Mwanafalsafa

  • HOME
Home → Habari → Ni haki kwa wenye mtindio wa ubongo kufungiwa kizazi ?

Ni haki kwa wenye mtindio wa ubongo kufungiwa kizazi ?

Habari
Friday, 5 December 2014










Watoto wenye akili taahira wakati mwingi hujipata tu wameshika mimba kwa kubakwa

Wakati dunia ilipoadhimisha siku ya Walemavu Duniani wiki hii, kilichozua mjadala nchini Kenya ni iwapo ni haki kwa mzazi au mfadhili wa mtoto mwenye akili taahira kumfungza kizazi ili asiweze kuzaa kabisa.
Ingawa kuna wale wanaosema kwamba ni haki ya kimsingi kwa mtu mwenye akili taahira kufurahia tendo la ngono na hata kuzaa kuna wengine wanaosema kuwa kwa kuwa wao hawawezi kujitunza wenyewe wala hawana ufahamu wa kuamua kilicho bora kwao wasiruhusiwe kujitwika mzigo wa ziada.
Mwandishi wa BBC Muliro Telewa aLIsafiri hadi Magharibi mwa Kenya kujionea hali inayowakumba wasichana wengi wenye akili taahira.
Katika kituo cha Kona mbaya katika eneo la Likuyani, Kaunti ya Kakamega, nilimpata mwanamke mwenye akilia taahira, mwenye umri wa miaka thelathini nilipoingia katika nyumba yake ya vyumba viwili.
Alikuwa ameketi kwenye kiti kirefu akiwa amebanwa kwa upande mmoja na mama yake mzazi, mwenye umri wa miaka 83 na upande mwingine na dada yake mwenye umri wa miaka 40, Annet Nekesa Ngosia.
Mwanamke huyo alitutizama kwa hofu na kuchanganyikiwa usoni mwake.
Hata hivyo dada yake Nekesa, alimwagiza atabasamu kidogo kwa kuwa sisi ni wapiga picha. Alitabasamu kwa muda mfupi tu lakini baada ya dakika moja uso wake ukarejelea picha ya awali. Dada yake Annet Nekesa Ngosia aliendelea kuelezea.
''Ikiwa yeye mwenyewe hawezi kujitunza, atatuza vipi mtoto wake bila kusaidiwa? watu kama hawa wanapaswa kufungwa kizazi. Iangwa anelewa ni kinyume na mafunzo ya biblia, uhalisia wa maisha ya sasa ndio unatuongoza. Mimi siwezi hata kufikia kuhusu kufungwa kizazi na pia ni vigumu kuwaelewa watu hawa labda na wao wana hisia na wangetaka k
upata watoto na hata kuwa na familia, ''anasema Nekesa.

Nekesa anasema ni vigumu kusema kuwa wafungwe kizazi lakini wenyewe hawawezi kuwalea watoto bila kusaidiwa

