Mwanafalsafa

  • HOME
Home → Habari → MKURUGENZI wa Ulinzi na Usalama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Wilfred Lwakatare, Aiburuza serikali mahakamani.

MKURUGENZI wa Ulinzi na Usalama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Wilfred Lwakatare, Aiburuza serikali mahakamani.

Habari
Friday, 5 December 2014


ameshinda rufaa ya maombi ya marejeo yaliyowasilishwa na Serikali kupinga uamuzi wa Mahakama Kuu ya Tanzania kumfutia mashitaka ya ugaidi.
Lwakatare, alipata ushindi huo jijini Dar es Salaam jana katika Mahakama ya Rufaa ya Tanzania, baada ya kutupilia mbali maombi ya Jamhuri ambayo yalilenga kupinga uamuzi uliotolewa na Jaji Lawrence Kaduri Mei 8, 2013.
Lwakatare alikuwa akitetewa na Mawakili Peter Kibatala akisaidiana na John Malya huku upande wa Jamhuri ukiwakilishwa na Faraja Nchimbi.
Akisoma uamuzi huo, Msajili wa Mahakama ya Rufaa, Zahara Maluma, alisema rufaa ya Jamhuri haikuambatanishwa na kumbukumbu za Mahakama Kuu katika uamuzi wa Jaji Kaduri, jambo ambalo ni kinyume cha sheria.
Alisema katika maelezo ya rufaa aliyoyasoma mbele ya Mawakili wa pande zote mbili, hakuna sehemu iliyoambatanishwa kumbukumbu ambazo zinaonyesha marejeo kuhusu uamuzi huo uliopita.Lwakatare aibwaga serikali kortini

Baada ya kutolewa uamuzi huo, Wakili Kibatala alisema kwamba, Mahakama hiyo inapaswa kupongezwa kutokana na kutenda haki bila ya kuangalia upande wowote.
“Naamini kama maamuzi yatakuwa hivi katika kesi zote, tutazidi kuimarisha imani ya mawakili kutokana na hukumu zinazotolewa katika kesi mbalimbali,”alisema.
Kufutwa kwa shauri hilo, kunatokana na ombi lililowahi kuwasilishwa na Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP), Dk. Eliezer Feleshi wakati huo, kuiomba mahakama hiyo itengue uamuzi wa Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam wa kumfutia mashitaka matatu ya ugaidi Lwakatare.

Share this article :
Tweet
✚
Newer Post
Older Post
Home

HABARI ZILIZO BAMBA TOP 10

  • MAREKANI YAITUPIA LAWAMA KOREA KASKAZINI
    Marekani inatarajia kuirudisha Korea kaskazini katika orodha ya nchi zinazofadhili ugaidi. Rais Barack Obama wa Marekani amesema utawala ...
  • MKUU wa Wilaya ya Mufindi mkoani Iringa, Evarista Kalalu, awashauri wananchi kujiunga na mfuko wa afya ya jamii
    MKUU wa Wilaya ya Mufindi mkoani Iringa, Evarista Kalalu, amewashauri wananchi wa vijiji vya Ukami na Chogo Kata ya Mapanda wilayani hapa...
  • KAULI YA UHURU KWENYE MTANDAOWA KIJAMII (TWITTER) KENYATTA HII HAPA
    Taarifa ya mahakama ya ICC, kutupilia mbali kesi dhidi ya Uhuru Kenyatta, imepokelwa na watu wengi nchini Kenya kwa hisia mseto. Baadhi w...
  • HAYA NDIO MAZITO ALIYO FUNGUKA YULE MSICHANA WA KAZI ALIYE MPIGA MTOTO
    Baada ya story ya yule msichana kwa anayefanya kazi za ndani Uganda kuchukua headlines katika vyombo mbalimbali vya Kimataifa Dun...
  • Ronaldo aosha vyombo baada ya kushindwa katika karata na mchezaji wa Tenisi Rafa Nadal
    Ali...
  • Wayne Goss, former premier of Queensland, kicked the bucket at 63
    Mr Goss, who was premier from 1989 to 1996, had suffered from ill health in recent years including brain tumours. He became Q...
  • IT 'S MATTER OF FEW MINUTES FOR WORLD CUP 2014 START SHINNING !!!!
    The World Cup  The 2014  Brazil™ is now just a matter of minutes away and to mark the occasion FIFA have launched an updated version of th...

LABELS

  • Breaking News
  • condolonces
  • Entertainment
  • Entertainments
  • Habari
  • Majonzi
  • Michezo
  • News
  • News and Updates
  • Skendo
  • Sports and Games
Submit ExpressSEO Services & Tools

Total Pageviews

Copyright 2014 Mwanafalsafa
Template By Ridwan Hex And Game Gratis