Mwanafalsafa

  • HOME
Home → Tanpa Kategori → MKE WA MTU ANASWA AKIJIUZA KUSAKA FEDHA ZA SIKUKUU

MKE WA MTU ANASWA AKIJIUZA KUSAKA FEDHA ZA SIKUKUU

Monday, 22 December 2014
Tabia ya wanawake kujiuza kwa kisingizio cha kusaka fedha kwa ajili ya Sikukuu ya Krismasi imewatokea puani wanawake zaidi ya kumi akiwemo mke wa mtu baada ya kunaswa mawindoni na kutiwa nguvuni.
Makamanda wa Polisi pamoja na kikosi cha OFM wakiwataiti wanawke waliokuwa wakijiuza.
Tukio hilo la aibu lilitokea katika msako maalum wa polisi waliotoa kolabo kwa Oparesheni Fichua Maovu (OFM) ya Global Publishers, uliofanyika katika eneo ‘korofi’ la ltinga, Msamvu Kata ya Mwembesongo mkoani hapa, wikiendi iliyopita.
Wanawake hao wakiwa chini ya ulinzi mkali.
Awali, Kamanda wa OFM mkoani hapa alipokea malalamiko lukuki kutoka kwa wananchi waishio jirani na eneo hilo waliokuwa wakiwalalamikia wanawake hao kugeuza vibanda vyao vya simu kuwa gesti na kuvitumia kufanyia ngono usiku na kuzagaa kwa kondom kila sehemu.
Mke wa mtu (wa kwanza kushoto) akijificha kwa aibu.
Kabla ya msako, OFM iliwashauri kupeleka malalamiko hayo kwenye serikali ya mtaa na polisi.
Kabla ya kufanya oparesheni hiyo, shushushu wetu alifanya upelelezi na kubaini kwamba ni kweli wanawake hao huvitumia vibanda hivyo kama gesti.
Baada ya kujiridhisha, OFM na jeshi la polisi walipofika eneo hilo majira ya saa 5:00 usiku na kuwanasa wanawake hao kisha kuwasukumiza kwenye difenda na kwenda kuwasweka lupango kusubiri sheria ichukue mkondo wake.
...Wakitupiwa kwenye difenda ili kuchukuliwa hatua za kisheria.
Katika hali ya kushangaza, mmoja wa wanawake hao alikuwa akiomba msamaha kwa madai kwamba ni mke wa mtu hivyo mumewe akijua ishu hiyo atamtoa roho.
“Jamani mimi ni mke wa mtu, mume wangu alivyo mkali akijua nimekutwa huko atanimaliza,” alisikika mwanamke huyo.

Share this article :
Tweet
✚
Newer Post
Older Post
Home

HABARI ZILIZO BAMBA TOP 10

  • The World leaders are arriving in Australia for this weekend's G20 summit in the Queensland city of Brisbane.
      The two-day summit, attended by the US, Chinese and Russian leaders among others, will focus on promoting growth. Australian Pri...
  • Ronaldo aosha vyombo baada ya kushindwa katika karata na mchezaji wa Tenisi Rafa Nadal
    Ali...
  • In long, dimly lit hallways, clusters of people wait anxiously outside courtrooms for their cases to come before a judge.
    The New York Immigration Court is an extraordinarily busy place. In long, dimly lit hallways, clusters of people wait anxiously outside co...
  • Chinese leader Xi Jinping has urged Asia-Pacific nations to accelerate economic integration to spur global growth, on day two of the Apec summit.
    The high-level meeting includes the leaders of the US, Russia, China, Japan and others He spoke as leaders from the 21-na...
  • John Doar, a civil rights lawyer who was a key figure in the struggle against racial segregation in the US, has died aged 92.
    John Doar was awarded the Presidential Medal of Freedom in 2012 Mr Doar dealt with some of the most prominent civil rights ca...
  • Ukweli kuhusu umoja wa fedha,Jumuiya ya Afrika Mashariki.
      OKTOBA 20 hadi 24 mwaka  huu, Benki Kuu ya Tanzania (BoT) iliandaa semi...
  • Kiungo mpya wa Azam, Amri Kiemba akiwa katika jezi ya timu hiyo kwenye Uwanja wa Chamazi, Dar es Salaam jana
       Klabu ya Yanga imemleta nchini kwa majaribio mshambuliaji raia wa Zambia, Jonas Sakuwaha ...
  • Rais wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa ametunukiwa Tuzo ya Mafanikio Katika Utumishi wa Umma kutokana na mchango alioutoa kwenye uchumi wakati wa utawala wake.
      Kwa ufupi Kufanya kazi bila kuchoka, kusisitiza uwazi na ukweli katika kuboresha uchumi katika kipindi chake kwampaisha....
  • Dies aged 87,singing legend, Sabah, Lebanese
      Sabah was nicknamed "Shahroura", Arabic for "singing bird" by her mil...
  • Tatizo la kuwapo bandari bubu linazidi kuongezeka.
    Rais Jakaya Kikwete.PICHA|MAKTABA   Jeshi la Polisi mkoani Tanga ju...

LABELS

  • Breaking News
  • condolonces
  • Entertainment
  • Entertainments
  • Habari
  • Majonzi
  • Michezo
  • News
  • News and Updates
  • Skendo
  • Sports and Games
Submit ExpressSEO Services & Tools

Total Pageviews

Copyright 2014 Mwanafalsafa
Template By Ridwan Hex And Game Gratis