Mwanafalsafa

  • HOME
Home → News and Updates → Rais wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa ametunukiwa Tuzo ya Mafanikio Katika Utumishi wa Umma kutokana na mchango alioutoa kwenye uchumi wakati wa utawala wake.

Rais wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa ametunukiwa Tuzo ya Mafanikio Katika Utumishi wa Umma kutokana na mchango alioutoa kwenye uchumi wakati wa utawala wake.

News and Updates
Tuesday, 25 November 2014


 
Kwa ufupi
Kufanya kazi bila kuchoka, kusisitiza uwazi na ukweli katika kuboresha uchumi katika kipindi chake kwampaisha.

Dar es Salaam. 
Akikabidhi tuzo hiyo iliyotolewa na Umoja wa Watendaji Wakuu (CEOrt) juzi, Balozi Ami Mbungwe alisema Rais Mkapa ametoa mchango mkubwa katika kuimarisha utawala bora na uwazi ndani na nje ya nchi.
“Alifanya kazi bila kuchoka, akisisitiza ukweli na uwazi wakati wa kipindi cha kuboresho sera za uchumi. Atakumbukwa kwa mchango wake mkubwa kwenye masuala ya uwekezaji,” alisema.
Akipokea tuzo hiyo katika hafla iliyohudhuriwa na viongozi mbalimbali, Mkapa alisema ameipokea kwa niaba ya wananchi ambao walikubali kupokea mabadiliko ya kiuchumi.
“Maono na mipango yangu wakati ule ilikuwa kuweka mazingira rafiki ambayo yangelinda haki za sekta binafsi, kuhakikisha mfumo wa fedha unakuwa rafiki kwa biashara, kukusanya mapato na kulipa madeni ya umma ili kufan uchumi uwe imara,” alisema.
Mkapa alisema hata alipogundua kuwa ujasiriamali unabanwa na kanuni zisizo sahihi, kodi kubwa, kukosekana kwa ushindani halali, alihakikisha anaondoa vikwazo na kuongeza ushindani wa kibiashara.
Alisema baadhi ya watu walilalamikia uboreshaji kwa madai kuwa sekta binafsi iligeuka sehemu ya kuficha kampuni za kigeni.
Mwenyekiti wa CEOrt, Ali Mufuruki alisema tuzo hiyo mwaka jana ilitolewa kwa Rais wa Serikali ya Awamu ya Pili, Ali Hassan Mwinyi, kutokana na mchango wake kwenye biashara huria, vyombo vya habari na kuanzisha siasa za vyama vingi.
Mufuruki alisema nishani hiyo haitolewi tu kwa viongozi wa kitaifa au marais, bali inakwenda kwa mtu yeyote ambaye mchango wake unatambuliwa na jamii.
Alisema kiongozi huyo aliingia madarakani wakati nchini ikiwa katika hali mbaya kiuchumi, lakini katika miaka miwili aliteremsha mfumko wa bei kutoka asilimia 30 mpaka nne.
“Aliweza kusimamisha kuporomoka kwa thamani ya shilingi, alihakikisha Serikali inatumia fedha ambayo inakusanya kutokana na mapato yake ya ndani. alisema Mufuruki.
Katika hafla hiyo, Mtendaji Mkuu kutoka Ofisi ya Rais-Ufuatiliaji wa Utekelezaji wa Miradi (PDB), Omari Issa alipewa tuzo ya Mwaka ya Utumishi wa Serikali kutokana na mchango wake alioutoa kwenye sekta binafsi nchini.

Share this article :
Tweet
✚
Newer Post
Older Post
Home

HABARI ZILIZO BAMBA TOP 10

  • MAREKANI YAITUPIA LAWAMA KOREA KASKAZINI
    Marekani inatarajia kuirudisha Korea kaskazini katika orodha ya nchi zinazofadhili ugaidi. Rais Barack Obama wa Marekani amesema utawala ...
  • MKUU wa Wilaya ya Mufindi mkoani Iringa, Evarista Kalalu, awashauri wananchi kujiunga na mfuko wa afya ya jamii
    MKUU wa Wilaya ya Mufindi mkoani Iringa, Evarista Kalalu, amewashauri wananchi wa vijiji vya Ukami na Chogo Kata ya Mapanda wilayani hapa...
  • KAULI YA UHURU KWENYE MTANDAOWA KIJAMII (TWITTER) KENYATTA HII HAPA
    Taarifa ya mahakama ya ICC, kutupilia mbali kesi dhidi ya Uhuru Kenyatta, imepokelwa na watu wengi nchini Kenya kwa hisia mseto. Baadhi w...
  • HAYA NDIO MAZITO ALIYO FUNGUKA YULE MSICHANA WA KAZI ALIYE MPIGA MTOTO
    Baada ya story ya yule msichana kwa anayefanya kazi za ndani Uganda kuchukua headlines katika vyombo mbalimbali vya Kimataifa Dun...
  • Ronaldo aosha vyombo baada ya kushindwa katika karata na mchezaji wa Tenisi Rafa Nadal
    Ali...
  • Wayne Goss, former premier of Queensland, kicked the bucket at 63
    Mr Goss, who was premier from 1989 to 1996, had suffered from ill health in recent years including brain tumours. He became Q...
  • IT 'S MATTER OF FEW MINUTES FOR WORLD CUP 2014 START SHINNING !!!!
    The World Cup  The 2014  Brazil™ is now just a matter of minutes away and to mark the occasion FIFA have launched an updated version of th...

LABELS

  • Breaking News
  • condolonces
  • Entertainment
  • Entertainments
  • Habari
  • Majonzi
  • Michezo
  • News
  • News and Updates
  • Skendo
  • Sports and Games
Submit ExpressSEO Services & Tools

Total Pageviews

Copyright 2014 Mwanafalsafa
Template By Ridwan Hex And Game Gratis