Mwanafalsafa

  • HOME
Home → News and Updates → Rais wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa ametunukiwa Tuzo ya Mafanikio Katika Utumishi wa Umma kutokana na mchango alioutoa kwenye uchumi wakati wa utawala wake.

Rais wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa ametunukiwa Tuzo ya Mafanikio Katika Utumishi wa Umma kutokana na mchango alioutoa kwenye uchumi wakati wa utawala wake.

News and Updates
Tuesday, 25 November 2014


 
Kwa ufupi
Kufanya kazi bila kuchoka, kusisitiza uwazi na ukweli katika kuboresha uchumi katika kipindi chake kwampaisha.

Dar es Salaam. 
Akikabidhi tuzo hiyo iliyotolewa na Umoja wa Watendaji Wakuu (CEOrt) juzi, Balozi Ami Mbungwe alisema Rais Mkapa ametoa mchango mkubwa katika kuimarisha utawala bora na uwazi ndani na nje ya nchi.
“Alifanya kazi bila kuchoka, akisisitiza ukweli na uwazi wakati wa kipindi cha kuboresho sera za uchumi. Atakumbukwa kwa mchango wake mkubwa kwenye masuala ya uwekezaji,” alisema.
Akipokea tuzo hiyo katika hafla iliyohudhuriwa na viongozi mbalimbali, Mkapa alisema ameipokea kwa niaba ya wananchi ambao walikubali kupokea mabadiliko ya kiuchumi.
“Maono na mipango yangu wakati ule ilikuwa kuweka mazingira rafiki ambayo yangelinda haki za sekta binafsi, kuhakikisha mfumo wa fedha unakuwa rafiki kwa biashara, kukusanya mapato na kulipa madeni ya umma ili kufan uchumi uwe imara,” alisema.
Mkapa alisema hata alipogundua kuwa ujasiriamali unabanwa na kanuni zisizo sahihi, kodi kubwa, kukosekana kwa ushindani halali, alihakikisha anaondoa vikwazo na kuongeza ushindani wa kibiashara.
Alisema baadhi ya watu walilalamikia uboreshaji kwa madai kuwa sekta binafsi iligeuka sehemu ya kuficha kampuni za kigeni.
Mwenyekiti wa CEOrt, Ali Mufuruki alisema tuzo hiyo mwaka jana ilitolewa kwa Rais wa Serikali ya Awamu ya Pili, Ali Hassan Mwinyi, kutokana na mchango wake kwenye biashara huria, vyombo vya habari na kuanzisha siasa za vyama vingi.
Mufuruki alisema nishani hiyo haitolewi tu kwa viongozi wa kitaifa au marais, bali inakwenda kwa mtu yeyote ambaye mchango wake unatambuliwa na jamii.
Alisema kiongozi huyo aliingia madarakani wakati nchini ikiwa katika hali mbaya kiuchumi, lakini katika miaka miwili aliteremsha mfumko wa bei kutoka asilimia 30 mpaka nne.
“Aliweza kusimamisha kuporomoka kwa thamani ya shilingi, alihakikisha Serikali inatumia fedha ambayo inakusanya kutokana na mapato yake ya ndani. alisema Mufuruki.
Katika hafla hiyo, Mtendaji Mkuu kutoka Ofisi ya Rais-Ufuatiliaji wa Utekelezaji wa Miradi (PDB), Omari Issa alipewa tuzo ya Mwaka ya Utumishi wa Serikali kutokana na mchango wake alioutoa kwenye sekta binafsi nchini.

Share this article :
Tweet
✚
Newer Post
Older Post
Home

HABARI ZILIZO BAMBA TOP 10

  • MAREKANI YAITUPIA LAWAMA KOREA KASKAZINI
    Marekani inatarajia kuirudisha Korea kaskazini katika orodha ya nchi zinazofadhili ugaidi. Rais Barack Obama wa Marekani amesema utawala ...
  • Mombasa based singer akothee gets naughty,Angalia hapa
  • Vita dhidi ya Ukimwi zashika kasi, mbinu madhubuti zachukuliwa !
    DESEMBA mosi, kila mwaka, watu wote duniani huadhimisha Siku ya Ukimwi Duniani. Siku hiyo ilianzishwa mwaka 1987 na hubeba maudhui mbalim...
  • ,Juncker reveals giant EU investment planJuncker said Europe needed a kick-start and the Commission was offering the jump-leads
    Mr  European Commission President Jean-Claude Juncker has given details of a €315bn (£250bn;$393bn) investment plan to kic...
  • Kwaninii serikali imewekeza katika siasa na imesahau wakulima ?
      Hata hivyo, wakulima wamekwazwa na kodi nyingi wanazotozwa kwa kila gunia inapotokea wakauza sehemu ya ...
  • Mdogo wa Zari Hassan apaka matope uhusiano wake na Diamond
    Mdogo wake na Zari Hassan aka The Bosslady, aitwaye Karim ametumia Facebook kumkosoa dada yake kwa kuwa na uhusiano na Diamond Platnumz amb...
  • DAVIDO,TIWA SWAGE,DIAMOND, MR.FLAVOUR ON THE SHOOT,CHECK THE NEW VIDEO HERE
    Africa MultiChoice has launched it’s biggest  campaign yet, to celebrate Africa’s positivity , successes and the ability to  te...
  • Wayne Goss, former premier of Queensland, kicked the bucket at 63
    Mr Goss, who was premier from 1989 to 1996, had suffered from ill health in recent years including brain tumours. He became Q...
  • Third death confirmed in Mali The Pasteur Clinic in Bamako has been placed in quarantine and is under armed guard
      A nurse and the patient he was treating have become the second and third people to die from Ebola in Mali. The patient,...
  • The poorest president, Jose Mujica gets $1m offer for his VW Beetle
    7 November 2014 Last updated at 07:04 GMT Uruguay's President Jose Mujica says he has been offered $1m (£630,000) for his vinta...

LABELS

  • Breaking News
  • condolonces
  • Entertainment
  • Entertainments
  • Habari
  • Majonzi
  • Michezo
  • News
  • News and Updates
  • Skendo
  • Sports and Games
Submit ExpressSEO Services & Tools

Total Pageviews

Copyright 2014 Mwanafalsafa
Template By Ridwan Hex And Game Gratis