Mwanafalsafa

  • HOME
Home → Habari → MKURUGENZI wa Ulinzi na Usalama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Wilfred Lwakatare, Aiburuza serikali mahakamani.

MKURUGENZI wa Ulinzi na Usalama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Wilfred Lwakatare, Aiburuza serikali mahakamani.

Habari
Friday, 5 December 2014


ameshinda rufaa ya maombi ya marejeo yaliyowasilishwa na Serikali kupinga uamuzi wa Mahakama Kuu ya Tanzania kumfutia mashitaka ya ugaidi.
Lwakatare, alipata ushindi huo jijini Dar es Salaam jana katika Mahakama ya Rufaa ya Tanzania, baada ya kutupilia mbali maombi ya Jamhuri ambayo yalilenga kupinga uamuzi uliotolewa na Jaji Lawrence Kaduri Mei 8, 2013.
Lwakatare alikuwa akitetewa na Mawakili Peter Kibatala akisaidiana na John Malya huku upande wa Jamhuri ukiwakilishwa na Faraja Nchimbi.
Akisoma uamuzi huo, Msajili wa Mahakama ya Rufaa, Zahara Maluma, alisema rufaa ya Jamhuri haikuambatanishwa na kumbukumbu za Mahakama Kuu katika uamuzi wa Jaji Kaduri, jambo ambalo ni kinyume cha sheria.
Alisema katika maelezo ya rufaa aliyoyasoma mbele ya Mawakili wa pande zote mbili, hakuna sehemu iliyoambatanishwa kumbukumbu ambazo zinaonyesha marejeo kuhusu uamuzi huo uliopita.Lwakatare aibwaga serikali kortini

Baada ya kutolewa uamuzi huo, Wakili Kibatala alisema kwamba, Mahakama hiyo inapaswa kupongezwa kutokana na kutenda haki bila ya kuangalia upande wowote.
“Naamini kama maamuzi yatakuwa hivi katika kesi zote, tutazidi kuimarisha imani ya mawakili kutokana na hukumu zinazotolewa katika kesi mbalimbali,”alisema.
Kufutwa kwa shauri hilo, kunatokana na ombi lililowahi kuwasilishwa na Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP), Dk. Eliezer Feleshi wakati huo, kuiomba mahakama hiyo itengue uamuzi wa Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam wa kumfutia mashitaka matatu ya ugaidi Lwakatare.

Share this article :
Tweet
✚
Newer Post
Older Post
Home

HABARI ZILIZO BAMBA TOP 10

  • Takribani watu 15 wapata upofu baada ya upasuaji nchini India
    Wagonjwa waliofanyiwa upasuaji walisema walishindwa kuona tena baada ya kuondoa bandeji kwenye macho yao Maafisa wa utawala nchini Indiaa w...
  • Familia ya mateka yasihi Al Qaeda kumwachilia
    Marekani imeeleza kuwa ilijaribu kumwokoa raia wake mzaliwa wa Uingereza Luke Somers, anayeshikiliwa mateka na al-Qaeda nchini Yemen. ...
  • Ona kilichotokea kwa jimama hili kipindi lina jaribu kucheza jirani na swimming pool.Noii huko Kenya mida ya jana jioni
       
  • AJIITA KIJANA MWENYE BAHATI AKIWA KATIKATI YA WAREMBO WAWILI
  • BRAZIL TO EDGE OUT GERMANY IN WORLD CUP SEMI FINAL
  • KAULI YA UHURU KWENYE MTANDAOWA KIJAMII (TWITTER) KENYATTA HII HAPA
    Taarifa ya mahakama ya ICC, kutupilia mbali kesi dhidi ya Uhuru Kenyatta, imepokelwa na watu wengi nchini Kenya kwa hisia mseto. Baadhi w...
  • Maandano zidi ya kutupiliwa mbali kwa kesi ya afisa polisi mjini New York
    Maandamano mjini New York Waandamanaji wameingia katika barabara za miji mingi Nchini Marekani kwa usiku wa pili mtawalia, kupinga maamu...
  • Jennifer Lawrence has joined her castmates at the world premiere of the penultimate Hunger Games movie, Mockingjay Part 1, in London.
    Lawrence plays the heroine Katniss Everdeen in the hit franchise Jennifer Lawrence has joined her castmates at the w...
  • MORE THAN 10,000 GRADUATES TURN UP FOR SEVENTY JOB VACANCIES IN DAR ES SLAAM.
    According to the list of names seen by The Guardian yesterday morning, the department listed 10,816 candidates to perform the interview tha...
  • Mshindi wa Nishani ya Nobel bint Malala amenukuliwa akisema "Nataka kuwa Waziri mkuu''
    Mshindi wa Nishani ya Nobel bint Malala Yousafzai raia wa Pakistani amesema kuwa siku zijazo anatarajia kuwa mwanasiasa. Malala a...

LABELS

  • Breaking News
  • condolonces
  • Entertainment
  • Entertainments
  • Habari
  • Majonzi
  • Michezo
  • News
  • News and Updates
  • Skendo
  • Sports and Games
Submit ExpressSEO Services & Tools

Total Pageviews

Copyright 2014 Mwanafalsafa
Template By Ridwan Hex And Game Gratis