Mwanafalsafa

  • HOME
Home → Tanpa Kategori → MASTAA WENGI TUTAKUFA NA UKIMWI...WENYEWE WAFUNGUKA..

MASTAA WENGI TUTAKUFA NA UKIMWI...WENYEWE WAFUNGUKA..

Saturday, 20 December 2014
WASANII wengi wa kike wamekuwa na tabia ya kuibiana mabwana jambo ambalo wenyewe wamekiri kwamba wako kwenye hatari ya kupukutika kama kuku kwa ugonjwa hatari wa Ukimwi.Wakizungumza  baadhi ya mastaa wenye majina makubwa Bongo walifungukia kamchezo hako ka kushea mabwana na wakati mwingine hufanya tendo hilo pasipo kutumia kinga. Tujiunge na baadhi ya mastaa waliozungumzia ishu hiyo:


Staa katika tasnia ya filamu Bongo,Tamrina Poshi 'Amanda'.

TAMRINA POSHI ‘AMANDA’
Wasanii wa kike wengi ni malimbukeni kwani wakiona flani ana maendeleo na yupo na mwanaume flani wanammendea na kumchukua. Nina uhakika kutokana na tabia hii wengi tukienda kupima Ukimwi itakuwa ni hatari, hakuna atakayepona.

TIKO HASSAN
Tabia hii ni ushamba pia kutokuwa waaminifu. Wapo wasanii walishawahi kunichukulia mwanaume wangu lakini siwezi kuwataja ila inakera sana. 
Kama ni ugonjwa wa Ukimwi basi utatuua wengi kwa sababu ya ushamba maana mtu akikuona uko na mtu wako anammendea wakati kabla hujawa naye walikuwa wanapishana tu.


Staa katika tasnia ya filamu Bongo,Zuwena Mohamed 'Shilole'.

ZUWENA MOHAMED ‘SHILOLE’
Ukweli hawana adabu na hawajafunzwa huko makwao. Kutokana na tabia hii ya kuchukuliana mabwana wengi tutaambukizana Ukimwi  maana hatujiheshimu.

ISABELA MPANDA
Mimi nasema hivi, asilimia 90 ya wasanii wa kike wana Ukimwi kwa sababu wana tamaa sana. Utakuta mwanaume mmoja anatoka kimapenzi na wasanii kumi huoni hii ni hatari?

ISABELA FRANCIS ‘VAI WA UKWELI’
Huwa nawasikia mastaa wengi wa kike wakilalamika kuibiana mabwana lakini mimi sijawahi kuiba nimetulia na Bonny wangu. Lakini tukija kwenye suala la maradhi ukweli kwa tabia hiyo, ni rahisi sana kuambukizana Ukimwi.

SALOME URASSA  ‘Thea’
Tuache hiyo tabia ya kujirahisisha kwa  sababu kwanza wanaume wanatudharau pia jamii inatuona sisi wasanii ni m****** ukiona mwenzako ana mtu wake mheshimu kama shemeji yako.
Kwa staili hii, Ukimwi ukianza kuua, itakuwa ni hatari kwa sababu asilimia 80 tutakufa kwa ngoma.


Staa katika tasnia ya filamu Bongo, Lulu Semagongo 'Aunt lulu.

LULU SEMAGONGO ‘AUNTY LULU’
Hii tabia ya kuibiana mabwana ipo sana kwani unakuta mtu anajua kabisa mimi natoka na mwanaume flani naye anajipenyeza. Ukimwi utatumaliza kila siku maana mzunguko wa wanaume na wanawake ni uleule.

Share this article :
Tweet
✚
Newer Post
Older Post
Home

HABARI ZILIZO BAMBA TOP 10

  • The World leaders are arriving in Australia for this weekend's G20 summit in the Queensland city of Brisbane.
      The two-day summit, attended by the US, Chinese and Russian leaders among others, will focus on promoting growth. Australian Pri...
  • Ronaldo aosha vyombo baada ya kushindwa katika karata na mchezaji wa Tenisi Rafa Nadal
    Ali...
  • In long, dimly lit hallways, clusters of people wait anxiously outside courtrooms for their cases to come before a judge.
    The New York Immigration Court is an extraordinarily busy place. In long, dimly lit hallways, clusters of people wait anxiously outside co...
  • Chinese leader Xi Jinping has urged Asia-Pacific nations to accelerate economic integration to spur global growth, on day two of the Apec summit.
    The high-level meeting includes the leaders of the US, Russia, China, Japan and others He spoke as leaders from the 21-na...
  • John Doar, a civil rights lawyer who was a key figure in the struggle against racial segregation in the US, has died aged 92.
    John Doar was awarded the Presidential Medal of Freedom in 2012 Mr Doar dealt with some of the most prominent civil rights ca...
  • Ukweli kuhusu umoja wa fedha,Jumuiya ya Afrika Mashariki.
      OKTOBA 20 hadi 24 mwaka  huu, Benki Kuu ya Tanzania (BoT) iliandaa semi...
  • Kiungo mpya wa Azam, Amri Kiemba akiwa katika jezi ya timu hiyo kwenye Uwanja wa Chamazi, Dar es Salaam jana
       Klabu ya Yanga imemleta nchini kwa majaribio mshambuliaji raia wa Zambia, Jonas Sakuwaha ...
  • Rais wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa ametunukiwa Tuzo ya Mafanikio Katika Utumishi wa Umma kutokana na mchango alioutoa kwenye uchumi wakati wa utawala wake.
      Kwa ufupi Kufanya kazi bila kuchoka, kusisitiza uwazi na ukweli katika kuboresha uchumi katika kipindi chake kwampaisha....
  • Dies aged 87,singing legend, Sabah, Lebanese
      Sabah was nicknamed "Shahroura", Arabic for "singing bird" by her mil...
  • Tatizo la kuwapo bandari bubu linazidi kuongezeka.
    Rais Jakaya Kikwete.PICHA|MAKTABA   Jeshi la Polisi mkoani Tanga ju...

LABELS

  • Breaking News
  • condolonces
  • Entertainment
  • Entertainments
  • Habari
  • Majonzi
  • Michezo
  • News
  • News and Updates
  • Skendo
  • Sports and Games
Submit ExpressSEO Services & Tools

Total Pageviews

Copyright 2014 Mwanafalsafa
Template By Ridwan Hex And Game Gratis