Mwanamke huyo mwenye akili taahira alikuwa amevalia rinda la bluu lililokuwa limefungiwa kifuani mwake kwa uzi.
Nilipomtizama usoni alionekana kama anayefuatilia tunayozungumza na kwa hivyo nikamwuliza iwapo anamjua mtoto wake akawa hana habari kulihusu hilo.
Alinielekeza kwa mkono wake alikokuwa msichana mrembo aliyekuwa ametoboa masikio yake yaliyokuwa hayajapona vizuri.
Anapofanya hivyo anatabasamu kidogo. Msichana huyo anasongea karibu nami ninapomwelekeza kufanya hivyo. Ananiambia jina lake na kunielezea zaidi.Nilipomuuliza ikiwa anamfahamu mtoto wake, alitabasamu tu.
Na mwendo wa kilomita 10 hivi kutoka aliko mama huyu, katika Kituo cha Biashara cha Moi’s Bridge, nilikutana na Bwana Daniel Mutimba, aliye na mtoto mvulana mwenye umri wa miaka 10 mwenye akili taahira.
Msimamo wake juu ya kuwafunga kizazi watoto wa aina hiyo unahitilafiana na ule wa Nekesa.
Dakitari bingwa wa maradhi ya akili katika hospitali ya Mafunzo na Rufaa ya Moi, mjini Eldoret, Edith Kwoba, alisema kuwa utafiti uliofanywa nchini Kenya unathibitisha kuwa asilimia 25 ya watu milioni 40 walioko nchini Kenya wana maradhiya akili ingawa wengi wao hawayajui.
Anaunga mkono kuwasimamisha uzazi wagonjwa wa akili:
Lakini Mkereketwa na mwalimu wa watoto wenye akili taahira, Mwaliumu Mkuu wa shule ya mtakatifu Vincent De Paul katika eneo la Likuyani, kaunti ya Kakamega, Bwna Konyango John Paul, anasema haki za kimsingi za watoto wenye akili taahira lazima zilindwe:
Sheria nchini Kenya hazielezi kikamilifu iwapo wagonjwa wanapaswa kukatizwa uzazi. Kwa sasa kuna kundi la kina mama walio na virusi vya HIV ambao wamefika mahakamani kuwashtaki baadhi ya madaktari kwa kuwafunga kizazi bila kuwafahamisha miaka ya 80.
Huku mjadala huo ukiendelea miongoni mwa wanaohusiana na wagonjwa wa akili taahira, msichana mwenye umri wa miaka 11 yungali anasubiri mama yake apone, huku yeye akizidi kufanya kazi badala ya kucheza kama watoto wenzake.








Share this article :
Tweet
✚
Newer Post
Older Post
Home

HABARI ZILIZO BAMBA TOP 10

  • Takribani watu 15 wapata upofu baada ya upasuaji nchini India
    Wagonjwa waliofanyiwa upasuaji walisema walishindwa kuona tena baada ya kuondoa bandeji kwenye macho yao Maafisa wa utawala nchini Indiaa w...
  • Familia ya mateka yasihi Al Qaeda kumwachilia
    Marekani imeeleza kuwa ilijaribu kumwokoa raia wake mzaliwa wa Uingereza Luke Somers, anayeshikiliwa mateka na al-Qaeda nchini Yemen. ...
  • Ona kilichotokea kwa jimama hili kipindi lina jaribu kucheza jirani na swimming pool.Noii huko Kenya mida ya jana jioni
       
  • AJIITA KIJANA MWENYE BAHATI AKIWA KATIKATI YA WAREMBO WAWILI
  • BRAZIL TO EDGE OUT GERMANY IN WORLD CUP SEMI FINAL
  • KAULI YA UHURU KWENYE MTANDAOWA KIJAMII (TWITTER) KENYATTA HII HAPA
    Taarifa ya mahakama ya ICC, kutupilia mbali kesi dhidi ya Uhuru Kenyatta, imepokelwa na watu wengi nchini Kenya kwa hisia mseto. Baadhi w...
  • Maandano zidi ya kutupiliwa mbali kwa kesi ya afisa polisi mjini New York
    Maandamano mjini New York Waandamanaji wameingia katika barabara za miji mingi Nchini Marekani kwa usiku wa pili mtawalia, kupinga maamu...
  • Jennifer Lawrence has joined her castmates at the world premiere of the penultimate Hunger Games movie, Mockingjay Part 1, in London.
    Lawrence plays the heroine Katniss Everdeen in the hit franchise Jennifer Lawrence has joined her castmates at the w...
  • MORE THAN 10,000 GRADUATES TURN UP FOR SEVENTY JOB VACANCIES IN DAR ES SLAAM.
    According to the list of names seen by The Guardian yesterday morning, the department listed 10,816 candidates to perform the interview tha...
  • Mshindi wa Nishani ya Nobel bint Malala amenukuliwa akisema "Nataka kuwa Waziri mkuu''
    Mshindi wa Nishani ya Nobel bint Malala Yousafzai raia wa Pakistani amesema kuwa siku zijazo anatarajia kuwa mwanasiasa. Malala a...

LABELS

  • Breaking News
  • condolonces
  • Entertainment
  • Entertainments
  • Habari
  • Majonzi
  • Michezo
  • News
  • News and Updates
  • Skendo
  • Sports and Games
Submit ExpressSEO Services & Tools

Total Pageviews

Copyright 2014 Mwanafalsafa
Template By Ridwan Hex And Game Gratis