Mwanafalsafa

  • HOME
Home → Habari → Radi yamuua mzee wa miaka 80 jijini Mbeya

Radi yamuua mzee wa miaka 80 jijini Mbeya

Habari
Friday, 5 December 2014
MKAZI wa kitongoji cha Ngena, wilayani hapa, Watsoni Mwakiposa (80) amefariki dunia baada ya kupigwa na radi akielekea kwenye kilabu cha pombe.
Akizungumza na waandishi wa habari jana, Ofisa Mtendaji wa Kijiji hicho, William Ndille, alisema mzee huyo alikutwa na umauti jana majira ya saa 1:00 usiku wakati akielekea katika kilabu cha pombe za kienyeji.
Akielezea tukio hilo, Ndille alisema mzee huyo alikuwa na mauti akiwa njiani kuelekea katika kilabu cha pombe ambapo kulikuwa na mvua iliyoambatana na radi.
Ndille alisema baada ya tukio hilo waliliarifu Jeshi la Polisi wilayani humo ambao walifika eneo hilo na kuupeleka mwili wa mzee huyo katika hospitali ya Wilaya ya Rungwe kwa uchunguzi zaidi.
Alisema kwa kuwa tukio hilo ni la pili, aliwataka wakazi wa kijiji hicho kupunguza miti iliyozidi katika eneo hilo ili kuepusha madhara.


Share this article :
Tweet
✚
Newer Post
Older Post
Home

HABARI ZILIZO BAMBA TOP 10

  • MAREKANI YAITUPIA LAWAMA KOREA KASKAZINI
    Marekani inatarajia kuirudisha Korea kaskazini katika orodha ya nchi zinazofadhili ugaidi. Rais Barack Obama wa Marekani amesema utawala ...
  • MKUU wa Wilaya ya Mufindi mkoani Iringa, Evarista Kalalu, awashauri wananchi kujiunga na mfuko wa afya ya jamii
    MKUU wa Wilaya ya Mufindi mkoani Iringa, Evarista Kalalu, amewashauri wananchi wa vijiji vya Ukami na Chogo Kata ya Mapanda wilayani hapa...
  • KAULI YA UHURU KWENYE MTANDAOWA KIJAMII (TWITTER) KENYATTA HII HAPA
    Taarifa ya mahakama ya ICC, kutupilia mbali kesi dhidi ya Uhuru Kenyatta, imepokelwa na watu wengi nchini Kenya kwa hisia mseto. Baadhi w...
  • HAYA NDIO MAZITO ALIYO FUNGUKA YULE MSICHANA WA KAZI ALIYE MPIGA MTOTO
    Baada ya story ya yule msichana kwa anayefanya kazi za ndani Uganda kuchukua headlines katika vyombo mbalimbali vya Kimataifa Dun...
  • Ronaldo aosha vyombo baada ya kushindwa katika karata na mchezaji wa Tenisi Rafa Nadal
    Ali...
  • Wayne Goss, former premier of Queensland, kicked the bucket at 63
    Mr Goss, who was premier from 1989 to 1996, had suffered from ill health in recent years including brain tumours. He became Q...
  • IT 'S MATTER OF FEW MINUTES FOR WORLD CUP 2014 START SHINNING !!!!
    The World Cup  The 2014  Brazil™ is now just a matter of minutes away and to mark the occasion FIFA have launched an updated version of th...

LABELS

  • Breaking News
  • condolonces
  • Entertainment
  • Entertainments
  • Habari
  • Majonzi
  • Michezo
  • News
  • News and Updates
  • Skendo
  • Sports and Games
Submit ExpressSEO Services & Tools

Total Pageviews

Copyright 2014 Mwanafalsafa
Template By Ridwan Hex And Game Gratis