Mwanafalsafa

  • HOME
Home → Habari → Ni haki kwa wenye mtindio wa ubongo kufungiwa kizazi ?

Ni haki kwa wenye mtindio wa ubongo kufungiwa kizazi ?

Habari
Friday, 5 December 2014










Watoto wenye akili taahira wakati mwingi hujipata tu wameshika mimba kwa kubakwa

Wakati dunia ilipoadhimisha siku ya Walemavu Duniani wiki hii, kilichozua mjadala nchini Kenya ni iwapo ni haki kwa mzazi au mfadhili wa mtoto mwenye akili taahira kumfungza kizazi ili asiweze kuzaa kabisa.
Ingawa kuna wale wanaosema kwamba ni haki ya kimsingi kwa mtu mwenye akili taahira kufurahia tendo la ngono na hata kuzaa kuna wengine wanaosema kuwa kwa kuwa wao hawawezi kujitunza wenyewe wala hawana ufahamu wa kuamua kilicho bora kwao wasiruhusiwe kujitwika mzigo wa ziada.
Mwandishi wa BBC Muliro Telewa aLIsafiri hadi Magharibi mwa Kenya kujionea hali inayowakumba wasichana wengi wenye akili taahira.
Katika kituo cha Kona mbaya katika eneo la Likuyani, Kaunti ya Kakamega, nilimpata mwanamke mwenye akilia taahira, mwenye umri wa miaka thelathini nilipoingia katika nyumba yake ya vyumba viwili.
Alikuwa ameketi kwenye kiti kirefu akiwa amebanwa kwa upande mmoja na mama yake mzazi, mwenye umri wa miaka 83 na upande mwingine na dada yake mwenye umri wa miaka 40, Annet Nekesa Ngosia.
Mwanamke huyo alitutizama kwa hofu na kuchanganyikiwa usoni mwake.
Hata hivyo dada yake Nekesa, alimwagiza atabasamu kidogo kwa kuwa sisi ni wapiga picha. Alitabasamu kwa muda mfupi tu lakini baada ya dakika moja uso wake ukarejelea picha ya awali. Dada yake Annet Nekesa Ngosia aliendelea kuelezea.
''Ikiwa yeye mwenyewe hawezi kujitunza, atatuza vipi mtoto wake bila kusaidiwa? watu kama hawa wanapaswa kufungwa kizazi. Iangwa anelewa ni kinyume na mafunzo ya biblia, uhalisia wa maisha ya sasa ndio unatuongoza. Mimi siwezi hata kufikia kuhusu kufungwa kizazi na pia ni vigumu kuwaelewa watu hawa labda na wao wana hisia na wangetaka k
upata watoto na hata kuwa na familia, ''anasema Nekesa.

Nekesa anasema ni vigumu kusema kuwa wafungwe kizazi lakini wenyewe hawawezi kuwalea watoto bila kusaidiwa

