Mwanafalsafa

  • HOME
Home → Habari → Maonyesho ya elimu yaweza kuibua mambo mazuri zaidi

Maonyesho ya elimu yaweza kuibua mambo mazuri zaidi

Habari
Tuesday, 25 November 2014
KATIKA kutatua baadhi ya changamoto zinazohusu masuala ya elimu kwa vijana nchini, imebainika hali hiyo wakati mwingine inachangiwa na sekta husika kutokuwa na mawasiliano ya karibu.
Hata hivyo, baadhi ya wadau baada ya kubaini changamoto hizo hivi sasa wanajipanga kujenga mtandao katika sekta zote za elimu na kuwa kitu kimoja.
Akizungumzia hali hiyo, Mkurugezi Mkuu wa Global Education Link LTD (Gel), Abdulmalik Mollel, anasema ili kuzipatia ufumbuzi wa kudumu changamoto hizi wameandaa maeonyesho ya elimu.
Maonyesho hayo ya kwanza na kimataifa ambayo yanatarajiwa kufanyika katika viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere, kuanzia Desemba 10 hadi 14 mwaka huu.
Anasema maonyesho hayo yanaandaliwa na kuratibiwa na Global Education Link Ltd (Gel), kwa kushirikiana na Ofisi ya Waziri Mkuu (Tamisemi), Wizara ya Elimu, Mafunzo na Ufundi na Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TanTrade).
“Maonyesho haya yanatarajiwa kuvuta washiriki zaidi 500 na watembeleaji zaidi ya 350,000 kutoka ndani na nje ya nchi.
“Kaulimbiu ya maonyesho haya ni ‘Kuweka jitihada za pamoja katika kuboresha mfumo wa elimu Tanzania ni njia thabiti ya kuleta maendeleo endelevu katika taifa,” anasema Mollel.
Mollel anasema lengo kuu la maonyesho hayo ni kuwaunganisha wadau wote wa elimu kwa pamoja, ili waweza kutoa huduma kwa wananchi na kuwaelimisha juu ya mambo muhimu yaliyopo katika sekta husika.
Anafafanua kwa kuwataja wadau wa sekta binafsi wa elimu ambao ni mifuko ya pensheni, wachapishaji wa vifaa vya shule, taasisi za kielimu.
Nyingine ni asasi za kielimu, vyuo vikuu vya elimu vya ndani na nje ya nchi, shule za awali na sekondari pamoja na wadau wengine, akibainisha kuwa itakuwa ni sehemu yao kuuza bidhaa zao mbele ya wadau lengwa.
Mollel anasema maonyesho hayo yataleta manufaa makubwa na changamoto chanya hasa kuongeza ushindani katika sekta ya elimu ambayo itasaidia mpango wa Matokeo Makubwa Sasa (RBN).
“Warsha kama hizi za elimu zina lengo la kuhamasisha ubora wa elimu na uchumi kutokana na hali halisi ya nchi yetu,”anasema Mollel.
Anataja baadhi ya faida katika ushiriki wa asasi mbalimbali nchini kwa uchache ni pamoja na kutengeneza ushindani wa bidhaa za elimu katika sekta za elimu nchini zitakazosababisha elimu yenye tija na kwenda na soko la ajira ndani na nje ya nchi.
Faida nyingine ni njia pekee ya kubadilishana na kuonyeshana ujuzi kutoka shule moja hadi nyingine, na wananchi watapata fursa ya kupata nafasi ya shule au chuo na kuweza kupata taarifa kwa uwazi juu ya elimu ya ndani katika eneo moja bila urasimu ndani ya eneo husika.
Pia wananchi watapata nafasi ya kuchagua kozi na kuzielewa vizuri kabla ya kufanya maamuzi yao ya mwisho na wanafunzi wazazi watapata ushauri kuhusu kozi mbalimbali wanazotaka watoto wao wakasome.
“Tume ya Vyuo Vikuu, sekta mbalimbali za elimu, benki na washiriki wengine toka nje ya nchi zitapata nafasi ya kutoa mada na kuuza biashara zao kwa wananchi zinazohusiana na bidhaa za elimu,”anaeleza Mollel.
Mkurugenzi Mkuu wa TanTrade,  Jacqueline Maleko, anasema ili kuweza kufanya vizuri katika mambo mbalimbali yanayohusu biashara ni lazima kuwa na elimu ya kutosha, hivyo maonyesho hayo yatawasaidia wanafunzi kupata elimu bora itakayowasaidia kufanya biashara zao kwa umakini.
“Kama sekta ya elimu hatutaijengea mazingira mazuri na vijana wakaweza kujiari, kuna hatari hapo baadaye nchi ikaja kuingia katika mifarakano makubwa.
“Wakati vijana wa mataifa ya wenzetu walipata nafasi mbalimbali za kazi hapa nchini wa kwetu wanakosa kwa madai kuwa hawaajiriki,”anasema Jacqueline.
Anasema vijana wengi wa nje wanapata ajira nchini kwa sababu nchi zao zimekuwa zikifanya vizuri katika kujitangaza kimataifa.
“Sisi tunavyo vyuo vikuu ambavyo ni vizuri, lakini tunashindwa kuvitangaza," anasema Jacqueline.
Hata hivyo, Maleko amewataka wanafunzi pamoja na wazazi kujitokeza kwa wingi katika maonyesho.

