Mwanafalsafa

  • HOME
Home → Habari → Wanafunzi wafundishwe ujasiriamali mapema

Wanafunzi wafundishwe ujasiriamali mapema

Habari
Tuesday, 25 November 2014


Kuna kaulimbiu za shule mbalimbali ambazo zimekuwa zikionekana katika nyaraka za shule.
Kwa mfano, unaweza utakutana na misemo kama “Elimu ni Maisha,” “Elimu ni Ufunguo wa Maisha” na nyingine nyingi.
Lengo la misemo hii ni kuonyesha jinsi taasisi husika inavyowaandaa watu wake kwa ajili ya maisha yao ya baadaye.
Kwa maana hiyo waandaliwa hao wanatakiwa wawe wakala wazuri wa shule zao uko waendako kwa kufanana na kaulimbiu hizo.
Pamoja na kwamba taasisi hizo huwa na malengo mazuri, suala la utekelezaji wa malengo hayo huwa ni changamoto.
Nasema ni changamoto kwa sababu tunaona jinsi idadi kubwa ya wahitimu wanaotoka katika taasisi wasivyohusiana na kaulimbiu za taasisi zao.
Funzo tunalolipata hapa ni kuwa hatuna budi kusimamia na kutekeleza kwa vitendo kauli mbiu tunazoziamini.
Utekelezaji wake kwa vitendo utazaa matunda yaliyokusudiwa. Katika elimu ya ujasiriamali, matendo ndicho kitu cha thamani kubwa kuliko maneno yatokayo katika mdomo wa mtu.
Wataalamu wa elimu ya ujasiriamali kama vile Garavan na Barra wanasema kuwa madhumuni ye elimu ya ujasiriamali ni pamoja na kupata maarifa stahiki ya ujasiriamali.
Pia, ni kupata ujuzi utakaosaidia kutumia mbinu mbalimbali za uchambuzi wa masuala ya biashara. Vilevile ni kubainisha na kuchochea ujasiriamali.
Madhumuni mengine ni kujenga na kuendeleza mambo yanayowagusa wajasiriamali ikiwa ni pamoja na kusaidia masuala yote yanayohusiana na ujasiriamali.
Kama haya yakifanyika katika viwango vyetu vya elimu itakuwa rahisi kwa Taifa letu kuwa na maendeleo endelevu. Tutakuwa tumejenga watu wenye maarifa na ujuzi wa kufanya kazi kwa manufaa yao na taifa lao

Share this article :
Tweet
✚
Newer Post
Older Post
Home

HABARI ZILIZO BAMBA TOP 10

  • MAREKANI YAITUPIA LAWAMA KOREA KASKAZINI
    Marekani inatarajia kuirudisha Korea kaskazini katika orodha ya nchi zinazofadhili ugaidi. Rais Barack Obama wa Marekani amesema utawala ...
  • Mombasa based singer akothee gets naughty,Angalia hapa
  • Vita dhidi ya Ukimwi zashika kasi, mbinu madhubuti zachukuliwa !
    DESEMBA mosi, kila mwaka, watu wote duniani huadhimisha Siku ya Ukimwi Duniani. Siku hiyo ilianzishwa mwaka 1987 na hubeba maudhui mbalim...
  • ,Juncker reveals giant EU investment planJuncker said Europe needed a kick-start and the Commission was offering the jump-leads
    Mr  European Commission President Jean-Claude Juncker has given details of a €315bn (£250bn;$393bn) investment plan to kic...
  • Kwaninii serikali imewekeza katika siasa na imesahau wakulima ?
      Hata hivyo, wakulima wamekwazwa na kodi nyingi wanazotozwa kwa kila gunia inapotokea wakauza sehemu ya ...
  • Mdogo wa Zari Hassan apaka matope uhusiano wake na Diamond
    Mdogo wake na Zari Hassan aka The Bosslady, aitwaye Karim ametumia Facebook kumkosoa dada yake kwa kuwa na uhusiano na Diamond Platnumz amb...
  • DAVIDO,TIWA SWAGE,DIAMOND, MR.FLAVOUR ON THE SHOOT,CHECK THE NEW VIDEO HERE
    Africa MultiChoice has launched it’s biggest  campaign yet, to celebrate Africa’s positivity , successes and the ability to  te...
  • Wayne Goss, former premier of Queensland, kicked the bucket at 63
    Mr Goss, who was premier from 1989 to 1996, had suffered from ill health in recent years including brain tumours. He became Q...
  • Third death confirmed in Mali The Pasteur Clinic in Bamako has been placed in quarantine and is under armed guard
      A nurse and the patient he was treating have become the second and third people to die from Ebola in Mali. The patient,...
  • The poorest president, Jose Mujica gets $1m offer for his VW Beetle
    7 November 2014 Last updated at 07:04 GMT Uruguay's President Jose Mujica says he has been offered $1m (£630,000) for his vinta...

LABELS

  • Breaking News
  • condolonces
  • Entertainment
  • Entertainments
  • Habari
  • Majonzi
  • Michezo
  • News
  • News and Updates
  • Skendo
  • Sports and Games
Submit ExpressSEO Services & Tools

Total Pageviews

Copyright 2014 Mwanafalsafa
Template By Ridwan Hex And Game Gratis