Mwanafalsafa

  • HOME
Home → Habari → Maonyesho ya elimu yaweza kuibua mambo mazuri zaidi

Maonyesho ya elimu yaweza kuibua mambo mazuri zaidi

Habari
Tuesday, 25 November 2014
KATIKA kutatua baadhi ya changamoto zinazohusu masuala ya elimu kwa vijana nchini, imebainika hali hiyo wakati mwingine inachangiwa na sekta husika kutokuwa na mawasiliano ya karibu.
Hata hivyo, baadhi ya wadau baada ya kubaini changamoto hizo hivi sasa wanajipanga kujenga mtandao katika sekta zote za elimu na kuwa kitu kimoja.
Akizungumzia hali hiyo, Mkurugezi Mkuu wa Global Education Link LTD (Gel), Abdulmalik Mollel, anasema ili kuzipatia ufumbuzi wa kudumu changamoto hizi wameandaa maeonyesho ya elimu.
Maonyesho hayo ya kwanza na kimataifa ambayo yanatarajiwa kufanyika katika viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere, kuanzia Desemba 10 hadi 14 mwaka huu.
Anasema maonyesho hayo yanaandaliwa na kuratibiwa na Global Education Link Ltd (Gel), kwa kushirikiana na Ofisi ya Waziri Mkuu (Tamisemi), Wizara ya Elimu, Mafunzo na Ufundi na Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TanTrade).
“Maonyesho haya yanatarajiwa kuvuta washiriki zaidi 500 na watembeleaji zaidi ya 350,000 kutoka ndani na nje ya nchi.
“Kaulimbiu ya maonyesho haya ni ‘Kuweka jitihada za pamoja katika kuboresha mfumo wa elimu Tanzania ni njia thabiti ya kuleta maendeleo endelevu katika taifa,” anasema Mollel.
Mollel anasema lengo kuu la maonyesho hayo ni kuwaunganisha wadau wote wa elimu kwa pamoja, ili waweza kutoa huduma kwa wananchi na kuwaelimisha juu ya mambo muhimu yaliyopo katika sekta husika.
Anafafanua kwa kuwataja wadau wa sekta binafsi wa elimu ambao ni mifuko ya pensheni, wachapishaji wa vifaa vya shule, taasisi za kielimu.
Nyingine ni asasi za kielimu, vyuo vikuu vya elimu vya ndani na nje ya nchi, shule za awali na sekondari pamoja na wadau wengine, akibainisha kuwa itakuwa ni sehemu yao kuuza bidhaa zao mbele ya wadau lengwa.
Mollel anasema maonyesho hayo yataleta manufaa makubwa na changamoto chanya hasa kuongeza ushindani katika sekta ya elimu ambayo itasaidia mpango wa Matokeo Makubwa Sasa (RBN).
“Warsha kama hizi za elimu zina lengo la kuhamasisha ubora wa elimu na uchumi kutokana na hali halisi ya nchi yetu,”anasema Mollel.
Anataja baadhi ya faida katika ushiriki wa asasi mbalimbali nchini kwa uchache ni pamoja na kutengeneza ushindani wa bidhaa za elimu katika sekta za elimu nchini zitakazosababisha elimu yenye tija na kwenda na soko la ajira ndani na nje ya nchi.
Faida nyingine ni njia pekee ya kubadilishana na kuonyeshana ujuzi kutoka shule moja hadi nyingine, na wananchi watapata fursa ya kupata nafasi ya shule au chuo na kuweza kupata taarifa kwa uwazi juu ya elimu ya ndani katika eneo moja bila urasimu ndani ya eneo husika.
Pia wananchi watapata nafasi ya kuchagua kozi na kuzielewa vizuri kabla ya kufanya maamuzi yao ya mwisho na wanafunzi wazazi watapata ushauri kuhusu kozi mbalimbali wanazotaka watoto wao wakasome.
“Tume ya Vyuo Vikuu, sekta mbalimbali za elimu, benki na washiriki wengine toka nje ya nchi zitapata nafasi ya kutoa mada na kuuza biashara zao kwa wananchi zinazohusiana na bidhaa za elimu,”anaeleza Mollel.
Mkurugenzi Mkuu wa TanTrade,  Jacqueline Maleko, anasema ili kuweza kufanya vizuri katika mambo mbalimbali yanayohusu biashara ni lazima kuwa na elimu ya kutosha, hivyo maonyesho hayo yatawasaidia wanafunzi kupata elimu bora itakayowasaidia kufanya biashara zao kwa umakini.
“Kama sekta ya elimu hatutaijengea mazingira mazuri na vijana wakaweza kujiari, kuna hatari hapo baadaye nchi ikaja kuingia katika mifarakano makubwa.
“Wakati vijana wa mataifa ya wenzetu walipata nafasi mbalimbali za kazi hapa nchini wa kwetu wanakosa kwa madai kuwa hawaajiriki,”anasema Jacqueline.
Anasema vijana wengi wa nje wanapata ajira nchini kwa sababu nchi zao zimekuwa zikifanya vizuri katika kujitangaza kimataifa.
“Sisi tunavyo vyuo vikuu ambavyo ni vizuri, lakini tunashindwa kuvitangaza," anasema Jacqueline.
Hata hivyo, Maleko amewataka wanafunzi pamoja na wazazi kujitokeza kwa wingi katika maonyesho.

