Mwanafalsafa

  • HOME
Home → News and Updates → Rais wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa ametunukiwa Tuzo ya Mafanikio Katika Utumishi wa Umma kutokana na mchango alioutoa kwenye uchumi wakati wa utawala wake.

Rais wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa ametunukiwa Tuzo ya Mafanikio Katika Utumishi wa Umma kutokana na mchango alioutoa kwenye uchumi wakati wa utawala wake.

News and Updates
Tuesday, 25 November 2014


 
Kwa ufupi
Kufanya kazi bila kuchoka, kusisitiza uwazi na ukweli katika kuboresha uchumi katika kipindi chake kwampaisha.

Dar es Salaam. 
Akikabidhi tuzo hiyo iliyotolewa na Umoja wa Watendaji Wakuu (CEOrt) juzi, Balozi Ami Mbungwe alisema Rais Mkapa ametoa mchango mkubwa katika kuimarisha utawala bora na uwazi ndani na nje ya nchi.
“Alifanya kazi bila kuchoka, akisisitiza ukweli na uwazi wakati wa kipindi cha kuboresho sera za uchumi. Atakumbukwa kwa mchango wake mkubwa kwenye masuala ya uwekezaji,” alisema.
Akipokea tuzo hiyo katika hafla iliyohudhuriwa na viongozi mbalimbali, Mkapa alisema ameipokea kwa niaba ya wananchi ambao walikubali kupokea mabadiliko ya kiuchumi.
“Maono na mipango yangu wakati ule ilikuwa kuweka mazingira rafiki ambayo yangelinda haki za sekta binafsi, kuhakikisha mfumo wa fedha unakuwa rafiki kwa biashara, kukusanya mapato na kulipa madeni ya umma ili kufan uchumi uwe imara,” alisema.
Mkapa alisema hata alipogundua kuwa ujasiriamali unabanwa na kanuni zisizo sahihi, kodi kubwa, kukosekana kwa ushindani halali, alihakikisha anaondoa vikwazo na kuongeza ushindani wa kibiashara.
Alisema baadhi ya watu walilalamikia uboreshaji kwa madai kuwa sekta binafsi iligeuka sehemu ya kuficha kampuni za kigeni.
Mwenyekiti wa CEOrt, Ali Mufuruki alisema tuzo hiyo mwaka jana ilitolewa kwa Rais wa Serikali ya Awamu ya Pili, Ali Hassan Mwinyi, kutokana na mchango wake kwenye biashara huria, vyombo vya habari na kuanzisha siasa za vyama vingi.
Mufuruki alisema nishani hiyo haitolewi tu kwa viongozi wa kitaifa au marais, bali inakwenda kwa mtu yeyote ambaye mchango wake unatambuliwa na jamii.
Alisema kiongozi huyo aliingia madarakani wakati nchini ikiwa katika hali mbaya kiuchumi, lakini katika miaka miwili aliteremsha mfumko wa bei kutoka asilimia 30 mpaka nne.
“Aliweza kusimamisha kuporomoka kwa thamani ya shilingi, alihakikisha Serikali inatumia fedha ambayo inakusanya kutokana na mapato yake ya ndani. alisema Mufuruki.
Katika hafla hiyo, Mtendaji Mkuu kutoka Ofisi ya Rais-Ufuatiliaji wa Utekelezaji wa Miradi (PDB), Omari Issa alipewa tuzo ya Mwaka ya Utumishi wa Serikali kutokana na mchango wake alioutoa kwenye sekta binafsi nchini.

Share this article :
Tweet
✚
Newer Post
Older Post
Home

HABARI ZILIZO BAMBA TOP 10

  • Umuhimu wa kushirikiana katika kazi hasa ya muziki
  • Wiki hii katika mtandao wa kijamii, whatsapp , Ni sheedah cheki picha kali hapa chini !
  • Mwanasheria mkuu wa serikali nchini Mexico, Jesus Murillo Karam,ametoa ahadi kuwa hakutakuwa na uonevu wowote katika kesi ya kupotea kwa wanafunzi nchi humo miezi miwili iliyopita
    . Kutoweka kwa wanafunzi hao kumesababisha maandamano ya wiki kadhaa nchini humo waandamanaji wakipinda rushwa na ukatili...
  • Ni majonzi makubwa Tazama picha za wana familia za wachimba machimbo ya kokoto waliouawa na Al Shabaab mjini Mandera
    Familia za wachimba machimbo ya kokoto waliouawa na Al Shabaab mjini Mandera leo waliwapokea wapendwa wao baada ya miili yao kufikishwa ch...
  • After more than two years of tension over a territorial row,the leaders of China and Japan hold formal talks on the sidelines of a major Asian summit.
    Chinese President Xi Jinping and Japanese PM Shinzo Abe met on the sidelines of the Asia-Pacific Economic Co-operation (Apec) summit in B...
  • CCM KUTOICHUKULIA HATUA AKAUNTI YA ESCROW
    Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye, alisema kuwa CCM haina mpango wa kuchukua hatua zozote dhidi ya wote waliotajwa kuh...
  • A hardline cleric in Pakistan is teaching the ideas of Osama Bin Laden in religious schools for about 5,000 children.
       Even while the Pakistani government fights the Taliban in the north-west of the country, it has no plans to clos...
  • Lorna Rutto is an entrepreneur who founded Ecopost, a Nairobi-based company that recycles plastic waste
    Lorna Rutto is an entrepreneur who founded Ecopost, a Nairobi-based company that recycles plastic waste. As part of the latest series o...
  • AJIITA KIJANA MWENYE BAHATI AKIWA KATIKATI YA WAREMBO WAWILI
  • HIVI NDIVYO Gangnam Walivyovunja rekodi huko YouTube
    Jump media player Media player help Out of media player. Press enter to return or tab to continue. Na Kim Kardashian a...

LABELS

  • Breaking News
  • condolonces
  • Entertainment
  • Entertainments
  • Habari
  • Majonzi
  • Michezo
  • News
  • News and Updates
  • Skendo
  • Sports and Games
Submit ExpressSEO Services & Tools

Total Pageviews

Copyright 2014 Mwanafalsafa
Template By Ridwan Hex And Game Gratis