Mwanafalsafa

  • HOME
Home → Habari → Wanafunzi wafundishwe ujasiriamali mapema

Wanafunzi wafundishwe ujasiriamali mapema

Habari
Tuesday, 25 November 2014


Kuna kaulimbiu za shule mbalimbali ambazo zimekuwa zikionekana katika nyaraka za shule.
Kwa mfano, unaweza utakutana na misemo kama “Elimu ni Maisha,” “Elimu ni Ufunguo wa Maisha” na nyingine nyingi.
Lengo la misemo hii ni kuonyesha jinsi taasisi husika inavyowaandaa watu wake kwa ajili ya maisha yao ya baadaye.
Kwa maana hiyo waandaliwa hao wanatakiwa wawe wakala wazuri wa shule zao uko waendako kwa kufanana na kaulimbiu hizo.
Pamoja na kwamba taasisi hizo huwa na malengo mazuri, suala la utekelezaji wa malengo hayo huwa ni changamoto.
Nasema ni changamoto kwa sababu tunaona jinsi idadi kubwa ya wahitimu wanaotoka katika taasisi wasivyohusiana na kaulimbiu za taasisi zao.
Funzo tunalolipata hapa ni kuwa hatuna budi kusimamia na kutekeleza kwa vitendo kauli mbiu tunazoziamini.
Utekelezaji wake kwa vitendo utazaa matunda yaliyokusudiwa. Katika elimu ya ujasiriamali, matendo ndicho kitu cha thamani kubwa kuliko maneno yatokayo katika mdomo wa mtu.
Wataalamu wa elimu ya ujasiriamali kama vile Garavan na Barra wanasema kuwa madhumuni ye elimu ya ujasiriamali ni pamoja na kupata maarifa stahiki ya ujasiriamali.
Pia, ni kupata ujuzi utakaosaidia kutumia mbinu mbalimbali za uchambuzi wa masuala ya biashara. Vilevile ni kubainisha na kuchochea ujasiriamali.
Madhumuni mengine ni kujenga na kuendeleza mambo yanayowagusa wajasiriamali ikiwa ni pamoja na kusaidia masuala yote yanayohusiana na ujasiriamali.
Kama haya yakifanyika katika viwango vyetu vya elimu itakuwa rahisi kwa Taifa letu kuwa na maendeleo endelevu. Tutakuwa tumejenga watu wenye maarifa na ujuzi wa kufanya kazi kwa manufaa yao na taifa lao

Share this article :
Tweet
✚
Newer Post
Older Post
Home

HABARI ZILIZO BAMBA TOP 10

  • MAREKANI YAITUPIA LAWAMA KOREA KASKAZINI
    Marekani inatarajia kuirudisha Korea kaskazini katika orodha ya nchi zinazofadhili ugaidi. Rais Barack Obama wa Marekani amesema utawala ...
  • MKUU wa Wilaya ya Mufindi mkoani Iringa, Evarista Kalalu, awashauri wananchi kujiunga na mfuko wa afya ya jamii
    MKUU wa Wilaya ya Mufindi mkoani Iringa, Evarista Kalalu, amewashauri wananchi wa vijiji vya Ukami na Chogo Kata ya Mapanda wilayani hapa...
  • KAULI YA UHURU KWENYE MTANDAOWA KIJAMII (TWITTER) KENYATTA HII HAPA
    Taarifa ya mahakama ya ICC, kutupilia mbali kesi dhidi ya Uhuru Kenyatta, imepokelwa na watu wengi nchini Kenya kwa hisia mseto. Baadhi w...
  • HAYA NDIO MAZITO ALIYO FUNGUKA YULE MSICHANA WA KAZI ALIYE MPIGA MTOTO
    Baada ya story ya yule msichana kwa anayefanya kazi za ndani Uganda kuchukua headlines katika vyombo mbalimbali vya Kimataifa Dun...
  • Ronaldo aosha vyombo baada ya kushindwa katika karata na mchezaji wa Tenisi Rafa Nadal
    Ali...
  • Wayne Goss, former premier of Queensland, kicked the bucket at 63
    Mr Goss, who was premier from 1989 to 1996, had suffered from ill health in recent years including brain tumours. He became Q...
  • IT 'S MATTER OF FEW MINUTES FOR WORLD CUP 2014 START SHINNING !!!!
    The World Cup  The 2014  Brazil™ is now just a matter of minutes away and to mark the occasion FIFA have launched an updated version of th...

LABELS

  • Breaking News
  • condolonces
  • Entertainment
  • Entertainments
  • Habari
  • Majonzi
  • Michezo
  • News
  • News and Updates
  • Skendo
  • Sports and Games
Submit ExpressSEO Services & Tools

Total Pageviews

Copyright 2014 Mwanafalsafa
Template By Ridwan Hex And Game Gratis