Mwanafalsafa

  • HOME
Home → Tanpa Kategori → MASTAA WENGI TUTAKUFA NA UKIMWI...WENYEWE WAFUNGUKA..

MASTAA WENGI TUTAKUFA NA UKIMWI...WENYEWE WAFUNGUKA..

Saturday, 20 December 2014
WASANII wengi wa kike wamekuwa na tabia ya kuibiana mabwana jambo ambalo wenyewe wamekiri kwamba wako kwenye hatari ya kupukutika kama kuku kwa ugonjwa hatari wa Ukimwi.Wakizungumza  baadhi ya mastaa wenye majina makubwa Bongo walifungukia kamchezo hako ka kushea mabwana na wakati mwingine hufanya tendo hilo pasipo kutumia kinga. Tujiunge na baadhi ya mastaa waliozungumzia ishu hiyo:


Staa katika tasnia ya filamu Bongo,Tamrina Poshi 'Amanda'.

TAMRINA POSHI ‘AMANDA’
Wasanii wa kike wengi ni malimbukeni kwani wakiona flani ana maendeleo na yupo na mwanaume flani wanammendea na kumchukua. Nina uhakika kutokana na tabia hii wengi tukienda kupima Ukimwi itakuwa ni hatari, hakuna atakayepona.

TIKO HASSAN
Tabia hii ni ushamba pia kutokuwa waaminifu. Wapo wasanii walishawahi kunichukulia mwanaume wangu lakini siwezi kuwataja ila inakera sana. 
Kama ni ugonjwa wa Ukimwi basi utatuua wengi kwa sababu ya ushamba maana mtu akikuona uko na mtu wako anammendea wakati kabla hujawa naye walikuwa wanapishana tu.


Staa katika tasnia ya filamu Bongo,Zuwena Mohamed 'Shilole'.

ZUWENA MOHAMED ‘SHILOLE’
Ukweli hawana adabu na hawajafunzwa huko makwao. Kutokana na tabia hii ya kuchukuliana mabwana wengi tutaambukizana Ukimwi  maana hatujiheshimu.

ISABELA MPANDA
Mimi nasema hivi, asilimia 90 ya wasanii wa kike wana Ukimwi kwa sababu wana tamaa sana. Utakuta mwanaume mmoja anatoka kimapenzi na wasanii kumi huoni hii ni hatari?

ISABELA FRANCIS ‘VAI WA UKWELI’
Huwa nawasikia mastaa wengi wa kike wakilalamika kuibiana mabwana lakini mimi sijawahi kuiba nimetulia na Bonny wangu. Lakini tukija kwenye suala la maradhi ukweli kwa tabia hiyo, ni rahisi sana kuambukizana Ukimwi.

SALOME URASSA  ‘Thea’
Tuache hiyo tabia ya kujirahisisha kwa  sababu kwanza wanaume wanatudharau pia jamii inatuona sisi wasanii ni m****** ukiona mwenzako ana mtu wake mheshimu kama shemeji yako.
Kwa staili hii, Ukimwi ukianza kuua, itakuwa ni hatari kwa sababu asilimia 80 tutakufa kwa ngoma.


Staa katika tasnia ya filamu Bongo, Lulu Semagongo 'Aunt lulu.

LULU SEMAGONGO ‘AUNTY LULU’
Hii tabia ya kuibiana mabwana ipo sana kwani unakuta mtu anajua kabisa mimi natoka na mwanaume flani naye anajipenyeza. Ukimwi utatumaliza kila siku maana mzunguko wa wanaume na wanawake ni uleule.

Share this article :
Tweet
✚
Newer Post
Older Post
Home

HABARI ZILIZO BAMBA TOP 10

  • MAREKANI YAITUPIA LAWAMA KOREA KASKAZINI
    Marekani inatarajia kuirudisha Korea kaskazini katika orodha ya nchi zinazofadhili ugaidi. Rais Barack Obama wa Marekani amesema utawala ...
  • Mombasa based singer akothee gets naughty,Angalia hapa
  • Vita dhidi ya Ukimwi zashika kasi, mbinu madhubuti zachukuliwa !
    DESEMBA mosi, kila mwaka, watu wote duniani huadhimisha Siku ya Ukimwi Duniani. Siku hiyo ilianzishwa mwaka 1987 na hubeba maudhui mbalim...
  • ,Juncker reveals giant EU investment planJuncker said Europe needed a kick-start and the Commission was offering the jump-leads
    Mr  European Commission President Jean-Claude Juncker has given details of a €315bn (£250bn;$393bn) investment plan to kic...
  • Kwaninii serikali imewekeza katika siasa na imesahau wakulima ?
      Hata hivyo, wakulima wamekwazwa na kodi nyingi wanazotozwa kwa kila gunia inapotokea wakauza sehemu ya ...
  • Mdogo wa Zari Hassan apaka matope uhusiano wake na Diamond
    Mdogo wake na Zari Hassan aka The Bosslady, aitwaye Karim ametumia Facebook kumkosoa dada yake kwa kuwa na uhusiano na Diamond Platnumz amb...
  • DAVIDO,TIWA SWAGE,DIAMOND, MR.FLAVOUR ON THE SHOOT,CHECK THE NEW VIDEO HERE
    Africa MultiChoice has launched it’s biggest  campaign yet, to celebrate Africa’s positivity , successes and the ability to  te...
  • Wayne Goss, former premier of Queensland, kicked the bucket at 63
    Mr Goss, who was premier from 1989 to 1996, had suffered from ill health in recent years including brain tumours. He became Q...
  • Third death confirmed in Mali The Pasteur Clinic in Bamako has been placed in quarantine and is under armed guard
      A nurse and the patient he was treating have become the second and third people to die from Ebola in Mali. The patient,...
  • The poorest president, Jose Mujica gets $1m offer for his VW Beetle
    7 November 2014 Last updated at 07:04 GMT Uruguay's President Jose Mujica says he has been offered $1m (£630,000) for his vinta...

LABELS

  • Breaking News
  • condolonces
  • Entertainment
  • Entertainments
  • Habari
  • Majonzi
  • Michezo
  • News
  • News and Updates
  • Skendo
  • Sports and Games
Submit ExpressSEO Services & Tools

Total Pageviews

Copyright 2014 Mwanafalsafa
Template By Ridwan Hex And Game Gratis