Mwanafalsafa

  • HOME
Home → Entertainment → Kiungo mpya wa Azam, Amri Kiemba akiwa katika jezi ya timu hiyo kwenye Uwanja wa Chamazi, Dar es Salaam jana

Kiungo mpya wa Azam, Amri Kiemba akiwa katika jezi ya timu hiyo kwenye Uwanja wa Chamazi, Dar es Salaam jana

Entertainment
Tuesday, 25 November 2014


 

 Klabu ya Yanga imemleta nchini kwa majaribio mshambuliaji raia wa Zambia, Jonas Sakuwaha anayeichezea klabu ya TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
Sakuwaha (31), pia amewahi kucheza soka katika klabu ya Zesco United (Zambia), Lorient (Ufaransa), Le Havre (Ufaransa) na El-Merreikh (Sudan).
Kwa mujibu wa kiongozi mmoja wa Yanga, kama Sakuwaha atafuzu majaribio, basi atachukua nafasi ya Hamis Kiiza raia wa Uganda katika orodha ya wachezaji wake watano wa kigeni kwa mujibu wa kanuni za Shirikisho la Soka Tanzania (TFF).
Mbali na Kiiza, Haruna Niyonzima yuko hatarini kuiacha Yanga na tayari Azam FC imemkaribisha kundini ikijinasibu kuwa raia huyo wa Rwanda ni mchezaji wao.
Azam wamekuwa wakidai kuwa walikuwa wa kwanza kumsajili Niyonzima kabla ya kutua Yanga, lakini aliyekuwa kocha wao, Stewart Hall alimkataa kwa kigezo cha ufupi, ndipo walipomshauri ajiunge na Yanga.
Yanga tayari inao wachezaji watano wa kigeni ambao ni, Mbuyu Twite, Andrey Coutinho, Hamis Kiiza, Haruna Niyonzima na Mbrazili mpya, Emerson de Oliveira Neves Rouqe, anayetarajiwa kuwasili nchini kesho kuziba nafasi ya Mbrazili Genilson Santos ‘Jaja’.
Kuwasili kwa Sakuwaha aliyeichezea Zambia michuano mbalimbali ya kimataifa na pengine ujio wa Emerson ni mabadiliko yanayolenga kuimarisha mfumo wa uchezaji Yanga.
Hata hivyo, hilo litategemea kuondoka kwa Kiiza na Niyonzima, ambao wameonyesha nia ya kutotaka kubakia kwenye klabu hiyo.
Habari zilizolifikia gazeti hili jana zilieleza kuwa Sakuwaha atawasili nchini akifuatana na wachezaji wengine wanne kutoka Zambia kwa ajili ya majaribio.
Jana kulikuwa na habari kuwa mshambuliaji chipukizi wa Uganda, Yunus Sentamu anayeichezea AS Vita ya DRC, naye atatua Yanga.
Katika hatua nyingine, Emerson de Oliveira Neves Rouqe anatarajiwa kuwasili nchini kesho saa 7.00 mchana kwa ajili ya majaribio.

Share this article :
Tweet
✚
Newer Post
Older Post
Home

HABARI ZILIZO BAMBA TOP 10

  • The World leaders are arriving in Australia for this weekend's G20 summit in the Queensland city of Brisbane.
      The two-day summit, attended by the US, Chinese and Russian leaders among others, will focus on promoting growth. Australian Pri...
  • Ronaldo aosha vyombo baada ya kushindwa katika karata na mchezaji wa Tenisi Rafa Nadal
    Ali...
  • In long, dimly lit hallways, clusters of people wait anxiously outside courtrooms for their cases to come before a judge.
    The New York Immigration Court is an extraordinarily busy place. In long, dimly lit hallways, clusters of people wait anxiously outside co...
  • Chinese leader Xi Jinping has urged Asia-Pacific nations to accelerate economic integration to spur global growth, on day two of the Apec summit.
    The high-level meeting includes the leaders of the US, Russia, China, Japan and others He spoke as leaders from the 21-na...
  • John Doar, a civil rights lawyer who was a key figure in the struggle against racial segregation in the US, has died aged 92.
    John Doar was awarded the Presidential Medal of Freedom in 2012 Mr Doar dealt with some of the most prominent civil rights ca...
  • Ukweli kuhusu umoja wa fedha,Jumuiya ya Afrika Mashariki.
      OKTOBA 20 hadi 24 mwaka  huu, Benki Kuu ya Tanzania (BoT) iliandaa semi...
  • Kiungo mpya wa Azam, Amri Kiemba akiwa katika jezi ya timu hiyo kwenye Uwanja wa Chamazi, Dar es Salaam jana
       Klabu ya Yanga imemleta nchini kwa majaribio mshambuliaji raia wa Zambia, Jonas Sakuwaha ...
  • Rais wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa ametunukiwa Tuzo ya Mafanikio Katika Utumishi wa Umma kutokana na mchango alioutoa kwenye uchumi wakati wa utawala wake.
      Kwa ufupi Kufanya kazi bila kuchoka, kusisitiza uwazi na ukweli katika kuboresha uchumi katika kipindi chake kwampaisha....
  • Dies aged 87,singing legend, Sabah, Lebanese
      Sabah was nicknamed "Shahroura", Arabic for "singing bird" by her mil...
  • Tatizo la kuwapo bandari bubu linazidi kuongezeka.
    Rais Jakaya Kikwete.PICHA|MAKTABA   Jeshi la Polisi mkoani Tanga ju...

LABELS

  • Breaking News
  • condolonces
  • Entertainment
  • Entertainments
  • Habari
  • Majonzi
  • Michezo
  • News
  • News and Updates
  • Skendo
  • Sports and Games
Submit ExpressSEO Services & Tools

Total Pageviews

Copyright 2014 Mwanafalsafa
Template By Ridwan Hex And Game Gratis