Mwanafalsafa

  • HOME
Home → Entertainments → Je . . . ., Kushiriki tendo la ndoa ni hobi ya mtu ?

Je . . . ., Kushiriki tendo la ndoa ni hobi ya mtu ?

Entertainments
Wednesday, 31 December 2014







Mara kwa mara utakuwa umekutana na marafiki wanaozungumza maneno mengi kuhusu ngono. Baadhi wanapozungumza, wanaonyesha wazi kutopendezwa na hali yao ya kupenda ngono kupita kiasi, lakini wengine huongea kwa kujisifu kwa vile ni mahodari wa kushiriki tendo lile.
Wanaojisifu, ndiyo hawa huja na kauli kuwa wao hobi yao ni mapenzi. Neno hili, hobi, ni la kiingereza linalomaanisha kitu ambacho mtu anakipenda. Mtu atasema hobi yake ni kusoma, mwingine michezo au muziki na kadhalika. Kila mmoja anacho akipendacho, yaani akikipata hicho, roho yake inakuwa raha burudani.
Katika siku za hivi karibuni nimeshuhudia mastaa wawili wakizungumzia ngono, ambao ni Elizabeth Michael ‘Lulu’ na Baby Madaha. Lulu alisema ngono zimekuwa zikimtesa kiasi kwamba kila mara hujikuta katika hali ya kutaka kufanya mapenzi, kitu ambacho mwenyewe anaamini ana jini mahaba.
Kwa upande wake, Baby Madaha yeye anakuja live kabisa akidai kwamba, kwake yeye, kufanya mapenzi ni hobi yake, yaani ndicho kitu anachokipenda kuliko vitu vingine vyote duniani, yaani kwake yeye, kushiriki tendo akiwa na mwenzi wake ndo faraja yake.
Wazungu wana msemo wao mmoja maarufu unaosema too much of anything is harmful, kwa tafsiri isiyo rasmi ni kwamba kitu chochote ukikizidisha, kitakupatia madhara.
Kushiriki tendo la ndoa ni kitu kinachofurahiwa na wengi, wake kwa waume, ingawa kila mmoja ana aina ya ufurahiaji wake. Wapo wanaozidisha ufanyaji wa tendo hili kutokana na sababu mbalimbali. Kuna wanaofanya hivi ili kujipatia kipato. Anakesha usiku kucha akibadilisha wanaume kwa ajili ya kipato.
Lakini wapo ambao wanapenda kushiriki tendo kwa sababu ya raha tu na siyo kingine. Kwa wote wenye aina hii ya mahitaji, wanaambiwa kuwa wana pepo la ngono!Sisemi kuhusu machangudoa, kwa sababu wote tunajua kuwa hawa wanafanya hivi ili kupata hela, nazungumza na wanawake na wanaume ambao muda wote wanawaza ngono na hata wakifanya hawaridhiki. Anatoka kuchepuka sehemu, lakini anapopanda kwenye daladala macho yake yanavutiwa na mwanamke mwingine na yupo tayari kumtongoza na kulazimisha kwenda naye muda uleule.
Ukimuona mtu wa aina hii, ni wa kumsaidia kwa sababu huo ni ugonjwa. Binadamu anao uwezo mkubwa wa kuhimili hisia za mapenzi yake. Wale waliooa au kuolewa wanaweza kuwa mashahidi wazuri wa hili. Unaweza kukuta wanandoa wanakaa hata wiki mbili bila kukutana, ingawa wanalala kitanda kimoja.
Tendo la ndoa ni kitu cha afya. Mwili hujiweka vizuri zaidi kwa ushiriki wake, lakini unapozidisha dozi, ni tatizo. Ugonjwa huu unatibika, nenda hospitali, onana na daktari bingwa wa saikolojia, atakueleza kwa nini unakuwa hivyo ulivyo na nini suluhisho la kudumu.






Share this article :
Tweet
✚
Newer Post
Older Post
Home

HABARI ZILIZO BAMBA TOP 10

  • Lorna Rutto is an entrepreneur who founded Ecopost, a Nairobi-based company that recycles plastic waste
    Lorna Rutto is an entrepreneur who founded Ecopost, a Nairobi-based company that recycles plastic waste. As part of the latest series o...
  • Wabunge wa Somali wameng'oa waziri mkuu
    Ni mara ya nne kwamba kura ya kutokuwa na imani dhidi yake ilipigwa baada ya majaribio ya awali kumalizika kwa ghasia. Waandishi ...
  • AJIITA KIJANA MWENYE BAHATI AKIWA KATIKATI YA WAREMBO WAWILI
  • John Doar, a civil rights lawyer who was a key figure in the struggle against racial segregation in the US, has died aged 92.
    John Doar was awarded the Presidential Medal of Freedom in 2012 Mr Doar dealt with some of the most prominent civil rights ca...
  • Ukweli kuhusu umoja wa fedha,Jumuiya ya Afrika Mashariki.
      OKTOBA 20 hadi 24 mwaka  huu, Benki Kuu ya Tanzania (BoT) iliandaa semi...
  • BRAZIL TO EDGE OUT GERMANY IN WORLD CUP SEMI FINAL
  • Chuo kikuu cha ardhi ARU chatoa zawadi kwa wanafunzi 30, mmoja, ambae ni muhitimu wa masomo ya surveying aibuka na machine ya millioni 35
    CHUO Kikuu Ardhi (ARU), kimewazawadia wanafuzi 130 wa masomo mbalimbali zawadi zenye thamani ya zaidi ya sh milioni 60 kutokana n...
  • Ajali ya gari huko south B kenya
    There was a bizarre accident today morning in Hazina Estate, South B involving a Range Rover that crashed into 7 vehicles. The Ran...
  • Jennifer Lawrence has joined her castmates at the world premiere of the penultimate Hunger Games movie, Mockingjay Part 1, in London.
    Lawrence plays the heroine Katniss Everdeen in the hit franchise Jennifer Lawrence has joined her castmates at the w...
  • Arsenal yamlenga Kramer anaechezea klabu ya Borussia Monchengladbach
    Arsenal wako tayari kutoa p...

LABELS

  • Breaking News
  • condolonces
  • Entertainment
  • Entertainments
  • Habari
  • Majonzi
  • Michezo
  • News
  • News and Updates
  • Skendo
  • Sports and Games
Submit ExpressSEO Services & Tools

Total Pageviews

Copyright 2014 Mwanafalsafa
Template By Ridwan Hex And Game Gratis