Mwanafalsafa

  • HOME
Home → Habari → Maonyesho ya elimu yaweza kuibua mambo mazuri zaidi

Maonyesho ya elimu yaweza kuibua mambo mazuri zaidi

Habari
Tuesday, 25 November 2014
KATIKA kutatua baadhi ya changamoto zinazohusu masuala ya elimu kwa vijana nchini, imebainika hali hiyo wakati mwingine inachangiwa na sekta husika kutokuwa na mawasiliano ya karibu.
Hata hivyo, baadhi ya wadau baada ya kubaini changamoto hizo hivi sasa wanajipanga kujenga mtandao katika sekta zote za elimu na kuwa kitu kimoja.
Akizungumzia hali hiyo, Mkurugezi Mkuu wa Global Education Link LTD (Gel), Abdulmalik Mollel, anasema ili kuzipatia ufumbuzi wa kudumu changamoto hizi wameandaa maeonyesho ya elimu.
Maonyesho hayo ya kwanza na kimataifa ambayo yanatarajiwa kufanyika katika viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere, kuanzia Desemba 10 hadi 14 mwaka huu.
Anasema maonyesho hayo yanaandaliwa na kuratibiwa na Global Education Link Ltd (Gel), kwa kushirikiana na Ofisi ya Waziri Mkuu (Tamisemi), Wizara ya Elimu, Mafunzo na Ufundi na Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TanTrade).
“Maonyesho haya yanatarajiwa kuvuta washiriki zaidi 500 na watembeleaji zaidi ya 350,000 kutoka ndani na nje ya nchi.
“Kaulimbiu ya maonyesho haya ni ‘Kuweka jitihada za pamoja katika kuboresha mfumo wa elimu Tanzania ni njia thabiti ya kuleta maendeleo endelevu katika taifa,” anasema Mollel.
Mollel anasema lengo kuu la maonyesho hayo ni kuwaunganisha wadau wote wa elimu kwa pamoja, ili waweza kutoa huduma kwa wananchi na kuwaelimisha juu ya mambo muhimu yaliyopo katika sekta husika.
Anafafanua kwa kuwataja wadau wa sekta binafsi wa elimu ambao ni mifuko ya pensheni, wachapishaji wa vifaa vya shule, taasisi za kielimu.
Nyingine ni asasi za kielimu, vyuo vikuu vya elimu vya ndani na nje ya nchi, shule za awali na sekondari pamoja na wadau wengine, akibainisha kuwa itakuwa ni sehemu yao kuuza bidhaa zao mbele ya wadau lengwa.
Mollel anasema maonyesho hayo yataleta manufaa makubwa na changamoto chanya hasa kuongeza ushindani katika sekta ya elimu ambayo itasaidia mpango wa Matokeo Makubwa Sasa (RBN).
“Warsha kama hizi za elimu zina lengo la kuhamasisha ubora wa elimu na uchumi kutokana na hali halisi ya nchi yetu,”anasema Mollel.
Anataja baadhi ya faida katika ushiriki wa asasi mbalimbali nchini kwa uchache ni pamoja na kutengeneza ushindani wa bidhaa za elimu katika sekta za elimu nchini zitakazosababisha elimu yenye tija na kwenda na soko la ajira ndani na nje ya nchi.
Faida nyingine ni njia pekee ya kubadilishana na kuonyeshana ujuzi kutoka shule moja hadi nyingine, na wananchi watapata fursa ya kupata nafasi ya shule au chuo na kuweza kupata taarifa kwa uwazi juu ya elimu ya ndani katika eneo moja bila urasimu ndani ya eneo husika.
Pia wananchi watapata nafasi ya kuchagua kozi na kuzielewa vizuri kabla ya kufanya maamuzi yao ya mwisho na wanafunzi wazazi watapata ushauri kuhusu kozi mbalimbali wanazotaka watoto wao wakasome.
“Tume ya Vyuo Vikuu, sekta mbalimbali za elimu, benki na washiriki wengine toka nje ya nchi zitapata nafasi ya kutoa mada na kuuza biashara zao kwa wananchi zinazohusiana na bidhaa za elimu,”anaeleza Mollel.
Mkurugenzi Mkuu wa TanTrade,  Jacqueline Maleko, anasema ili kuweza kufanya vizuri katika mambo mbalimbali yanayohusu biashara ni lazima kuwa na elimu ya kutosha, hivyo maonyesho hayo yatawasaidia wanafunzi kupata elimu bora itakayowasaidia kufanya biashara zao kwa umakini.
“Kama sekta ya elimu hatutaijengea mazingira mazuri na vijana wakaweza kujiari, kuna hatari hapo baadaye nchi ikaja kuingia katika mifarakano makubwa.
“Wakati vijana wa mataifa ya wenzetu walipata nafasi mbalimbali za kazi hapa nchini wa kwetu wanakosa kwa madai kuwa hawaajiriki,”anasema Jacqueline.
Anasema vijana wengi wa nje wanapata ajira nchini kwa sababu nchi zao zimekuwa zikifanya vizuri katika kujitangaza kimataifa.
“Sisi tunavyo vyuo vikuu ambavyo ni vizuri, lakini tunashindwa kuvitangaza," anasema Jacqueline.
Hata hivyo, Maleko amewataka wanafunzi pamoja na wazazi kujitokeza kwa wingi katika maonyesho.

