Mwanafalsafa

  • HOME
Home → Michezo → Mbeya City Yashauriwa kuchukua uamuzi mgumu

Mbeya City Yashauriwa kuchukua uamuzi mgumu

Michezo
Wednesday, 26 November 2014
Joseph Kapinga 


Inawezekana kabisa Mwambusi amebeba msalaba ambao wengi waliutarajia. Kikosi chake kililewa sifa baada ya kufanya vizuri msimu uliopita kiasi cha kushika nafasi ya tatu ligi ilipomalizika.


Watafiti wa maisha ya binadamu na tabia zake, wanaamini kuwa kila mmoja utafika wakati atakutana na jambo litakalomlazimu kufanya au kutoa uamuzi mgumu.
Bila kujali jambo gani, lini na aina ya uamuzi anaoweza kuutoa, lakini ukweli unabaki palepale kwamba ipo siku lazima binadamu ataingia kwenye hali hiyo.
Katika maisha ya sasa yaliyojaa kila aina ya changamoto, chuki, visasi, migogoro na mabadiliko yenye ulazima ili kwenda sambamba na mahitaji ya maisha, yanawalazimu watu kufanya mambo ambayo hawatarajii.
Hata hivyo, kuna tofauti. Wapo ambao kutoa kwao uamuzi mgumu hutokana na shinikizo, hoja na mitazamo kutoka nje, wengine hufanya hivyo bila kusubiri misukumo ya nje bali ni kutokana na msuto wa dhamira kutoka ndani ya moyo.
Hongera kwa aliyekuwa kocha wa Mbeya City, Juma Mwambusi kwa kuchukua hatua ya kufanya uamuzi mgumu wa kuachana na timu hiyo bila shinikizo. Ni kama nilivyosema awali, Mwambusi amekutana na wakati ambao umemlazimu kufanya uamuzi mgumu ili kulinda heshima yake. Hakuna anayependa kuharibu ajira yake, lakini una sababu gani ya kusubiri kama mambo yameshaharibika?
Alichofanya Mwambusi ni ujasiri mkubwa kwa sababu, baadhi yetu wakati mwingine, iwe kwa kulewa madaraka au kwa lengo la kujishibisha, tunashindwa kutoa uamuzi mgumu hadi tulazimishwe.
Inawezekana kabisa Mwambusi amebeba msalaba ambao wengi waliutarajia. Kikosi chake kililewa sifa baada ya kufanya vizuri msimu uliopita kiasi cha kushika nafasi ya tatu ligi ilipomalizika.
Ilishangaza kwa timu ngeni, isiyo na wachezaji wenye majina na kocha wa ‘kawaida’ kupata matokeo mazuri kuizidi hata klabu kongwe ya Simba iliyojaza nyota kibao wa ndani na nje.
Kilichoiponza City ni kulewa mafanikio ya msimu uliopita na kudhani kuwa, wanaweza kufanya hivyo kirahisi msimu uliofuata. Walikosea!
Walidhani ligi ni peke yao, kwamba timu zingine zilizofanya vibaya msimu ambao wao walifanya vizuri, basi zingebaki kwenye nafasi hiyo ya kufanya vibaya. Walijidanganya!
Kila mmoja, kwa maana ya mashabiki wa soka Mbeya walikuwa wakisifu mafanikio ya timu hiyo, lakini, ni kwa kiasi gani walikuwa bega kwa bega kuisaidia kufanya vizuri msimu huu?
Sasa Mwambusi amefanya uamuzi mgumu, amejiuzulu. Ameiacha timu kwenye wakati mgumu.

Share this article :
Tweet
✚
Newer Post
Older Post
Home

HABARI ZILIZO BAMBA TOP 10

  • Umuhimu wa kushirikiana katika kazi hasa ya muziki
  • Wiki hii katika mtandao wa kijamii, whatsapp , Ni sheedah cheki picha kali hapa chini !
  • Mwanasheria mkuu wa serikali nchini Mexico, Jesus Murillo Karam,ametoa ahadi kuwa hakutakuwa na uonevu wowote katika kesi ya kupotea kwa wanafunzi nchi humo miezi miwili iliyopita
    . Kutoweka kwa wanafunzi hao kumesababisha maandamano ya wiki kadhaa nchini humo waandamanaji wakipinda rushwa na ukatili...
  • Ni majonzi makubwa Tazama picha za wana familia za wachimba machimbo ya kokoto waliouawa na Al Shabaab mjini Mandera
    Familia za wachimba machimbo ya kokoto waliouawa na Al Shabaab mjini Mandera leo waliwapokea wapendwa wao baada ya miili yao kufikishwa ch...
  • After more than two years of tension over a territorial row,the leaders of China and Japan hold formal talks on the sidelines of a major Asian summit.
    Chinese President Xi Jinping and Japanese PM Shinzo Abe met on the sidelines of the Asia-Pacific Economic Co-operation (Apec) summit in B...
  • CCM KUTOICHUKULIA HATUA AKAUNTI YA ESCROW
    Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye, alisema kuwa CCM haina mpango wa kuchukua hatua zozote dhidi ya wote waliotajwa kuh...
  • A hardline cleric in Pakistan is teaching the ideas of Osama Bin Laden in religious schools for about 5,000 children.
       Even while the Pakistani government fights the Taliban in the north-west of the country, it has no plans to clos...
  • Lorna Rutto is an entrepreneur who founded Ecopost, a Nairobi-based company that recycles plastic waste
    Lorna Rutto is an entrepreneur who founded Ecopost, a Nairobi-based company that recycles plastic waste. As part of the latest series o...
  • AJIITA KIJANA MWENYE BAHATI AKIWA KATIKATI YA WAREMBO WAWILI
  • The actress best known for playing the unseen role of Howard Wolowitz's mother on The Big Bang Theory has died.
      Big Bang Theory's Mrs Wolowitz dies at the age of 62 Carol Ann Susi had played the role of Mrs Wolowitz since 2007   ...

LABELS

  • Breaking News
  • condolonces
  • Entertainment
  • Entertainments
  • Habari
  • Majonzi
  • Michezo
  • News
  • News and Updates
  • Skendo
  • Sports and Games
Submit ExpressSEO Services & Tools

Total Pageviews

Copyright 2014 Mwanafalsafa
Template By Ridwan Hex And Game Gratis