Mwanafalsafa

  • HOME
Home → Habari → Majonzi → HILI NDILO BALAA LA MAFURIKO YALIYOTOKEA HUKO MWANZA

HILI NDILO BALAA LA MAFURIKO YALIYOTOKEA HUKO MWANZA

Habari, Majonzi
Friday, 5 December 2014

Kivuko asilia ni ajira kwa wengine.

Wanajeshi wa Kikosi cha zimamoto Mwanza wakimvusha mama huyu kutoka juu ya paa la nyumba moja hadi upande wa pili penye usalama kupisha maji yaliyokuwa yamefurika hata kuzifunika nyumba za wananchi eneo la Mabatini jijini Mwanza. 

MVUA kubwa iliyonyeesha juzi (jumanne) asubuhi imeleta mafuriko katika maeneo mbalimbali Jijini Mwanza  huku eneo la mabatini likiathirika zaidi na mafuriko hayo yaliyoambatana na mvua kubwa iliyonyeesha takribani  kwa muda usipoungua  masaa mawili.

Mafuriko hayo yalisababisha maji kujaa katika nyumba za wakazi wa maeneo ya mabatini,pia mafuriko hayo yalisababisha magari kutopita eneo la daraja la mabatini linalotumiwa na waenda kwa miguu baada ya maji hayo ya mafuriko kuigawa barabara ya mabatini hali iliyosababisha kukatika kwa mawasiliano.

Juhudi za jeshi la Zimamoto na uokoaji ambao walifika mapema eneo la tukio zilisaidia kuokoa baadhi ya wakazi wa nyumba zilizokumbwa na mafuriko yaliyosababisha nyumba hizo kujaa maji ndani.
Katika zoezi hilo la uokoaji watu mbalimbali waliokolewa wakiwepo watoto wadogo na akina mama huku mali mbalimbali zikiwemo runinga,vitanda,magari yakisombwa na mafuriko hayo.
Akizungumzia tathimini ya zoezi nzima la uokoaji Kamanda wa Jeshi la zimamoto na uokoaji Jijini Mwanza,Andrew James Mbate amesema zoezi la uokoaji lilienda vizuri na walifanikiwa kuokoa maisha ya watu waliokowepo ndani ya nyumba huku akitanabaisha changamoto mbalimbali walizokutana nazo katika zoezi zima. 
“Zoezi la uokoaji lilienda limeenda salama na linaendelea vizuri tunashukuru wenzetu wa shirika la umeme waliwahi kukata umeme mapema hali iliyopelekea sisi kama Jeshi kuanza kazi mara moja tulivyofika eneo la tukio”. Aliongeza Gadafi ambaye ni msemaji wa jeshi la Zimamoto

Akizungumza juu ya mafuriko hayo mkazi wa mabatini,Charles Samson alisema wamepoteza vitu vyao vya thamani huku wakioomba serikali iwasaidie kuhama mabondeni kwani madhara yaliyowakuta ni makubwa.

Tanesco walizima umeme kwaajili ya tahadhali.




Gari hili nyang'anyang'a mara baada ya kusombwa na mafuriko na kubinuliwa kisha kutoswa mtaroni. 
Msaada tutani.
Eneo la mabatini ni eneo ambalo mto mirongo unapita hali iliyosababisha mafuriko hayo kuwa makubwa kwa kuwa maji yam to huo yanatoka sehemu mbalimbali za wilaya zilizopo Mkoani Mwanza ikiwemo wilaya ya magu.

Share this article :
Tweet
✚
Newer Post
Older Post
Home

HABARI ZILIZO BAMBA TOP 10

  • MAREKANI YAITUPIA LAWAMA KOREA KASKAZINI
    Marekani inatarajia kuirudisha Korea kaskazini katika orodha ya nchi zinazofadhili ugaidi. Rais Barack Obama wa Marekani amesema utawala ...
  • MKUU wa Wilaya ya Mufindi mkoani Iringa, Evarista Kalalu, awashauri wananchi kujiunga na mfuko wa afya ya jamii
    MKUU wa Wilaya ya Mufindi mkoani Iringa, Evarista Kalalu, amewashauri wananchi wa vijiji vya Ukami na Chogo Kata ya Mapanda wilayani hapa...
  • KAULI YA UHURU KWENYE MTANDAOWA KIJAMII (TWITTER) KENYATTA HII HAPA
    Taarifa ya mahakama ya ICC, kutupilia mbali kesi dhidi ya Uhuru Kenyatta, imepokelwa na watu wengi nchini Kenya kwa hisia mseto. Baadhi w...
  • HAYA NDIO MAZITO ALIYO FUNGUKA YULE MSICHANA WA KAZI ALIYE MPIGA MTOTO
    Baada ya story ya yule msichana kwa anayefanya kazi za ndani Uganda kuchukua headlines katika vyombo mbalimbali vya Kimataifa Dun...
  • Ronaldo aosha vyombo baada ya kushindwa katika karata na mchezaji wa Tenisi Rafa Nadal
    Ali...
  • Wayne Goss, former premier of Queensland, kicked the bucket at 63
    Mr Goss, who was premier from 1989 to 1996, had suffered from ill health in recent years including brain tumours. He became Q...
  • IT 'S MATTER OF FEW MINUTES FOR WORLD CUP 2014 START SHINNING !!!!
    The World Cup  The 2014  Brazil™ is now just a matter of minutes away and to mark the occasion FIFA have launched an updated version of th...

LABELS

  • Breaking News
  • condolonces
  • Entertainment
  • Entertainments
  • Habari
  • Majonzi
  • Michezo
  • News
  • News and Updates
  • Skendo
  • Sports and Games
Submit ExpressSEO Services & Tools

Total Pageviews

Copyright 2014 Mwanafalsafa
Template By Ridwan Hex And Game Gratis