Mwanafalsafa

  • HOME
Home → Entertainments → Je . . . ., Kushiriki tendo la ndoa ni hobi ya mtu ?

Je . . . ., Kushiriki tendo la ndoa ni hobi ya mtu ?

Entertainments
Wednesday, 31 December 2014







Mara kwa mara utakuwa umekutana na marafiki wanaozungumza maneno mengi kuhusu ngono. Baadhi wanapozungumza, wanaonyesha wazi kutopendezwa na hali yao ya kupenda ngono kupita kiasi, lakini wengine huongea kwa kujisifu kwa vile ni mahodari wa kushiriki tendo lile.
Wanaojisifu, ndiyo hawa huja na kauli kuwa wao hobi yao ni mapenzi. Neno hili, hobi, ni la kiingereza linalomaanisha kitu ambacho mtu anakipenda. Mtu atasema hobi yake ni kusoma, mwingine michezo au muziki na kadhalika. Kila mmoja anacho akipendacho, yaani akikipata hicho, roho yake inakuwa raha burudani.
Katika siku za hivi karibuni nimeshuhudia mastaa wawili wakizungumzia ngono, ambao ni Elizabeth Michael ‘Lulu’ na Baby Madaha. Lulu alisema ngono zimekuwa zikimtesa kiasi kwamba kila mara hujikuta katika hali ya kutaka kufanya mapenzi, kitu ambacho mwenyewe anaamini ana jini mahaba.
Kwa upande wake, Baby Madaha yeye anakuja live kabisa akidai kwamba, kwake yeye, kufanya mapenzi ni hobi yake, yaani ndicho kitu anachokipenda kuliko vitu vingine vyote duniani, yaani kwake yeye, kushiriki tendo akiwa na mwenzi wake ndo faraja yake.
Wazungu wana msemo wao mmoja maarufu unaosema too much of anything is harmful, kwa tafsiri isiyo rasmi ni kwamba kitu chochote ukikizidisha, kitakupatia madhara.
Kushiriki tendo la ndoa ni kitu kinachofurahiwa na wengi, wake kwa waume, ingawa kila mmoja ana aina ya ufurahiaji wake. Wapo wanaozidisha ufanyaji wa tendo hili kutokana na sababu mbalimbali. Kuna wanaofanya hivi ili kujipatia kipato. Anakesha usiku kucha akibadilisha wanaume kwa ajili ya kipato.
Lakini wapo ambao wanapenda kushiriki tendo kwa sababu ya raha tu na siyo kingine. Kwa wote wenye aina hii ya mahitaji, wanaambiwa kuwa wana pepo la ngono!Sisemi kuhusu machangudoa, kwa sababu wote tunajua kuwa hawa wanafanya hivi ili kupata hela, nazungumza na wanawake na wanaume ambao muda wote wanawaza ngono na hata wakifanya hawaridhiki. Anatoka kuchepuka sehemu, lakini anapopanda kwenye daladala macho yake yanavutiwa na mwanamke mwingine na yupo tayari kumtongoza na kulazimisha kwenda naye muda uleule.
Ukimuona mtu wa aina hii, ni wa kumsaidia kwa sababu huo ni ugonjwa. Binadamu anao uwezo mkubwa wa kuhimili hisia za mapenzi yake. Wale waliooa au kuolewa wanaweza kuwa mashahidi wazuri wa hili. Unaweza kukuta wanandoa wanakaa hata wiki mbili bila kukutana, ingawa wanalala kitanda kimoja.
Tendo la ndoa ni kitu cha afya. Mwili hujiweka vizuri zaidi kwa ushiriki wake, lakini unapozidisha dozi, ni tatizo. Ugonjwa huu unatibika, nenda hospitali, onana na daktari bingwa wa saikolojia, atakueleza kwa nini unakuwa hivyo ulivyo na nini suluhisho la kudumu.






Share this article :
Tweet
✚
Newer Post
Older Post
Home

HABARI ZILIZO BAMBA TOP 10

  • The World leaders are arriving in Australia for this weekend's G20 summit in the Queensland city of Brisbane.
      The two-day summit, attended by the US, Chinese and Russian leaders among others, will focus on promoting growth. Australian Pri...
  • Ronaldo aosha vyombo baada ya kushindwa katika karata na mchezaji wa Tenisi Rafa Nadal
    Ali...
  • In long, dimly lit hallways, clusters of people wait anxiously outside courtrooms for their cases to come before a judge.
    The New York Immigration Court is an extraordinarily busy place. In long, dimly lit hallways, clusters of people wait anxiously outside co...
  • Chinese leader Xi Jinping has urged Asia-Pacific nations to accelerate economic integration to spur global growth, on day two of the Apec summit.
    The high-level meeting includes the leaders of the US, Russia, China, Japan and others He spoke as leaders from the 21-na...
  • John Doar, a civil rights lawyer who was a key figure in the struggle against racial segregation in the US, has died aged 92.
    John Doar was awarded the Presidential Medal of Freedom in 2012 Mr Doar dealt with some of the most prominent civil rights ca...
  • Ukweli kuhusu umoja wa fedha,Jumuiya ya Afrika Mashariki.
      OKTOBA 20 hadi 24 mwaka  huu, Benki Kuu ya Tanzania (BoT) iliandaa semi...
  • Kiungo mpya wa Azam, Amri Kiemba akiwa katika jezi ya timu hiyo kwenye Uwanja wa Chamazi, Dar es Salaam jana
       Klabu ya Yanga imemleta nchini kwa majaribio mshambuliaji raia wa Zambia, Jonas Sakuwaha ...
  • Rais wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa ametunukiwa Tuzo ya Mafanikio Katika Utumishi wa Umma kutokana na mchango alioutoa kwenye uchumi wakati wa utawala wake.
      Kwa ufupi Kufanya kazi bila kuchoka, kusisitiza uwazi na ukweli katika kuboresha uchumi katika kipindi chake kwampaisha....
  • Dies aged 87,singing legend, Sabah, Lebanese
      Sabah was nicknamed "Shahroura", Arabic for "singing bird" by her mil...
  • Tatizo la kuwapo bandari bubu linazidi kuongezeka.
    Rais Jakaya Kikwete.PICHA|MAKTABA   Jeshi la Polisi mkoani Tanga ju...

LABELS

  • Breaking News
  • condolonces
  • Entertainment
  • Entertainments
  • Habari
  • Majonzi
  • Michezo
  • News
  • News and Updates
  • Skendo
  • Sports and Games
Submit ExpressSEO Services & Tools

Total Pageviews

Copyright 2014 Mwanafalsafa
Template By Ridwan Hex And Game Gratis