Mwanafalsafa

  • HOME
Home → Entertainment → Kiungo mpya wa Azam, Amri Kiemba akiwa katika jezi ya timu hiyo kwenye Uwanja wa Chamazi, Dar es Salaam jana

Kiungo mpya wa Azam, Amri Kiemba akiwa katika jezi ya timu hiyo kwenye Uwanja wa Chamazi, Dar es Salaam jana

Entertainment
Tuesday, 25 November 2014


 

 Klabu ya Yanga imemleta nchini kwa majaribio mshambuliaji raia wa Zambia, Jonas Sakuwaha anayeichezea klabu ya TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
Sakuwaha (31), pia amewahi kucheza soka katika klabu ya Zesco United (Zambia), Lorient (Ufaransa), Le Havre (Ufaransa) na El-Merreikh (Sudan).
Kwa mujibu wa kiongozi mmoja wa Yanga, kama Sakuwaha atafuzu majaribio, basi atachukua nafasi ya Hamis Kiiza raia wa Uganda katika orodha ya wachezaji wake watano wa kigeni kwa mujibu wa kanuni za Shirikisho la Soka Tanzania (TFF).
Mbali na Kiiza, Haruna Niyonzima yuko hatarini kuiacha Yanga na tayari Azam FC imemkaribisha kundini ikijinasibu kuwa raia huyo wa Rwanda ni mchezaji wao.
Azam wamekuwa wakidai kuwa walikuwa wa kwanza kumsajili Niyonzima kabla ya kutua Yanga, lakini aliyekuwa kocha wao, Stewart Hall alimkataa kwa kigezo cha ufupi, ndipo walipomshauri ajiunge na Yanga.
Yanga tayari inao wachezaji watano wa kigeni ambao ni, Mbuyu Twite, Andrey Coutinho, Hamis Kiiza, Haruna Niyonzima na Mbrazili mpya, Emerson de Oliveira Neves Rouqe, anayetarajiwa kuwasili nchini kesho kuziba nafasi ya Mbrazili Genilson Santos ‘Jaja’.
Kuwasili kwa Sakuwaha aliyeichezea Zambia michuano mbalimbali ya kimataifa na pengine ujio wa Emerson ni mabadiliko yanayolenga kuimarisha mfumo wa uchezaji Yanga.
Hata hivyo, hilo litategemea kuondoka kwa Kiiza na Niyonzima, ambao wameonyesha nia ya kutotaka kubakia kwenye klabu hiyo.
Habari zilizolifikia gazeti hili jana zilieleza kuwa Sakuwaha atawasili nchini akifuatana na wachezaji wengine wanne kutoka Zambia kwa ajili ya majaribio.
Jana kulikuwa na habari kuwa mshambuliaji chipukizi wa Uganda, Yunus Sentamu anayeichezea AS Vita ya DRC, naye atatua Yanga.
Katika hatua nyingine, Emerson de Oliveira Neves Rouqe anatarajiwa kuwasili nchini kesho saa 7.00 mchana kwa ajili ya majaribio.

Share this article :
Tweet
✚
Newer Post
Older Post
Home

HABARI ZILIZO BAMBA TOP 10

  • MAREKANI YAITUPIA LAWAMA KOREA KASKAZINI
    Marekani inatarajia kuirudisha Korea kaskazini katika orodha ya nchi zinazofadhili ugaidi. Rais Barack Obama wa Marekani amesema utawala ...
  • HAYA NDIO MAZITO ALIYO FUNGUKA YULE MSICHANA WA KAZI ALIYE MPIGA MTOTO
    Baada ya story ya yule msichana kwa anayefanya kazi za ndani Uganda kuchukua headlines katika vyombo mbalimbali vya Kimataifa Dun...
  • Ronaldo aosha vyombo baada ya kushindwa katika karata na mchezaji wa Tenisi Rafa Nadal
    Ali...
  • Wayne Goss, former premier of Queensland, kicked the bucket at 63
    Mr Goss, who was premier from 1989 to 1996, had suffered from ill health in recent years including brain tumours. He became Q...
  • IT 'S MATTER OF FEW MINUTES FOR WORLD CUP 2014 START SHINNING !!!!
    The World Cup  The 2014  Brazil™ is now just a matter of minutes away and to mark the occasion FIFA have launched an updated version of th...

LABELS

  • Breaking News
  • condolonces
  • Entertainment
  • Entertainments
  • Habari
  • Majonzi
  • Michezo
  • News
  • News and Updates
  • Skendo
  • Sports and Games
Submit ExpressSEO Services & Tools

Total Pageviews

Copyright 2014 Mwanafalsafa
Template By Ridwan Hex And Game Gratis