Mwanafalsafa

  • HOME
Home → Michezo → Mbeya City Yashauriwa kuchukua uamuzi mgumu

Mbeya City Yashauriwa kuchukua uamuzi mgumu

Michezo
Wednesday, 26 November 2014
Joseph Kapinga 


Inawezekana kabisa Mwambusi amebeba msalaba ambao wengi waliutarajia. Kikosi chake kililewa sifa baada ya kufanya vizuri msimu uliopita kiasi cha kushika nafasi ya tatu ligi ilipomalizika.


Watafiti wa maisha ya binadamu na tabia zake, wanaamini kuwa kila mmoja utafika wakati atakutana na jambo litakalomlazimu kufanya au kutoa uamuzi mgumu.
Bila kujali jambo gani, lini na aina ya uamuzi anaoweza kuutoa, lakini ukweli unabaki palepale kwamba ipo siku lazima binadamu ataingia kwenye hali hiyo.
Katika maisha ya sasa yaliyojaa kila aina ya changamoto, chuki, visasi, migogoro na mabadiliko yenye ulazima ili kwenda sambamba na mahitaji ya maisha, yanawalazimu watu kufanya mambo ambayo hawatarajii.
Hata hivyo, kuna tofauti. Wapo ambao kutoa kwao uamuzi mgumu hutokana na shinikizo, hoja na mitazamo kutoka nje, wengine hufanya hivyo bila kusubiri misukumo ya nje bali ni kutokana na msuto wa dhamira kutoka ndani ya moyo.
Hongera kwa aliyekuwa kocha wa Mbeya City, Juma Mwambusi kwa kuchukua hatua ya kufanya uamuzi mgumu wa kuachana na timu hiyo bila shinikizo. Ni kama nilivyosema awali, Mwambusi amekutana na wakati ambao umemlazimu kufanya uamuzi mgumu ili kulinda heshima yake. Hakuna anayependa kuharibu ajira yake, lakini una sababu gani ya kusubiri kama mambo yameshaharibika?
Alichofanya Mwambusi ni ujasiri mkubwa kwa sababu, baadhi yetu wakati mwingine, iwe kwa kulewa madaraka au kwa lengo la kujishibisha, tunashindwa kutoa uamuzi mgumu hadi tulazimishwe.
Inawezekana kabisa Mwambusi amebeba msalaba ambao wengi waliutarajia. Kikosi chake kililewa sifa baada ya kufanya vizuri msimu uliopita kiasi cha kushika nafasi ya tatu ligi ilipomalizika.
Ilishangaza kwa timu ngeni, isiyo na wachezaji wenye majina na kocha wa ‘kawaida’ kupata matokeo mazuri kuizidi hata klabu kongwe ya Simba iliyojaza nyota kibao wa ndani na nje.
Kilichoiponza City ni kulewa mafanikio ya msimu uliopita na kudhani kuwa, wanaweza kufanya hivyo kirahisi msimu uliofuata. Walikosea!
Walidhani ligi ni peke yao, kwamba timu zingine zilizofanya vibaya msimu ambao wao walifanya vizuri, basi zingebaki kwenye nafasi hiyo ya kufanya vibaya. Walijidanganya!
Kila mmoja, kwa maana ya mashabiki wa soka Mbeya walikuwa wakisifu mafanikio ya timu hiyo, lakini, ni kwa kiasi gani walikuwa bega kwa bega kuisaidia kufanya vizuri msimu huu?
Sasa Mwambusi amefanya uamuzi mgumu, amejiuzulu. Ameiacha timu kwenye wakati mgumu.

Share this article :
Tweet
✚
Newer Post
Older Post
Home

HABARI ZILIZO BAMBA TOP 10

  • Lorna Rutto is an entrepreneur who founded Ecopost, a Nairobi-based company that recycles plastic waste
    Lorna Rutto is an entrepreneur who founded Ecopost, a Nairobi-based company that recycles plastic waste. As part of the latest series o...
  • Ajali ya gari huko south B kenya
    There was a bizarre accident today morning in Hazina Estate, South B involving a Range Rover that crashed into 7 vehicles. The Ran...
  • Jennifer Lawrence has joined her castmates at the world premiere of the penultimate Hunger Games movie, Mockingjay Part 1, in London.
    Lawrence plays the heroine Katniss Everdeen in the hit franchise Jennifer Lawrence has joined her castmates at the w...
  • Catalonia's regional president Artur Mas says an official referendum is needed following Catalonia vote: 80% back independence - officials
    \ An informal vote on independence for Catalonia has shown more than 80% in favour, officials say. The non-binding vote went ahead after ...
  • After more than two years of tension over a territorial row,the leaders of China and Japan hold formal talks on the sidelines of a major Asian summit.
    Chinese President Xi Jinping and Japanese PM Shinzo Abe met on the sidelines of the Asia-Pacific Economic Co-operation (Apec) summit in B...
  • MAREKANI YAITUPIA LAWAMA KOREA KASKAZINI
    Marekani inatarajia kuirudisha Korea kaskazini katika orodha ya nchi zinazofadhili ugaidi. Rais Barack Obama wa Marekani amesema utawala ...
  • The poorest president, Jose Mujica gets $1m offer for his VW Beetle
    7 November 2014 Last updated at 07:04 GMT Uruguay's President Jose Mujica says he has been offered $1m (£630,000) for his vinta...
  • Report says,Fossil fuel promises are being broken,World governments have been breaking promises to phase out subsidies for fossil fuels, a report says.
    The report said G20 nations had been spending almost $90bn a year on finding more oil, g...
  • Wabunge wa Somali wameng'oa waziri mkuu
    Ni mara ya nne kwamba kura ya kutokuwa na imani dhidi yake ilipigwa baada ya majaribio ya awali kumalizika kwa ghasia. Waandishi ...
  • AJIITA KIJANA MWENYE BAHATI AKIWA KATIKATI YA WAREMBO WAWILI

LABELS

  • Breaking News
  • condolonces
  • Entertainment
  • Entertainments
  • Habari
  • Majonzi
  • Michezo
  • News
  • News and Updates
  • Skendo
  • Sports and Games
Submit ExpressSEO Services & Tools

Total Pageviews

Copyright 2014 Mwanafalsafa
Template By Ridwan Hex And Game Gratis