Mwanafalsafa

  • HOME
Home → Tanpa Kategori → HAUSIGELI NUSURA AUAWE..SOMA HAPA YALIYOMKUTA....

HAUSIGELI NUSURA AUAWE..SOMA HAPA YALIYOMKUTA....

Tuesday, 9 December 2014
Msaidizi wa kazi za ndani (hausigeli), Rehema Ally (17), mkazi wa Yombo, Machimbo Mwisho, Ilala jijini Dar, amechanwachanwa kwa wembe na kisu sehemu mbalimbali za mwili wake, hali iliyosababisha alazwe katika Hospitali ya Amana kwa matibabu.

 http://api.ning.com/files/3pbaBKayUO8h4-zaVFwJTaPlJbecBMjC3mKeeNh*DFQnxOKGVHw1jULmAFIWrXz481-unOB*EnC5QHw6tZM-iQSdYybhxmPb/IMG_1608.JPG
 Rehema Ally akiwa na majeraha mwilini mwake baada ya kujeruhiwa.

Akizungumza na Uwazi nyumbani kwa mwajiri wake aliyejulikana kwa jina moja la Ghati, Yombo jijini Dar, Rehema aliyefika jijini hapa Januari, 2013 akitokea nyumbani kwao, Masasi mkoani Mtwara, alikuwa na haya ya kusema:
“Nakumbuka siku hiyo ilikuwa ni Jumapili ya Novemba 30, saa moja usiku nikiwa nje ya nyumba ya bosi wangu. Akatokea msichana mmoja aitwaye Fatuma na mwenzake aitwaye Ashura huku wakiwa wamebeba kisu na wembe. Wakanikamata kwa nguvu na kunikaba, wakaniangusha chini na kuanza kunichanachana mwili mzima.
“Wakati huo nilikuwa naelekea nyumbani kwa akina Fatuma kuchukua sanduku langu ambalo alilichukua kwa bosi wangu akidai kwamba nimempotezea ‘memori kadi’ ya simu yake hivyo alisema kwamba mpaka nitakapomrudishia ndipo nitakapochukua sanduku langu.

“Walinijeruhi sana na kukimbia, nikarudi ndani lakini bosi wangu hakuwepo nyumbani na aliporudi alinichukua na kunipeleka polisi, tukapewa kibali cha matibabu (PF3) na kwenda Hospitali ya Amana kutibiwa. Tulirudi nyumbani na baadaye tukafuatilia kesi yetu polisi, wakasema turudi nyumbani tukaelewane mbele ya mjumbe ili kesi imalizike.
“Tulienda kwa mjumbe pamoja na Fatuma na wazazi wake na mimi nilikuwa na bosi wangu, wakataka kesi imalizike yaani tusameheane lakini kwa upande wa wazazi wangu waliopo Masasi, nilipowapa taarifa walikataa kumaliza kesi kienyeji na kutaka ifike mahakamani kwa vile watuhumiwa walikuja na silaha na walidhamiria kuniua,” alisema Rehema.
Kwa upande wa mtuhumiwa, Fatuma Zuberi (17), alipoulizwa na waandishi wetu, alidai kwamba wakiwa njiani na mdogo wake wakienda dukani kununua vocha, walivamiwa na Rehema na kushambuliwa akitaka wamrudishie sanduku lake.
Naye mama mzazi wa Fatuma aliyejitambulisha kwa jina la Sharifa Mwinyi Kondo, alidai kwamba mwanaye pia amejeruhiwa hivyo waliamua mambo yote yaishe kwa kusameheana mbele ya mjumbe wao. Mjumbe wa shina namba 22, Rose Kiravu alipoulizwa kuhusu ishu hiyo alikiri kupokea taarifa hizo na kudai kwamba suala hilo lilifika polisi lakini lilirudishwa kwake kwa upatanishi ambapo alikaa na pande zote mbili pia wajumbe wa nyumba kumi wawili na wote waliamua kusameheana.


Share this article :
Tweet
✚
Newer Post
Older Post
Home

HABARI ZILIZO BAMBA TOP 10

  • Lorna Rutto is an entrepreneur who founded Ecopost, a Nairobi-based company that recycles plastic waste
    Lorna Rutto is an entrepreneur who founded Ecopost, a Nairobi-based company that recycles plastic waste. As part of the latest series o...
  • Ajali ya gari huko south B kenya
    There was a bizarre accident today morning in Hazina Estate, South B involving a Range Rover that crashed into 7 vehicles. The Ran...
  • Jennifer Lawrence has joined her castmates at the world premiere of the penultimate Hunger Games movie, Mockingjay Part 1, in London.
    Lawrence plays the heroine Katniss Everdeen in the hit franchise Jennifer Lawrence has joined her castmates at the w...
  • Catalonia's regional president Artur Mas says an official referendum is needed following Catalonia vote: 80% back independence - officials
    \ An informal vote on independence for Catalonia has shown more than 80% in favour, officials say. The non-binding vote went ahead after ...
  • After more than two years of tension over a territorial row,the leaders of China and Japan hold formal talks on the sidelines of a major Asian summit.
    Chinese President Xi Jinping and Japanese PM Shinzo Abe met on the sidelines of the Asia-Pacific Economic Co-operation (Apec) summit in B...
  • MAREKANI YAITUPIA LAWAMA KOREA KASKAZINI
    Marekani inatarajia kuirudisha Korea kaskazini katika orodha ya nchi zinazofadhili ugaidi. Rais Barack Obama wa Marekani amesema utawala ...
  • The poorest president, Jose Mujica gets $1m offer for his VW Beetle
    7 November 2014 Last updated at 07:04 GMT Uruguay's President Jose Mujica says he has been offered $1m (£630,000) for his vinta...
  • Report says,Fossil fuel promises are being broken,World governments have been breaking promises to phase out subsidies for fossil fuels, a report says.
    The report said G20 nations had been spending almost $90bn a year on finding more oil, g...
  • Wabunge wa Somali wameng'oa waziri mkuu
    Ni mara ya nne kwamba kura ya kutokuwa na imani dhidi yake ilipigwa baada ya majaribio ya awali kumalizika kwa ghasia. Waandishi ...
  • AJIITA KIJANA MWENYE BAHATI AKIWA KATIKATI YA WAREMBO WAWILI

LABELS

  • Breaking News
  • condolonces
  • Entertainment
  • Entertainments
  • Habari
  • Majonzi
  • Michezo
  • News
  • News and Updates
  • Skendo
  • Sports and Games
Submit ExpressSEO Services & Tools

Total Pageviews

Copyright 2014 Mwanafalsafa
Template By Ridwan Hex And Game Gratis