Mwanafalsafa

  • HOME
Home → Habari → Wafuasi hao watano wa chama cha demokrasia na maendeleo CHADEMA mkoani Morogoro waanzakusotea maandamano

Wafuasi hao watano wa chama cha demokrasia na maendeleo CHADEMA mkoani Morogoro waanzakusotea maandamano

Habari
Friday, 21 November 2014
SIKU moja baada ya Jeshi la Polisi kudhibiti maandamano yaliyoandaliwa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), wafuasi watatu wa chama hicho wamefikishwa mahakamani jijini Dar es Salaam na wengine watano wanashikiliwa na polisi mkoani Morogoro.

Wafuasi hao watano wa mkoani Morogoro wanashikiliwa na polisi wakidaiwa kupinga agizo lilitolewa na viongozi wa jeshi hilo la kuwataka kutoandamana.

Wanachama waliokamatwa ni pamoja na Witnes Makoyola (29), Katibu wa Chadema tawi la Kiwanja cha ndege, Shukuru Makamba(46), Maria Lissu (28) mkazi wa Kilakala na Katibu wa Baraza la Wanawake wilaya ya Morogoro Mjini, Hussein Hassani (28) mkazi wa Mafiga na Odwin Peter (65) mkazi wa Kiwanja cha ndege.

Akizungumza na waandishi wa habari jana, Kamanda wa Polisi mkoani Morogoro, Leonard Paul alisema tukio hilo lilitokea jana majira ya saa 5:30 asubuhi katika maeneo ya mtaa wa Konga.

Kamanda Paul alisema Septemba 17 viongozi wa chama hicho waliandika barua ya kuomba kuandamana, huku wakidai kuwa lengo la maandamano hayo ni kupinga hatua ya wabunge wa Bunge la Katiba kuendelea na vikao huku wakijua kuwa katiba haitapatikana.

Aidha Kamanda Paul alisema kuwa barua hizo zilienda kwa wakuu wa polisi na kwamba jeshi hilo lilizuia maandamano kutokana na taarifa za kiintelijensia kuwa wapo baadhi ya wananchi walipanga kufanya uhalifu wakati wa maandamano, ikiwa ni pamoja na kuwa kesi ya suala hilo bado iko mahakamani.

Hata hivyo, kamanda huyo alisema kuwa jeshi hilo liliwaita viongozi wa chama hicho, lengo likiwa ni kuwazuia kuandamana ambapo alisema kuwa jana majira ya saa 5:30 asubuhi katika maeneo ya mtaa wa Konga kulianza kufanyika mkusanyiko wa watu wakijiandaa kuandamana baada ya kuweka ulinzi katika maeneo yote waliyopanga kuanzia maandamano ya wafuasi wa chama hicho.

Hata hivyo, kamanda huyo alisema walifanikiwa kutawanya mkusanyiko huo kwa kurusha mabomu ya machozi sambamba na kuwakamata watuhumiwa hao ambapo alisema kuwa watafikishwa mahakamani muda wowote kuanzia sasa.

Kwa upande wake katibu wa chama hicho mkoani hapa, Boniface Ngonyani alisema kuwa maandamano hayo yaliyotarajiwa kufanyika jana majira ya saa 5.00 asubuhi yalizuiwa na jeshi la polisi ambapo jeshi hilo lilidaiwa kuingia ndani ya ofisi za chama hicho na kuanza kupekua nyaraka na kuzitwaa nyingine na kuondoka nazo.

Aidha alisema baada ya hekaheka hiyo baadae wakabaini kwamba kompyuta mpakato ya Mwenyekiti wa Chadema Wilaya, James Mkude pamoja na simu yake ya mkononi havionekani.

Hata hivyo, alisema kutokana na kukamatwa kwa wanachama hao ofisi ya Chadema mkoa wa Morogoro tayari imewatuma wanasheria wake wawili ili kuweza kufika polisi na kuangalia tatizo lililofanya kukamatwa kwa wanachama hao.