Share this article :
Tweet
✚
Newer Post
Older Post
Home

HABARI ZILIZO BAMBA TOP 10

  • Umuhimu wa kushirikiana katika kazi hasa ya muziki
  • Wiki hii katika mtandao wa kijamii, whatsapp , Ni sheedah cheki picha kali hapa chini !
  • Mwanasheria mkuu wa serikali nchini Mexico, Jesus Murillo Karam,ametoa ahadi kuwa hakutakuwa na uonevu wowote katika kesi ya kupotea kwa wanafunzi nchi humo miezi miwili iliyopita
    . Kutoweka kwa wanafunzi hao kumesababisha maandamano ya wiki kadhaa nchini humo waandamanaji wakipinda rushwa na ukatili...
  • Ni majonzi makubwa Tazama picha za wana familia za wachimba machimbo ya kokoto waliouawa na Al Shabaab mjini Mandera
    Familia za wachimba machimbo ya kokoto waliouawa na Al Shabaab mjini Mandera leo waliwapokea wapendwa wao baada ya miili yao kufikishwa ch...
  • After more than two years of tension over a territorial row,the leaders of China and Japan hold formal talks on the sidelines of a major Asian summit.
    Chinese President Xi Jinping and Japanese PM Shinzo Abe met on the sidelines of the Asia-Pacific Economic Co-operation (Apec) summit in B...
  • CCM KUTOICHUKULIA HATUA AKAUNTI YA ESCROW
    Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye, alisema kuwa CCM haina mpango wa kuchukua hatua zozote dhidi ya wote waliotajwa kuh...
  • A hardline cleric in Pakistan is teaching the ideas of Osama Bin Laden in religious schools for about 5,000 children.
       Even while the Pakistani government fights the Taliban in the north-west of the country, it has no plans to clos...
  • Lorna Rutto is an entrepreneur who founded Ecopost, a Nairobi-based company that recycles plastic waste
    Lorna Rutto is an entrepreneur who founded Ecopost, a Nairobi-based company that recycles plastic waste. As part of the latest series o...
  • AJIITA KIJANA MWENYE BAHATI AKIWA KATIKATI YA WAREMBO WAWILI
  • HIVI NDIVYO Gangnam Walivyovunja rekodi huko YouTube
    Jump media player Media player help Out of media player. Press enter to return or tab to continue. Na Kim Kardashian a...

LABELS

  • Breaking News
  • condolonces
  • Entertainment
  • Entertainments
  • Habari
  • Majonzi
  • Michezo
  • News
  • News and Updates
  • Skendo
  • Sports and Games
Submit ExpressSEO Services & Tools

Total Pageviews

Copyright 2014 Mwanafalsafa
Template By Ridwan Hex And Game Gratis