Mwanamke huyo mwenye akili taahira alikuwa amevalia rinda la bluu lililokuwa limefungiwa kifuani mwake kwa uzi.
Nilipomtizama usoni alionekana kama anayefuatilia tunayozungumza na kwa hivyo nikamwuliza iwapo anamjua mtoto wake akawa hana habari kulihusu hilo.
Alinielekeza kwa mkono wake alikokuwa msichana mrembo aliyekuwa ametoboa masikio yake yaliyokuwa hayajapona vizuri.
Anapofanya hivyo anatabasamu kidogo. Msichana huyo anasongea karibu nami ninapomwelekeza kufanya hivyo. Ananiambia jina lake na kunielezea zaidi.Nilipomuuliza ikiwa anamfahamu mtoto wake, alitabasamu tu.
Na mwendo wa kilomita 10 hivi kutoka aliko mama huyu, katika Kituo cha Biashara cha Moi’s Bridge, nilikutana na Bwana Daniel Mutimba, aliye na mtoto mvulana mwenye umri wa miaka 10 mwenye akili taahira.
Msimamo wake juu ya kuwafunga kizazi watoto wa aina hiyo unahitilafiana na ule wa Nekesa.
Dakitari bingwa wa maradhi ya akili katika hospitali ya Mafunzo na Rufaa ya Moi, mjini Eldoret, Edith Kwoba, alisema kuwa utafiti uliofanywa nchini Kenya unathibitisha kuwa asilimia 25 ya watu milioni 40 walioko nchini Kenya wana maradhiya akili ingawa wengi wao hawayajui.
Anaunga mkono kuwasimamisha uzazi wagonjwa wa akili:
Lakini Mkereketwa na mwalimu wa watoto wenye akili taahira, Mwaliumu Mkuu wa shule ya mtakatifu Vincent De Paul katika eneo la Likuyani, kaunti ya Kakamega, Bwna Konyango John Paul, anasema haki za kimsingi za watoto wenye akili taahira lazima zilindwe:
Sheria nchini Kenya hazielezi kikamilifu iwapo wagonjwa wanapaswa kukatizwa uzazi. Kwa sasa kuna kundi la kina mama walio na virusi vya HIV ambao wamefika mahakamani kuwashtaki baadhi ya madaktari kwa kuwafunga kizazi bila kuwafahamisha miaka ya 80.
Huku mjadala huo ukiendelea miongoni mwa wanaohusiana na wagonjwa wa akili taahira, msichana mwenye umri wa miaka 11 yungali anasubiri mama yake apone, huku yeye akizidi kufanya kazi badala ya kucheza kama watoto wenzake.








Share this article :
Tweet
✚
Newer Post
Older Post
Home

HABARI ZILIZO BAMBA TOP 10

  • Umuhimu wa kushirikiana katika kazi hasa ya muziki
  • After more than two years of tension over a territorial row,the leaders of China and Japan hold formal talks on the sidelines of a major Asian summit.
    Chinese President Xi Jinping and Japanese PM Shinzo Abe met on the sidelines of the Asia-Pacific Economic Co-operation (Apec) summit in B...
  • MAREKANI YAITUPIA LAWAMA KOREA KASKAZINI
    Marekani inatarajia kuirudisha Korea kaskazini katika orodha ya nchi zinazofadhili ugaidi. Rais Barack Obama wa Marekani amesema utawala ...
  • AJIITA KIJANA MWENYE BAHATI AKIWA KATIKATI YA WAREMBO WAWILI
  • The actress best known for playing the unseen role of Howard Wolowitz's mother on The Big Bang Theory has died.
      Big Bang Theory's Mrs Wolowitz dies at the age of 62 Carol Ann Susi had played the role of Mrs Wolowitz since 2007   ...
  • Al Shabaab kero kubwa kwa wakenya
    Tazama picha hapa 4 Disemba 2014 Imebadilishwa mwisho saa 11:29 GMT Nchi yetu na watu wetu wanashambuliwa" Haya ni maneno ya...
  • Mombasa based singer akothee gets naughty,Angalia hapa
  • Sintofahamu yaibuka juu ya maelezo ya kifo cha aliyekuwa mshitakiwa wa ugaidi.
    WAKATI Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha ikielezwa kuwa taratibu za mazishi ya mtuhumiwa wa pili katika kesi ya ugaidi ya tukio la mli...
  • MKURUGENZI wa Ulinzi na Usalama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Wilfred Lwakatare, Aiburuza serikali mahakamani.
    ameshinda rufaa ya maombi ya marejeo yaliyowasilishwa na Serikali kupinga uamuzi wa Mahakama Kuu ya Tanzania kumfutia mashitaka ya ugai...
  • Former Youth Fund CEO, Evans Gor Semalang’o, Look at these cute pics.
    Former Youth Fund CEO, Evans Gor Semalang’o, claims that former Prime Minister Raila Odinga may have gone mad after he said that he...

LABELS

  • Breaking News
  • condolonces
  • Entertainment
  • Entertainments
  • Habari
  • Majonzi
  • Michezo
  • News
  • News and Updates
  • Skendo
  • Sports and Games
Submit ExpressSEO Services & Tools

Total Pageviews

Copyright 2014 Mwanafalsafa
Template By Ridwan Hex And Game Gratis