Mwanafalsafa

  • HOME
Home → Breaking News → TOKA DIAMOND AANZE MUZIKI HAPA NDIPO ALIPOFIKIA

TOKA DIAMOND AANZE MUZIKI HAPA NDIPO ALIPOFIKIA

Breaking News
Monday, 15 December 2014









WIKI iliyopita katika simulizi hii ya Diamond  tuliishia pale ambapo staa huyo aliongelea namna wimbo wake wa Mbagala ulivyopendwa kiasi cha kumfanya  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Kikwete ‘JK’ kumteua kuwa mburudishaji kwenye ziara za kampeni ya Uchaguzi Mkuu wa Rais, mwaka 2010.Wiki hii tunaendelea…

Mkali wa Bongo fleva Nasib Abdul Diamond Platinumz.  Oktoba 2, mwaka 2010, Diamond alipata safari yake ya kwanza kabisa ambapo alikwenda jijini London, Uingereza na kufanya shoo.Mwaka 2011, Diamond alishinda Tuzo ya
 Nzumari iliyotolea nchini Kenya akiwa Msanii Bora wa Kiume toka Tanzania.
Diamond aliweka rekodi ya msanii wa kwanza Bongo kufanya shoo kwenye Ukumbi wa Maisha Club jijini Dar na kujaza mashabiki wengi kiasi kwamba wengine walishindwa kuingia ndani ya ukumbi huo.
 AACHIA ALBAMU YA PILI
Ilikuwa Januari, 2012 Platnumz aliachia albamu yake ya pili  na kufikia rekodi ya kuwa msanii nambari wani Bongo kuuza kopi zaidi ya 1,200,000.
 Mwaka huohuo,  Diamond alifanya shoo bab’kubwa iliyoitwa Diamonds are forever iliyofanyika Ukumbi wa Mlimani City jijini Dar kwa kiinglio  cha shilingi 50,000. Diamond alikuwa peke yake na aliuza tiketi  zaidi 1,500.
 MSANII WA KWANZA BONGO KUSHUKA UWANJANI NA CHOPA
Mei, 2012, Diamond aliweka rekodi ya kuwa msanii wa kwanza kufanya shoo ya nguvu na kujaza zaidi ya watu 10,000 kwa kiingilio cha 20,000 ndani ya Uwanja wa Taifa wa Burudani wa Dar Live  huku akishuka uwanjani hapo na chopa (helikopta). Hata hivyo, Desemba 25, mwaka huu (Krismasi), Diamond atakuwepo tena ndani ya Dar Live!
 AENDA ULAYA, AKAMUA
Mwaka huohuo 2012,  Diamond alifanya
ziara Ulaya ambapo alitembelea nchi kadhaa kama Italia, Uholanzi, Sweden na Ugiriki, nako alifanya shoo za nguvu.
 Nyota ya 2012 ilizidi kuwa nzuri kwa Diamond kwani aliachia nyimbo mbili kwa mpigo, Nataka Kulewa na Kesho zilizoambata na video zake zenye ubora.
 AWA BALOZI
Mwanzoni mwa mwaka 2013, Diamond alichaguliwa kuwa balozi wa kampuni moja ya vinywaji baridi nchini na  kufanya ziara nchi za Afrika Mashariki, Burundi, DRC, Kenya, Uganda na Rwanda na kuwa msanii wa kwanza katika nchi za ukanda huo kupiga shoo peke yake kwenye uwanja na kujaza zaidi ya watu 30,000.
 ASHINDA TUZO TENA

June 2013, Diamond alishinda tuzo mbili  za Tanzania Kili
 Music Awards akiwa Msanii Bora wa Kiume wa Bongo Fleva
 na Msanii Bora  wa Kiume kwa wanamuziki wote nchini.
 NUMBER ONE

Julai 2013, Diamond  aliachia singo ya Number One ambayo 

video yake aliifanyia jijini Capetown, Afrika Kusini na 

Kampuni ya Ogopa Video. Aliweka rekodi ya kuwa msanii wa
 kwanza kuzindua video hiyo bila kiingilio ndani ya Hotel ya Serena na kuwaalika viongozi mbalimbali.
 Katika uzinduzi huo, Diamond alifanya tukio la kihistoria ambapo alimzawadia gari aina ya Totoya FunCargo aliyekuwa mwanamuziki nguli nchini, marehemu Muhidin Maalim Gurumo. 
Itaendelea wiki ijayo.







Share this article :
Tweet
✚
Newer Post
Older Post
Home

HABARI ZILIZO BAMBA TOP 10

  • The World leaders are arriving in Australia for this weekend's G20 summit in the Queensland city of Brisbane.
      The two-day summit, attended by the US, Chinese and Russian leaders among others, will focus on promoting growth. Australian Pri...
  • Ronaldo aosha vyombo baada ya kushindwa katika karata na mchezaji wa Tenisi Rafa Nadal
    Ali...
  • In long, dimly lit hallways, clusters of people wait anxiously outside courtrooms for their cases to come before a judge.
    The New York Immigration Court is an extraordinarily busy place. In long, dimly lit hallways, clusters of people wait anxiously outside co...
  • Chinese leader Xi Jinping has urged Asia-Pacific nations to accelerate economic integration to spur global growth, on day two of the Apec summit.
    The high-level meeting includes the leaders of the US, Russia, China, Japan and others He spoke as leaders from the 21-na...
  • John Doar, a civil rights lawyer who was a key figure in the struggle against racial segregation in the US, has died aged 92.
    John Doar was awarded the Presidential Medal of Freedom in 2012 Mr Doar dealt with some of the most prominent civil rights ca...
  • Ukweli kuhusu umoja wa fedha,Jumuiya ya Afrika Mashariki.
      OKTOBA 20 hadi 24 mwaka  huu, Benki Kuu ya Tanzania (BoT) iliandaa semi...
  • Kiungo mpya wa Azam, Amri Kiemba akiwa katika jezi ya timu hiyo kwenye Uwanja wa Chamazi, Dar es Salaam jana
       Klabu ya Yanga imemleta nchini kwa majaribio mshambuliaji raia wa Zambia, Jonas Sakuwaha ...
  • Rais wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa ametunukiwa Tuzo ya Mafanikio Katika Utumishi wa Umma kutokana na mchango alioutoa kwenye uchumi wakati wa utawala wake.
      Kwa ufupi Kufanya kazi bila kuchoka, kusisitiza uwazi na ukweli katika kuboresha uchumi katika kipindi chake kwampaisha....
  • Dies aged 87,singing legend, Sabah, Lebanese
      Sabah was nicknamed "Shahroura", Arabic for "singing bird" by her mil...
  • Tatizo la kuwapo bandari bubu linazidi kuongezeka.
    Rais Jakaya Kikwete.PICHA|MAKTABA   Jeshi la Polisi mkoani Tanga ju...

LABELS

  • Breaking News
  • condolonces
  • Entertainment
  • Entertainments
  • Habari
  • Majonzi
  • Michezo
  • News
  • News and Updates
  • Skendo
  • Sports and Games
Submit ExpressSEO Services & Tools

Total Pageviews

Copyright 2014 Mwanafalsafa
Template By Ridwan Hex And Game Gratis