Mwanafalsafa

  • HOME
Home → Habari → Majonzi → HILI NDILO BALAA LA MAFURIKO YALIYOTOKEA HUKO MWANZA

HILI NDILO BALAA LA MAFURIKO YALIYOTOKEA HUKO MWANZA

Habari, Majonzi
Friday, 5 December 2014

Kivuko asilia ni ajira kwa wengine.

Wanajeshi wa Kikosi cha zimamoto Mwanza wakimvusha mama huyu kutoka juu ya paa la nyumba moja hadi upande wa pili penye usalama kupisha maji yaliyokuwa yamefurika hata kuzifunika nyumba za wananchi eneo la Mabatini jijini Mwanza. 

MVUA kubwa iliyonyeesha juzi (jumanne) asubuhi imeleta mafuriko katika maeneo mbalimbali Jijini Mwanza  huku eneo la mabatini likiathirika zaidi na mafuriko hayo yaliyoambatana na mvua kubwa iliyonyeesha takribani  kwa muda usipoungua  masaa mawili.

Mafuriko hayo yalisababisha maji kujaa katika nyumba za wakazi wa maeneo ya mabatini,pia mafuriko hayo yalisababisha magari kutopita eneo la daraja la mabatini linalotumiwa na waenda kwa miguu baada ya maji hayo ya mafuriko kuigawa barabara ya mabatini hali iliyosababisha kukatika kwa mawasiliano.

Juhudi za jeshi la Zimamoto na uokoaji ambao walifika mapema eneo la tukio zilisaidia kuokoa baadhi ya wakazi wa nyumba zilizokumbwa na mafuriko yaliyosababisha nyumba hizo kujaa maji ndani.
Katika zoezi hilo la uokoaji watu mbalimbali waliokolewa wakiwepo watoto wadogo na akina mama huku mali mbalimbali zikiwemo runinga,vitanda,magari yakisombwa na mafuriko hayo.
Akizungumzia tathimini ya zoezi nzima la uokoaji Kamanda wa Jeshi la zimamoto na uokoaji Jijini Mwanza,Andrew James Mbate amesema zoezi la uokoaji lilienda vizuri na walifanikiwa kuokoa maisha ya watu waliokowepo ndani ya nyumba huku akitanabaisha changamoto mbalimbali walizokutana nazo katika zoezi zima. 
“Zoezi la uokoaji lilienda limeenda salama na linaendelea vizuri tunashukuru wenzetu wa shirika la umeme waliwahi kukata umeme mapema hali iliyopelekea sisi kama Jeshi kuanza kazi mara moja tulivyofika eneo la tukio”. Aliongeza Gadafi ambaye ni msemaji wa jeshi la Zimamoto

Akizungumza juu ya mafuriko hayo mkazi wa mabatini,Charles Samson alisema wamepoteza vitu vyao vya thamani huku wakioomba serikali iwasaidie kuhama mabondeni kwani madhara yaliyowakuta ni makubwa.

Tanesco walizima umeme kwaajili ya tahadhali.




Gari hili nyang'anyang'a mara baada ya kusombwa na mafuriko na kubinuliwa kisha kutoswa mtaroni. 
Msaada tutani.
Eneo la mabatini ni eneo ambalo mto mirongo unapita hali iliyosababisha mafuriko hayo kuwa makubwa kwa kuwa maji yam to huo yanatoka sehemu mbalimbali za wilaya zilizopo Mkoani Mwanza ikiwemo wilaya ya magu.

Share this article :
Tweet
✚
Newer Post
Older Post
Home

HABARI ZILIZO BAMBA TOP 10

  • MAREKANI YAITUPIA LAWAMA KOREA KASKAZINI
    Marekani inatarajia kuirudisha Korea kaskazini katika orodha ya nchi zinazofadhili ugaidi. Rais Barack Obama wa Marekani amesema utawala ...
  • Mamboya whatsapp haya hapa.!!!!! (18+)
  • SIMBA Vs EXPRESS YA UGANDA ,0-0 LEO UWANJA WA TAIFA
    Katongole Henry akimtoka mshambulia wa Simba, Ramadhani Singano 'Mess'. Kipa wa The Express, Mutumba Ivan akir...
  • AKOTHEE Takes Her Beautiful Daughters TO FLY OVER ! look at these beautiful photos.
  • APIGWA MVUA YA MIAKA 60 JELA, KWA KUTOROSHA TWIGA
    HATIMAYE Mahakama ya hakimu mkazi Moshi, mkoani Kilimanjaro, imemhukumu miaka 60 jela, Kamran Ahmed, raia wa Pakistani kwa kosa la kutoro...
  • TEKNOLOGIA:GARI LINALOWEZA KUPAKI LENYEWE KWA KUTUMIA SAA YA SMARTPHONE BILA KUWA NA DEREVA NDANI..
    Kampuni ya BMW imezindua kifaa ambacho kinawezesha gari lako kujiegesha lenyewe.. Hakuna kitu kibaya kama kusahau ulikoegesha gari lako ka...
  • Spotify's chief executive has defended its business model, saying it has paid out $2bn (£1.2bn) to the music industry to date.
      Daniel Ek pitches Spotify as a more lucrative alternative to piracy Daniel Ek's lengthy blog post follows a high profil...
  • Mombasa based singer akothee gets naughty,Angalia hapa
  • ,Juncker reveals giant EU investment planJuncker said Europe needed a kick-start and the Commission was offering the jump-leads
    Mr  European Commission President Jean-Claude Juncker has given details of a €315bn (£250bn;$393bn) investment plan to kic...
  • HILI NDILO BALAA LA MAFURIKO YALIYOTOKEA HUKO MWANZA
    Kivuko asilia ni ajira kwa wengine. Wanajeshi wa Kikosi cha zimamoto Mwanza wakimvusha mama huyu kutoka juu ya paa la nyumba moja had...

LABELS

  • Breaking News
  • condolonces
  • Entertainment
  • Entertainments
  • Habari
  • Majonzi
  • Michezo
  • News
  • News and Updates
  • Skendo
  • Sports and Games
Submit ExpressSEO Services & Tools

Total Pageviews

Copyright 2014 Mwanafalsafa
Template By Ridwan Hex And Game Gratis