Share this article :
Tweet
✚
Newer Post
Older Post
Home

HABARI ZILIZO BAMBA TOP 10

  • MAREKANI YAITUPIA LAWAMA KOREA KASKAZINI
    Marekani inatarajia kuirudisha Korea kaskazini katika orodha ya nchi zinazofadhili ugaidi. Rais Barack Obama wa Marekani amesema utawala ...
  • Mombasa based singer akothee gets naughty,Angalia hapa
  • Vita dhidi ya Ukimwi zashika kasi, mbinu madhubuti zachukuliwa !
    DESEMBA mosi, kila mwaka, watu wote duniani huadhimisha Siku ya Ukimwi Duniani. Siku hiyo ilianzishwa mwaka 1987 na hubeba maudhui mbalim...
  • ,Juncker reveals giant EU investment planJuncker said Europe needed a kick-start and the Commission was offering the jump-leads
    Mr  European Commission President Jean-Claude Juncker has given details of a €315bn (£250bn;$393bn) investment plan to kic...
  • Kwaninii serikali imewekeza katika siasa na imesahau wakulima ?
      Hata hivyo, wakulima wamekwazwa na kodi nyingi wanazotozwa kwa kila gunia inapotokea wakauza sehemu ya ...
  • Mdogo wa Zari Hassan apaka matope uhusiano wake na Diamond
    Mdogo wake na Zari Hassan aka The Bosslady, aitwaye Karim ametumia Facebook kumkosoa dada yake kwa kuwa na uhusiano na Diamond Platnumz amb...
  • DAVIDO,TIWA SWAGE,DIAMOND, MR.FLAVOUR ON THE SHOOT,CHECK THE NEW VIDEO HERE
    Africa MultiChoice has launched it’s biggest  campaign yet, to celebrate Africa’s positivity , successes and the ability to  te...
  • Wayne Goss, former premier of Queensland, kicked the bucket at 63
    Mr Goss, who was premier from 1989 to 1996, had suffered from ill health in recent years including brain tumours. He became Q...
  • Third death confirmed in Mali The Pasteur Clinic in Bamako has been placed in quarantine and is under armed guard
      A nurse and the patient he was treating have become the second and third people to die from Ebola in Mali. The patient,...
  • The poorest president, Jose Mujica gets $1m offer for his VW Beetle
    7 November 2014 Last updated at 07:04 GMT Uruguay's President Jose Mujica says he has been offered $1m (£630,000) for his vinta...

LABELS

  • Breaking News
  • condolonces
  • Entertainment
  • Entertainments
  • Habari
  • Majonzi
  • Michezo
  • News
  • News and Updates
  • Skendo
  • Sports and Games
Submit ExpressSEO Services & Tools

Total Pageviews

Copyright 2014 Mwanafalsafa
Template By Ridwan Hex And Game Gratis