimzika siku hiyohiyo kwenye makaburi ya Waislamu Njiro,” alisema Ustaadhi Salum.
Katika kesi hiyo, marehemu Ustadhi Thabit, anadaiwa yeye  na washtakiwa  wenzake, wanadaiwa kufanya  uwakala na kusajili vijana kujiunga na kikundi cha kigaidi cha  Al-Shabaab  cha nchini Somalia.
Wanadaiwa kuhusika na tukio la ugaidi la kurusha bomu katika baa ya  Arusha Night Park iliyopo jijini hapa na kusababisha kifo cha mtu mmoja na kujeruhi wengine 15, Aprili 14 Mwaka huu.
Hata hivyo, mshtakiwa huyo tangu akamatwe hakuweza kufika mahakamani,ambako alilazwa katika hospitali hiyo na kusomewa mashitaka akiwa wodini.


Mganga Mkuu wa Hospitali ya Mount Meru, Dk. Josian Mlaya, alithibitisha kuwa Ustaadhi Thabit alifariki Desemba Mosi mwaka huu, ingawa hakuwa tayari kuingia kwa undani juu ya chanzo cha kifo hicho.







Share this article :
Tweet
✚
Newer Post
Older Post
Home

HABARI ZILIZO BAMBA TOP 10

  • Takribani watu 15 wapata upofu baada ya upasuaji nchini India
    Wagonjwa waliofanyiwa upasuaji walisema walishindwa kuona tena baada ya kuondoa bandeji kwenye macho yao Maafisa wa utawala nchini Indiaa w...
  • Familia ya mateka yasihi Al Qaeda kumwachilia
    Marekani imeeleza kuwa ilijaribu kumwokoa raia wake mzaliwa wa Uingereza Luke Somers, anayeshikiliwa mateka na al-Qaeda nchini Yemen. ...
  • Ona kilichotokea kwa jimama hili kipindi lina jaribu kucheza jirani na swimming pool.Noii huko Kenya mida ya jana jioni
       
  • AJIITA KIJANA MWENYE BAHATI AKIWA KATIKATI YA WAREMBO WAWILI
  • BRAZIL TO EDGE OUT GERMANY IN WORLD CUP SEMI FINAL
  • KAULI YA UHURU KWENYE MTANDAOWA KIJAMII (TWITTER) KENYATTA HII HAPA
    Taarifa ya mahakama ya ICC, kutupilia mbali kesi dhidi ya Uhuru Kenyatta, imepokelwa na watu wengi nchini Kenya kwa hisia mseto. Baadhi w...
  • Maandano zidi ya kutupiliwa mbali kwa kesi ya afisa polisi mjini New York
    Maandamano mjini New York Waandamanaji wameingia katika barabara za miji mingi Nchini Marekani kwa usiku wa pili mtawalia, kupinga maamu...
  • Jennifer Lawrence has joined her castmates at the world premiere of the penultimate Hunger Games movie, Mockingjay Part 1, in London.
    Lawrence plays the heroine Katniss Everdeen in the hit franchise Jennifer Lawrence has joined her castmates at the w...
  • MORE THAN 10,000 GRADUATES TURN UP FOR SEVENTY JOB VACANCIES IN DAR ES SLAAM.
    According to the list of names seen by The Guardian yesterday morning, the department listed 10,816 candidates to perform the interview tha...
  • Mshindi wa Nishani ya Nobel bint Malala amenukuliwa akisema "Nataka kuwa Waziri mkuu''
    Mshindi wa Nishani ya Nobel bint Malala Yousafzai raia wa Pakistani amesema kuwa siku zijazo anatarajia kuwa mwanasiasa. Malala a...

LABELS

  • Breaking News
  • condolonces
  • Entertainment
  • Entertainments
  • Habari
  • Majonzi
  • Michezo
  • News
  • News and Updates
  • Skendo
  • Sports and Games
Submit ExpressSEO Services & Tools

Total Pageviews

Copyright 2014 Mwanafalsafa
Template By Ridwan Hex And Game Gratis