Mwanafalsafa

  • HOME
Home → Entertainments → Je . . . ., Kushiriki tendo la ndoa ni hobi ya mtu ?

Je . . . ., Kushiriki tendo la ndoa ni hobi ya mtu ?

Entertainments
Wednesday, 31 December 2014







Mara kwa mara utakuwa umekutana na marafiki wanaozungumza maneno mengi kuhusu ngono. Baadhi wanapozungumza, wanaonyesha wazi kutopendezwa na hali yao ya kupenda ngono kupita kiasi, lakini wengine huongea kwa kujisifu kwa vile ni mahodari wa kushiriki tendo lile.
Wanaojisifu, ndiyo hawa huja na kauli kuwa wao hobi yao ni mapenzi. Neno hili, hobi, ni la kiingereza linalomaanisha kitu ambacho mtu anakipenda. Mtu atasema hobi yake ni kusoma, mwingine michezo au muziki na kadhalika. Kila mmoja anacho akipendacho, yaani akikipata hicho, roho yake inakuwa raha burudani.
Katika siku za hivi karibuni nimeshuhudia mastaa wawili wakizungumzia ngono, ambao ni Elizabeth Michael ‘Lulu’ na Baby Madaha. Lulu alisema ngono zimekuwa zikimtesa kiasi kwamba kila mara hujikuta katika hali ya kutaka kufanya mapenzi, kitu ambacho mwenyewe anaamini ana jini mahaba.
Kwa upande wake, Baby Madaha yeye anakuja live kabisa akidai kwamba, kwake yeye, kufanya mapenzi ni hobi yake, yaani ndicho kitu anachokipenda kuliko vitu vingine vyote duniani, yaani kwake yeye, kushiriki tendo akiwa na mwenzi wake ndo faraja yake.
Wazungu wana msemo wao mmoja maarufu unaosema too much of anything is harmful, kwa tafsiri isiyo rasmi ni kwamba kitu chochote ukikizidisha, kitakupatia madhara.
Kushiriki tendo la ndoa ni kitu kinachofurahiwa na wengi, wake kwa waume, ingawa kila mmoja ana aina ya ufurahiaji wake. Wapo wanaozidisha ufanyaji wa tendo hili kutokana na sababu mbalimbali. Kuna wanaofanya hivi ili kujipatia kipato. Anakesha usiku kucha akibadilisha wanaume kwa ajili ya kipato.
Lakini wapo ambao wanapenda kushiriki tendo kwa sababu ya raha tu na siyo kingine. Kwa wote wenye aina hii ya mahitaji, wanaambiwa kuwa wana pepo la ngono!Sisemi kuhusu machangudoa, kwa sababu wote tunajua kuwa hawa wanafanya hivi ili kupata hela, nazungumza na wanawake na wanaume ambao muda wote wanawaza ngono na hata wakifanya hawaridhiki. Anatoka kuchepuka sehemu, lakini anapopanda kwenye daladala macho yake yanavutiwa na mwanamke mwingine na yupo tayari kumtongoza na kulazimisha kwenda naye muda uleule.
Ukimuona mtu wa aina hii, ni wa kumsaidia kwa sababu huo ni ugonjwa. Binadamu anao uwezo mkubwa wa kuhimili hisia za mapenzi yake. Wale waliooa au kuolewa wanaweza kuwa mashahidi wazuri wa hili. Unaweza kukuta wanandoa wanakaa hata wiki mbili bila kukutana, ingawa wanalala kitanda kimoja.
Tendo la ndoa ni kitu cha afya. Mwili hujiweka vizuri zaidi kwa ushiriki wake, lakini unapozidisha dozi, ni tatizo. Ugonjwa huu unatibika, nenda hospitali, onana na daktari bingwa wa saikolojia, atakueleza kwa nini unakuwa hivyo ulivyo na nini suluhisho la kudumu.






Share this article :
Tweet
✚
Newer Post
Older Post
Home

HABARI ZILIZO BAMBA TOP 10

  • MAREKANI YAITUPIA LAWAMA KOREA KASKAZINI
    Marekani inatarajia kuirudisha Korea kaskazini katika orodha ya nchi zinazofadhili ugaidi. Rais Barack Obama wa Marekani amesema utawala ...
  • Mombasa based singer akothee gets naughty,Angalia hapa
  • Vita dhidi ya Ukimwi zashika kasi, mbinu madhubuti zachukuliwa !
    DESEMBA mosi, kila mwaka, watu wote duniani huadhimisha Siku ya Ukimwi Duniani. Siku hiyo ilianzishwa mwaka 1987 na hubeba maudhui mbalim...
  • ,Juncker reveals giant EU investment planJuncker said Europe needed a kick-start and the Commission was offering the jump-leads
    Mr  European Commission President Jean-Claude Juncker has given details of a €315bn (£250bn;$393bn) investment plan to kic...
  • Kwaninii serikali imewekeza katika siasa na imesahau wakulima ?
      Hata hivyo, wakulima wamekwazwa na kodi nyingi wanazotozwa kwa kila gunia inapotokea wakauza sehemu ya ...
  • Mdogo wa Zari Hassan apaka matope uhusiano wake na Diamond
    Mdogo wake na Zari Hassan aka The Bosslady, aitwaye Karim ametumia Facebook kumkosoa dada yake kwa kuwa na uhusiano na Diamond Platnumz amb...
  • DAVIDO,TIWA SWAGE,DIAMOND, MR.FLAVOUR ON THE SHOOT,CHECK THE NEW VIDEO HERE
    Africa MultiChoice has launched it’s biggest  campaign yet, to celebrate Africa’s positivity , successes and the ability to  te...
  • Wayne Goss, former premier of Queensland, kicked the bucket at 63
    Mr Goss, who was premier from 1989 to 1996, had suffered from ill health in recent years including brain tumours. He became Q...
  • Third death confirmed in Mali The Pasteur Clinic in Bamako has been placed in quarantine and is under armed guard
      A nurse and the patient he was treating have become the second and third people to die from Ebola in Mali. The patient,...
  • The poorest president, Jose Mujica gets $1m offer for his VW Beetle
    7 November 2014 Last updated at 07:04 GMT Uruguay's President Jose Mujica says he has been offered $1m (£630,000) for his vinta...

LABELS

  • Breaking News
  • condolonces
  • Entertainment
  • Entertainments
  • Habari
  • Majonzi
  • Michezo
  • News
  • News and Updates
  • Skendo
  • Sports and Games
Submit ExpressSEO Services & Tools

Total Pageviews

Copyright 2014 Mwanafalsafa
Template By Ridwan Hex And Game Gratis