Na habari kutoka mkoani Dar es Salaam, wafuasi watatu wa Chadema wamefikishwa mahakamani kwa tuhuma za kuingia katika Makao Makuu ya Jeshi la Polisi kinyume na utaratibu.
Wafuasi hao ambao walifikishwa mahakamani hapo jana ni Ngaiza Kamugisha (28) dereva, mkazi wa Vingunguti, Benito Mwapinga (30) Fundi nguo mkazi wa Mtoni kwa Azzi Ally na Eliasante Bugeji (51) Mhasibu wa Hospitali ya CCBRT mkazi wa Komakoma Kinondoni, Dar es Salaam.

Akisoma hati ya mashitaka Wakili wa Serikali Mkuu, Bernard Kongola akisaidiana na Wakili wa Serikali Mwandamizi, Tumaini Kweka na George Barasa, ambapo alidai kuwa wafuasi hao wanakabiliwa na mashtaka matatu.

Mbele ya Hakimu Mkazi Frank Moshi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Kongola alidai mashtaka hayo ni kuingia kwa nguvu Makao Makuu ya Jeshi la Polisi, kukaidi amri halali na kutoa lugha ya matusi.

Ilidaiwa mahakamani hapo kuwa Septemba 18 mwaka huu, washtakiwa waliingia kinyume cha sheria ndani ya Makao Makuu ya Jeshi la Polisi kwa hali ya fujo.

Aidha, ilidaiwa katika tarehe hiyo na maeneo hayo washtakiwa walikataa kutii amri ya halali ya kutawanyika kutoka eneo la makao hayo ya polisi iliyotolewa na Mkaguzi wa Jeshi la Polisi, Inspekta Zuhura, ambaye alitoa amri hiyo baada ya kuruhusiwa na viongozi wake.

Akiendelea kusoma mashitaka hayo, alidai katika kosa la tatu linamkabili Bugeji peke yake, inadaiwa akiwa katika mazingira ya Makao Makuu ya Jeshi la Polisi alitoa lugha ya matusi kwa maofisa wa Polisi. Ilidaiwa maneno hayo yaliyotolewa na mshitakiwa huyo yalikuwa yakiashiria uvunjivu wa amani.

Upelelezi wa kesi hiyo umekamilika na upande wa mashitaka umeomba tarehe nyingine ya kuwasomea washtakiwa maelezo ya awali.

Wakili wa wafuasi hao Peter Kibatala alidai mashtaka yanayowakabili washtakiwa yanadhaminika, hivyo akaomba mahakama iwapatie masharti nafuu kwa mujibu wa sheria.

Hata hivyo, Kongola aliendelea kudai kuwa mahakama inatakiwa itoe masharti yanayoendana na mazingira ambayo washtakiwa wametenda kosa hilo. Kibatala alidai kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania dhamana ya washtakiwa ni haki yao na pia washtakiwa bado haijawatia hatiani, kwa hiyo dhamana ni haki yao.

Hakimu Moshi alisema ili washtakiwa wawe nje kwa dhamana wanatakiwa wawe na wadhamini wawili wa kuaminika wakiwemo watumishi wa Serikali au watumishi kutoka katika Taasisi inayotambulika wakiwa na barua za waajili wao na vitambulisho vya kazi na wadhamini watasaini bondi ya Sh 500,000 kwa kila mmoja.

Kesi hiyo iliahirishwa hadi Septemba 24 mwaka huu kwa washtakiwa kusomewa maelezo ya awali na akaamuru washtakiwa warudishwe rumande kwa sababu hawakuwa na wadhamini.

Mpaka gazeti hili linaondoka katika eneo la Mahakama washtakiwa walikuwa hawajapata dhamana, ambapo kulikuwa na jitihada za kupiga simu Makao Makuu ya Chadema ili wapate wadhamini.

