Mwanafalsafa

  • HOME
Home → Michezo → Mbeya City Yashauriwa kuchukua uamuzi mgumu

Mbeya City Yashauriwa kuchukua uamuzi mgumu

Michezo
Wednesday, 26 November 2014
Joseph Kapinga 


Inawezekana kabisa Mwambusi amebeba msalaba ambao wengi waliutarajia. Kikosi chake kililewa sifa baada ya kufanya vizuri msimu uliopita kiasi cha kushika nafasi ya tatu ligi ilipomalizika.


Watafiti wa maisha ya binadamu na tabia zake, wanaamini kuwa kila mmoja utafika wakati atakutana na jambo litakalomlazimu kufanya au kutoa uamuzi mgumu.
Bila kujali jambo gani, lini na aina ya uamuzi anaoweza kuutoa, lakini ukweli unabaki palepale kwamba ipo siku lazima binadamu ataingia kwenye hali hiyo.
Katika maisha ya sasa yaliyojaa kila aina ya changamoto, chuki, visasi, migogoro na mabadiliko yenye ulazima ili kwenda sambamba na mahitaji ya maisha, yanawalazimu watu kufanya mambo ambayo hawatarajii.
Hata hivyo, kuna tofauti. Wapo ambao kutoa kwao uamuzi mgumu hutokana na shinikizo, hoja na mitazamo kutoka nje, wengine hufanya hivyo bila kusubiri misukumo ya nje bali ni kutokana na msuto wa dhamira kutoka ndani ya moyo.
Hongera kwa aliyekuwa kocha wa Mbeya City, Juma Mwambusi kwa kuchukua hatua ya kufanya uamuzi mgumu wa kuachana na timu hiyo bila shinikizo. Ni kama nilivyosema awali, Mwambusi amekutana na wakati ambao umemlazimu kufanya uamuzi mgumu ili kulinda heshima yake. Hakuna anayependa kuharibu ajira yake, lakini una sababu gani ya kusubiri kama mambo yameshaharibika?
Alichofanya Mwambusi ni ujasiri mkubwa kwa sababu, baadhi yetu wakati mwingine, iwe kwa kulewa madaraka au kwa lengo la kujishibisha, tunashindwa kutoa uamuzi mgumu hadi tulazimishwe.
Inawezekana kabisa Mwambusi amebeba msalaba ambao wengi waliutarajia. Kikosi chake kililewa sifa baada ya kufanya vizuri msimu uliopita kiasi cha kushika nafasi ya tatu ligi ilipomalizika.
Ilishangaza kwa timu ngeni, isiyo na wachezaji wenye majina na kocha wa ‘kawaida’ kupata matokeo mazuri kuizidi hata klabu kongwe ya Simba iliyojaza nyota kibao wa ndani na nje.
Kilichoiponza City ni kulewa mafanikio ya msimu uliopita na kudhani kuwa, wanaweza kufanya hivyo kirahisi msimu uliofuata. Walikosea!
Walidhani ligi ni peke yao, kwamba timu zingine zilizofanya vibaya msimu ambao wao walifanya vizuri, basi zingebaki kwenye nafasi hiyo ya kufanya vibaya. Walijidanganya!
Kila mmoja, kwa maana ya mashabiki wa soka Mbeya walikuwa wakisifu mafanikio ya timu hiyo, lakini, ni kwa kiasi gani walikuwa bega kwa bega kuisaidia kufanya vizuri msimu huu?
Sasa Mwambusi amefanya uamuzi mgumu, amejiuzulu. Ameiacha timu kwenye wakati mgumu.

Share this article :
Tweet
✚
Newer Post
Older Post
Home

HABARI ZILIZO BAMBA TOP 10

  • MAREKANI YAITUPIA LAWAMA KOREA KASKAZINI
    Marekani inatarajia kuirudisha Korea kaskazini katika orodha ya nchi zinazofadhili ugaidi. Rais Barack Obama wa Marekani amesema utawala ...
  • MKUU wa Wilaya ya Mufindi mkoani Iringa, Evarista Kalalu, awashauri wananchi kujiunga na mfuko wa afya ya jamii
    MKUU wa Wilaya ya Mufindi mkoani Iringa, Evarista Kalalu, amewashauri wananchi wa vijiji vya Ukami na Chogo Kata ya Mapanda wilayani hapa...
  • KAULI YA UHURU KWENYE MTANDAOWA KIJAMII (TWITTER) KENYATTA HII HAPA
    Taarifa ya mahakama ya ICC, kutupilia mbali kesi dhidi ya Uhuru Kenyatta, imepokelwa na watu wengi nchini Kenya kwa hisia mseto. Baadhi w...
  • HAYA NDIO MAZITO ALIYO FUNGUKA YULE MSICHANA WA KAZI ALIYE MPIGA MTOTO
    Baada ya story ya yule msichana kwa anayefanya kazi za ndani Uganda kuchukua headlines katika vyombo mbalimbali vya Kimataifa Dun...
  • Ronaldo aosha vyombo baada ya kushindwa katika karata na mchezaji wa Tenisi Rafa Nadal
    Ali...
  • Wayne Goss, former premier of Queensland, kicked the bucket at 63
    Mr Goss, who was premier from 1989 to 1996, had suffered from ill health in recent years including brain tumours. He became Q...
  • IT 'S MATTER OF FEW MINUTES FOR WORLD CUP 2014 START SHINNING !!!!
    The World Cup  The 2014  Brazil™ is now just a matter of minutes away and to mark the occasion FIFA have launched an updated version of th...

LABELS

  • Breaking News
  • condolonces
  • Entertainment
  • Entertainments
  • Habari
  • Majonzi
  • Michezo
  • News
  • News and Updates
  • Skendo
  • Sports and Games
Submit ExpressSEO Services & Tools

Total Pageviews

Copyright 2014 Mwanafalsafa
Template By Ridwan Hex And Game Gratis