Mwanafalsafa

  • HOME
Home → Habari → Hii ndiyo siri ya kufanikisha biashara yako

Hii ndiyo siri ya kufanikisha biashara yako

Habari
Thursday, 4 December 2014

Kama mwanzo wa makala ya hivi punde ya African Dream,mwanabiashara Mercy Kitomari-ambaye alianzisha kampuni ya kutengeza aiskrimu hai ya Nelwa's Gelato-anaeleza mbinu kumi bora anazotumia katika kuuza kwenye mitandao ya kijamii kwa wanabiashara chipukizi:
Anza na Lengo.
Kwanini uko kwenye mitandao ya kijamii? ana nadi
Kuna majibu matatu pekee yanayokubalika: a)kuongeza kujulikana kwa bidhaa zako kwa kufikia watu zaidi b)kujenga imani ya wateja kwa kuwapa usaidizi zaidi ama c)kuongeza mauzo kwa kutafuta wanunuzi zaidi,watakaonunua mara kwa kwa mara.Usianze kama huwezi jibu swali hili.
Wapuuze wapinzani wako-
Kujaribu kuiba wateja wa watu wengine ni mbinu mbovu.Utaanza kuunda maamuzi mabaya kwa sababu unajaribu kuwafikia.
Fikra na kampeni bora zaidi bado hazijatendeka katika sekta yako.Angalia nafasi ambazo hazijaguzwa unazoweza kupata na kutumia.Tazama kile watu wanafanya kwenye sekta tofauti na ujaribu mbinu hizo.
Usiwe kwenye mitandao yote ya kijamii.
Usimamizi wa kijamii utamaliza rasilmali zako zote.Kila mtandao wa kijamii unaosimamia utakugharimu muda,pesa na nguvu zaidi,kwa hivyo amua zile utazipa kipao mbele.
Una pesa na wakati wa kutosha.
Watu huwa wanasema kuwa hawana muda na pesa za kuwekeza katika mitandao ya kijamii.Lakini ukweli wa mambo ni kuwa hauwezi kutowekeza.Kama hauna fedha za kutosha,inafaa uwe na wakati zaidi wa kuunda maudhui ama kuunda mtandao.
Mercy Kitomari ana mkahawa wa Nelwa's Gelato mjini Dar es Salaam inayosambaza kwenye hoteli na biashara zingine.
Weka lengo rahisi-
Kwa mfano,kuchapisha mara mbili zaidi kila wiki-ama kufikia bloga mmoja kwa siku.Pia fanya ukaguzi wa ndani kujua jinsi unavyotumia muda wako kwa sasa.
Mitandao ya kijamii ni bora,lakini watu wengi huchanganya kushikika na kazi na kuwa na ufanisi.Tambua shughuli zinazoleta ''mapato kutoka kwa uwekezaji'' ya juu zaidi,zipe kipao mbele na uweke mipaka.
Kuwa na nidhamu na kuwajibika kwa wengine.
Mwishowe,utahitajika kuchukua msimamo mgumu.Utahitaji kugawanya rasilmali zako chache na kuchagua kile utakachofanya (na kile utakachopuuza).Lakini utaona kuwa uamuzi huu ni rahisi kama una lengo.Matumizi yako ya mitandao ya kijamii yatakuwa na kusudi.Utapata kuwa una wakati wa kutosha wa kuitumia kimkakati.
Tambua kile kinachohamasisha wasikilizaji wako.
''Sekta'' ama ''biashara'' hazichoshi-watu wanaosema hayo ndio wanaochosha.Jinsi unavyojenga mawazo ya maudhui ya blogi ni kuelewa wasikilizaji wako na faida ambazo bidhaa na huduma zako zinawapa.
Mercy Kitomari anasema kuwa huduma ya wateja ni muhimu sana kwenye mitandao sawia na ya uso kwa uso.

Kuwa na sauti.
Watu hawapendi kuungana na mashirika yasiyokuwa na uso.Wanataka kuungana na wanadamu wa kweli.Hakuna atakayiependa,amini ama kuheshimu kampuni yako ikiwa hawezi kupata majibu yaliyo sawa na yenye uaminifu kwa wakati ufaao.Mitandao ya kijamii ni zaidi ya ''kujiingiza katika mazungumzo''.Ni njia mpya ya kufanya mambo,na vifaa kadhaa vipya kukusaidia kufanya hivo.
Lakini misingi ya njia za mauzo inabakia.Unahitaji kuvutia watu,kujenga imani yao na kuwawezesha kushiriki zaidi.
Tamba sana kupia Facebook na Twitter.
Mitandao ya kijamii na mauzo kwenye mtandao inaanza na DNA yako,bidhaa ama huduma zako,na watu wako.Kwa hivyo kama unataka kuimarisha majibu yako kwenye mitandao ya kijamii,anda na kushughulikia utenda kazi wa ndani wa kampuni yako.

Share this article :
Tweet
✚
Newer Post
Older Post
Home

HABARI ZILIZO BAMBA TOP 10

  • Lorna Rutto is an entrepreneur who founded Ecopost, a Nairobi-based company that recycles plastic waste
    Lorna Rutto is an entrepreneur who founded Ecopost, a Nairobi-based company that recycles plastic waste. As part of the latest series o...
  • Jennifer Lawrence has joined her castmates at the world premiere of the penultimate Hunger Games movie, Mockingjay Part 1, in London.
    Lawrence plays the heroine Katniss Everdeen in the hit franchise Jennifer Lawrence has joined her castmates at the w...
  • Catalonia's regional president Artur Mas says an official referendum is needed following Catalonia vote: 80% back independence - officials
    \ An informal vote on independence for Catalonia has shown more than 80% in favour, officials say. The non-binding vote went ahead after ...
  • After more than two years of tension over a territorial row,the leaders of China and Japan hold formal talks on the sidelines of a major Asian summit.
    Chinese President Xi Jinping and Japanese PM Shinzo Abe met on the sidelines of the Asia-Pacific Economic Co-operation (Apec) summit in B...
  • MAREKANI YAITUPIA LAWAMA KOREA KASKAZINI
    Marekani inatarajia kuirudisha Korea kaskazini katika orodha ya nchi zinazofadhili ugaidi. Rais Barack Obama wa Marekani amesema utawala ...
  • The poorest president, Jose Mujica gets $1m offer for his VW Beetle
    7 November 2014 Last updated at 07:04 GMT Uruguay's President Jose Mujica says he has been offered $1m (£630,000) for his vinta...
  • Report says,Fossil fuel promises are being broken,World governments have been breaking promises to phase out subsidies for fossil fuels, a report says.
    The report said G20 nations had been spending almost $90bn a year on finding more oil, g...
  • Wabunge wa Somali wameng'oa waziri mkuu
    Ni mara ya nne kwamba kura ya kutokuwa na imani dhidi yake ilipigwa baada ya majaribio ya awali kumalizika kwa ghasia. Waandishi ...
  • AJIITA KIJANA MWENYE BAHATI AKIWA KATIKATI YA WAREMBO WAWILI
  • Burkina Faso leaders agree transitional framework following the meeting held in Ouagadougou
      The blueprint for transition was agreed unanimously at the meeting in Ouagadougou A framework for a transitional government ...

LABELS

  • Breaking News
  • condolonces
  • Entertainment
  • Entertainments
  • Habari
  • Majonzi
  • Michezo
  • News
  • News and Updates
  • Skendo
  • Sports and Games
Submit ExpressSEO Services & Tools

Total Pageviews

Copyright 2014 Mwanafalsafa
Template By Ridwan Hex And Game Gratis