Nje ya mahakama Mratibu wa Chadema Kanda ya Pwani, Nickson Tugala alikuwa aking'ang'ania kuingia mahabusu kuwaona washtakiwa, jambo ambalo lilisababisha fujo katika eneo hilo. Tugala alionekana kubishana na Insepkta wa Jeshi la Polisi, Mussa Mkini mpaka kufikia hatua ya kusogelea kwa karibu hali iliyowatia hofu watu waliyokuwa katika eneo hilo kuwa watu hao wanataka kupigana.

Kutokana na hali hiyo, ilimlazimu Mkini aombe nguvu kutoka Polisi na ilipofika saa 6:10 mchana ziliingia gari mbili za polisi namba PT 1846 na PT 1145 zikiwa na askari wenye silaha za moto. Mkini alitoa amri ya Tugala kuchukuliwa na kupelekwa Kituo Kikuu cha Polisi cha Mkoa wa Dar es Salaam kutokana na fujo ambazo alikuwa anafanya, lakini bado Tugala alikuwa akiwagomea askari hao.

Baadaye alikubali kuondoka nao, ambapo askari wawili walipanda kwenye gari ambalo alikuwa akiendesha la M4C namba T 351 CAY. Askari mmoja alipanda ndani ya gari na mwingine alipanda nyuma ya gari hilo wakiongoza kwenda Central.
Chanzo:Habarileo

Share this article :
Tweet
✚
Newer Post
Older Post
Home

HABARI ZILIZO BAMBA TOP 10

  • The World leaders are arriving in Australia for this weekend's G20 summit in the Queensland city of Brisbane.
      The two-day summit, attended by the US, Chinese and Russian leaders among others, will focus on promoting growth. Australian Pri...
  • Ronaldo aosha vyombo baada ya kushindwa katika karata na mchezaji wa Tenisi Rafa Nadal
    Ali...
  • In long, dimly lit hallways, clusters of people wait anxiously outside courtrooms for their cases to come before a judge.
    The New York Immigration Court is an extraordinarily busy place. In long, dimly lit hallways, clusters of people wait anxiously outside co...
  • Chinese leader Xi Jinping has urged Asia-Pacific nations to accelerate economic integration to spur global growth, on day two of the Apec summit.
    The high-level meeting includes the leaders of the US, Russia, China, Japan and others He spoke as leaders from the 21-na...
  • John Doar, a civil rights lawyer who was a key figure in the struggle against racial segregation in the US, has died aged 92.
    John Doar was awarded the Presidential Medal of Freedom in 2012 Mr Doar dealt with some of the most prominent civil rights ca...
  • Ukweli kuhusu umoja wa fedha,Jumuiya ya Afrika Mashariki.
      OKTOBA 20 hadi 24 mwaka  huu, Benki Kuu ya Tanzania (BoT) iliandaa semi...
  • Kiungo mpya wa Azam, Amri Kiemba akiwa katika jezi ya timu hiyo kwenye Uwanja wa Chamazi, Dar es Salaam jana
       Klabu ya Yanga imemleta nchini kwa majaribio mshambuliaji raia wa Zambia, Jonas Sakuwaha ...
  • Rais wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa ametunukiwa Tuzo ya Mafanikio Katika Utumishi wa Umma kutokana na mchango alioutoa kwenye uchumi wakati wa utawala wake.
      Kwa ufupi Kufanya kazi bila kuchoka, kusisitiza uwazi na ukweli katika kuboresha uchumi katika kipindi chake kwampaisha....
  • Dies aged 87,singing legend, Sabah, Lebanese
      Sabah was nicknamed "Shahroura", Arabic for "singing bird" by her mil...
  • Tatizo la kuwapo bandari bubu linazidi kuongezeka.
    Rais Jakaya Kikwete.PICHA|MAKTABA   Jeshi la Polisi mkoani Tanga ju...

LABELS

  • Breaking News
  • condolonces
  • Entertainment
  • Entertainments
  • Habari
  • Majonzi
  • Michezo
  • News
  • News and Updates
  • Skendo
  • Sports and Games
Submit ExpressSEO Services & Tools

Total Pageviews

Copyright 2014 Mwanafalsafa
Template By Ridwan Hex And Game Gratis