Share this article :
Tweet
✚
Newer Post
Older Post
Home

HABARI ZILIZO BAMBA TOP 10

  • The World leaders are arriving in Australia for this weekend's G20 summit in the Queensland city of Brisbane.
      The two-day summit, attended by the US, Chinese and Russian leaders among others, will focus on promoting growth. Australian Pri...
  • Ronaldo aosha vyombo baada ya kushindwa katika karata na mchezaji wa Tenisi Rafa Nadal
    Ali...
  • In long, dimly lit hallways, clusters of people wait anxiously outside courtrooms for their cases to come before a judge.
    The New York Immigration Court is an extraordinarily busy place. In long, dimly lit hallways, clusters of people wait anxiously outside co...
  • Chinese leader Xi Jinping has urged Asia-Pacific nations to accelerate economic integration to spur global growth, on day two of the Apec summit.
    The high-level meeting includes the leaders of the US, Russia, China, Japan and others He spoke as leaders from the 21-na...
  • John Doar, a civil rights lawyer who was a key figure in the struggle against racial segregation in the US, has died aged 92.
    John Doar was awarded the Presidential Medal of Freedom in 2012 Mr Doar dealt with some of the most prominent civil rights ca...
  • Ukweli kuhusu umoja wa fedha,Jumuiya ya Afrika Mashariki.
      OKTOBA 20 hadi 24 mwaka  huu, Benki Kuu ya Tanzania (BoT) iliandaa semi...
  • Kiungo mpya wa Azam, Amri Kiemba akiwa katika jezi ya timu hiyo kwenye Uwanja wa Chamazi, Dar es Salaam jana
       Klabu ya Yanga imemleta nchini kwa majaribio mshambuliaji raia wa Zambia, Jonas Sakuwaha ...
  • Rais wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa ametunukiwa Tuzo ya Mafanikio Katika Utumishi wa Umma kutokana na mchango alioutoa kwenye uchumi wakati wa utawala wake.
      Kwa ufupi Kufanya kazi bila kuchoka, kusisitiza uwazi na ukweli katika kuboresha uchumi katika kipindi chake kwampaisha....
  • Dies aged 87,singing legend, Sabah, Lebanese
      Sabah was nicknamed "Shahroura", Arabic for "singing bird" by her mil...
  • Tatizo la kuwapo bandari bubu linazidi kuongezeka.
    Rais Jakaya Kikwete.PICHA|MAKTABA   Jeshi la Polisi mkoani Tanga ju...

LABELS

  • Breaking News
  • condolonces
  • Entertainment
  • Entertainments
  • Habari
  • Majonzi
  • Michezo
  • News
  • News and Updates
  • Skendo
  • Sports and Games
Submit ExpressSEO Services & Tools

Total Pageviews

Copyright 2014 Mwanafalsafa
Template By Ridwan Hex And Game Gratis