Mwanafalsafa

  • HOME
Home → Entertainment → Kiungo mpya wa Azam, Amri Kiemba akiwa katika jezi ya timu hiyo kwenye Uwanja wa Chamazi, Dar es Salaam jana

Kiungo mpya wa Azam, Amri Kiemba akiwa katika jezi ya timu hiyo kwenye Uwanja wa Chamazi, Dar es Salaam jana

Entertainment
Tuesday, 25 November 2014


 

 Klabu ya Yanga imemleta nchini kwa majaribio mshambuliaji raia wa Zambia, Jonas Sakuwaha anayeichezea klabu ya TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
Sakuwaha (31), pia amewahi kucheza soka katika klabu ya Zesco United (Zambia), Lorient (Ufaransa), Le Havre (Ufaransa) na El-Merreikh (Sudan).
Kwa mujibu wa kiongozi mmoja wa Yanga, kama Sakuwaha atafuzu majaribio, basi atachukua nafasi ya Hamis Kiiza raia wa Uganda katika orodha ya wachezaji wake watano wa kigeni kwa mujibu wa kanuni za Shirikisho la Soka Tanzania (TFF).
Mbali na Kiiza, Haruna Niyonzima yuko hatarini kuiacha Yanga na tayari Azam FC imemkaribisha kundini ikijinasibu kuwa raia huyo wa Rwanda ni mchezaji wao.
Azam wamekuwa wakidai kuwa walikuwa wa kwanza kumsajili Niyonzima kabla ya kutua Yanga, lakini aliyekuwa kocha wao, Stewart Hall alimkataa kwa kigezo cha ufupi, ndipo walipomshauri ajiunge na Yanga.
Yanga tayari inao wachezaji watano wa kigeni ambao ni, Mbuyu Twite, Andrey Coutinho, Hamis Kiiza, Haruna Niyonzima na Mbrazili mpya, Emerson de Oliveira Neves Rouqe, anayetarajiwa kuwasili nchini kesho kuziba nafasi ya Mbrazili Genilson Santos ‘Jaja’.
Kuwasili kwa Sakuwaha aliyeichezea Zambia michuano mbalimbali ya kimataifa na pengine ujio wa Emerson ni mabadiliko yanayolenga kuimarisha mfumo wa uchezaji Yanga.
Hata hivyo, hilo litategemea kuondoka kwa Kiiza na Niyonzima, ambao wameonyesha nia ya kutotaka kubakia kwenye klabu hiyo.
Habari zilizolifikia gazeti hili jana zilieleza kuwa Sakuwaha atawasili nchini akifuatana na wachezaji wengine wanne kutoka Zambia kwa ajili ya majaribio.
Jana kulikuwa na habari kuwa mshambuliaji chipukizi wa Uganda, Yunus Sentamu anayeichezea AS Vita ya DRC, naye atatua Yanga.
Katika hatua nyingine, Emerson de Oliveira Neves Rouqe anatarajiwa kuwasili nchini kesho saa 7.00 mchana kwa ajili ya majaribio.

Share this article :
Tweet
✚
Newer Post
Older Post
Home

HABARI ZILIZO BAMBA TOP 10

  • Lorna Rutto is an entrepreneur who founded Ecopost, a Nairobi-based company that recycles plastic waste
    Lorna Rutto is an entrepreneur who founded Ecopost, a Nairobi-based company that recycles plastic waste. As part of the latest series o...
  • After more than two years of tension over a territorial row,the leaders of China and Japan hold formal talks on the sidelines of a major Asian summit.
    Chinese President Xi Jinping and Japanese PM Shinzo Abe met on the sidelines of the Asia-Pacific Economic Co-operation (Apec) summit in B...
  • The poorest president, Jose Mujica gets $1m offer for his VW Beetle
    7 November 2014 Last updated at 07:04 GMT Uruguay's President Jose Mujica says he has been offered $1m (£630,000) for his vinta...
  • Report says,Fossil fuel promises are being broken,World governments have been breaking promises to phase out subsidies for fossil fuels, a report says.
    The report said G20 nations had been spending almost $90bn a year on finding more oil, g...
  • Wabunge wa Somali wameng'oa waziri mkuu
    Ni mara ya nne kwamba kura ya kutokuwa na imani dhidi yake ilipigwa baada ya majaribio ya awali kumalizika kwa ghasia. Waandishi ...
  • AJIITA KIJANA MWENYE BAHATI AKIWA KATIKATI YA WAREMBO WAWILI
  • Burkina Faso leaders agree transitional framework following the meeting held in Ouagadougou
      The blueprint for transition was agreed unanimously at the meeting in Ouagadougou A framework for a transitional government ...
  • John Doar, a civil rights lawyer who was a key figure in the struggle against racial segregation in the US, has died aged 92.
    John Doar was awarded the Presidential Medal of Freedom in 2012 Mr Doar dealt with some of the most prominent civil rights ca...
  • Ukweli kuhusu umoja wa fedha,Jumuiya ya Afrika Mashariki.
      OKTOBA 20 hadi 24 mwaka  huu, Benki Kuu ya Tanzania (BoT) iliandaa semi...
  • BRAZIL TO EDGE OUT GERMANY IN WORLD CUP SEMI FINAL

LABELS

  • Breaking News
  • condolonces
  • Entertainment
  • Entertainments
  • Habari
  • Majonzi
  • Michezo
  • News
  • News and Updates
  • Skendo
  • Sports and Games
Submit ExpressSEO Services & Tools

Total Pageviews

Copyright 2014 Mwanafalsafa
Template By Ridwan Hex And Game Gratis