Mwanafalsafa

  • HOME
Home → Tanpa Kategori → KAMPUNI YA USAMBAZAJI WA FILAMU NCHINI-(STEPS ENTERTAINMENT) YASHUSHA BEI ZA FILAMU ZA KIBONGO.

KAMPUNI YA USAMBAZAJI WA FILAMU NCHINI-(STEPS ENTERTAINMENT) YASHUSHA BEI ZA FILAMU ZA KIBONGO.

Saturday, 20 December 2014
Wasanii wa filamu pamoja na kampuni ya usambazaji wa filamu nchini ‘Steps Entertainment’ wameamua kushusha bei ya filamu hadi kufikia shilingi 1,500 kwa nakala moja ili kujaribu kupambana na waharamia wa kazi za wasanii.



Muigizaji Salma Jabu aka Nisha ambaye hufanya kazi na kampuni hiyo ameiambia Bongo5 kuwa imewabidi wafanye hivyo ili kuwawezesha watanzania wote kuwa na uwezo wa kupata kopi halisi za kuacha kununua feki.

“Kweli tumekaa na Steps, tunaona njia pekee ya kupambana na waharamia wa kazi zetu ni kupunguza bei ya filamu zetu,” amesema Nisha. “Kuanzia mwezi February 2015, filamu zitaanza kuuzwa kwa bei ya shilingi 1,500 za kitanzania badala ya 3,000 kama bei ya rejereja. Kwahiyo kama utakuwa unahitaji mbili ina maana utatoa shilingi 3,000. Tumeshuka ili kumshawishi mtanzania kuacha kununuA filamu za mitaani kwa bei ya 1,000, ni bora tupunguze hii filamu yetu orijino iliyokuwa inauzwa 3,000 tupunguze mpaka 1,500 ili aweze kuinunua,” ameongeza.

“Kwahiyo kama alikuwa anahitaji mbili, anatoa shilingi 3,000 badala ya 6,000 ambayo ilikuwa bei ya mwanzo. Kwahiyo sisi kama wasanii tumeona bora tuuze kwa bei hiyo tukiwa tuna imani tutauza filamu nyingi na tutakuwa tunapata faida.”



Pia Nisha amewataka watanzania kumuunga mkono kwa kununua filamu yake mpya, ‘Hakuna Matata’ inayotarajiwa kutoka December 22 mwaka huu.

Share this article :
Tweet
✚
Newer Post
Older Post
Home

HABARI ZILIZO BAMBA TOP 10

  • Lorna Rutto is an entrepreneur who founded Ecopost, a Nairobi-based company that recycles plastic waste
    Lorna Rutto is an entrepreneur who founded Ecopost, a Nairobi-based company that recycles plastic waste. As part of the latest series o...
  • Wabunge wa Somali wameng'oa waziri mkuu
    Ni mara ya nne kwamba kura ya kutokuwa na imani dhidi yake ilipigwa baada ya majaribio ya awali kumalizika kwa ghasia. Waandishi ...
  • AJIITA KIJANA MWENYE BAHATI AKIWA KATIKATI YA WAREMBO WAWILI
  • Ukweli kuhusu umoja wa fedha,Jumuiya ya Afrika Mashariki.
      OKTOBA 20 hadi 24 mwaka  huu, Benki Kuu ya Tanzania (BoT) iliandaa semi...
  • BRAZIL TO EDGE OUT GERMANY IN WORLD CUP SEMI FINAL
  • Chuo kikuu cha ardhi ARU chatoa zawadi kwa wanafunzi 30, mmoja, ambae ni muhitimu wa masomo ya surveying aibuka na machine ya millioni 35
    CHUO Kikuu Ardhi (ARU), kimewazawadia wanafuzi 130 wa masomo mbalimbali zawadi zenye thamani ya zaidi ya sh milioni 60 kutokana n...
  • Ajali ya gari huko south B kenya
    There was a bizarre accident today morning in Hazina Estate, South B involving a Range Rover that crashed into 7 vehicles. The Ran...
  • Jennifer Lawrence has joined her castmates at the world premiere of the penultimate Hunger Games movie, Mockingjay Part 1, in London.
    Lawrence plays the heroine Katniss Everdeen in the hit franchise Jennifer Lawrence has joined her castmates at the w...
  • Arsenal yamlenga Kramer anaechezea klabu ya Borussia Monchengladbach
    Arsenal wako tayari kutoa p...
  • Catalonia's regional president Artur Mas says an official referendum is needed following Catalonia vote: 80% back independence - officials
    \ An informal vote on independence for Catalonia has shown more than 80% in favour, officials say. The non-binding vote went ahead after ...

LABELS

  • Breaking News
  • condolonces
  • Entertainment
  • Entertainments
  • Habari
  • Majonzi
  • Michezo
  • News
  • News and Updates
  • Skendo
  • Sports and Games
Submit ExpressSEO Services & Tools

Total Pageviews

Copyright 2014 Mwanafalsafa
Template By Ridwan Hex And Game Gratis